Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Gari ya mizigo/biashara kwa beginner yeyote usijelogwa ukanunua used bongo , usijelogwa .. nunua used bongo ikiwa tayari ww Ni expert
Najazia hapo, kamwe usithubutu kununua gari USED ya mizigo au ya biashara ikiwa wewe ndio unaanza.

Ila hii kitu hapa home tokea nazaliwa hadi kufikia umri 20's sijawahi kuona dingi au ndugu wa karibu akinunua gari showroom labda zaidi ya hizi gari ndogo za kutembelea.
 
Mimi hii kitu naijua nje ndani yani mkuu kuanzia kuendesha nilijipatia uzoefu najua mipigo ya madereva najua faida najua vimeo

Na ni kweli inawezekana kuanza na gari moja mie nilianza na Tani 2 ya Mazda Titan miaka Mingi nikaja Kenta 3.5 Fuso Tandam/Kipisi ambacho saiz ni Mende na nna Semi za Howo . Mungu akisaidia ntatafuta Pulling ila sio Scania
Hongera mkuu, ama kwa hakika umepambana.
 
Lakini alisema lile gari jipya ndo trip ya kwanza.
No Dear, alisema alilinua kwa 15m i think kisha akalifufua hadi kufikia 83m, kwahio siku ile ndio ilikua trip yake ya kwanza tangu kulifufua na kwamba dereva alishalalamika kuwa kulikua na hitilafu.....

Sasa kufufua gari kwa mazingira ya kibongo bongo na huna ujuzi wa spare parts, utapewa spare yoyote ile. Ilitakiwa asiende umbali mrefu na ile gari at least ingepiga masafa ya Dar hata Chalinze ili kukagua uwezo wa kuhimili kashkash. Karibu Lunch
 
Mimi nilianza biashara ya Usafirishaji miaka kama 10 iliyopita. Hata sasa hivi nafanya usafirishaji mizigo sana tu local ila kwakua imenibidi(Niko kwenye supply business) kwahiyo swala la kuwa na Gari linasaidia kupunguza gharama ya bidhaa nnazouza.

Ila kama ingekua ni uamuzi wangu nisingekuja kumiliki gari la mizigo tena KAMWE

Hio mil 100 tafuta biashara nyingine sio ya kuwa na gari moja.Ni Risk kubwa mno unajitafutia .Hakuna cha bima wala upuuzi wa bima .Utakufa siku sio zako

Ukiwa na magari mengi inasaidia kugawanyisha Risks. Madereva nao dahh kila siku ni kutishana na bastola mezani na kutiana lockup

Hakuna biashara pasua kichwa kama hii katika biashara zote nilizokwisha kufanya

Usione kina Usangu,Overland wanazungusha chuma tu kisauzi ila hii biashara sio mchezo.

Ungekua na mtaji wa Billion plus ningekushauri hata uanze kupambana na kina Sham Nunu na hao underdogs wengine na nisingekushauri huko kwenye Mascania. Howo anafanya vizuri sana saivi anaenda ligi za kina Daf/Volvo
Kwa kuwa wewe ni mmiliki naomba nisaidie kabla sijaenda field nikapigwa.
Kukodisha gari la mizigo kwa ajili ya mazao ndizi n. K. tufanye kutoa Moshi sokoni kuleta dar sokoni ni sh ngapi?
Kwa aina ya tandam na fuso.
Na makubaliano yanakuwaje?
Ahsante sana ukinijibu na kama kuna wengine wanajua wanisaidie.
Na gari kwa huku nazipata wapi bila kupitia kwa dalali.
 
Mkuu mie nakushauri anza na Fuso Tandam ndio utapiga pesa zaid. Ninakushauri hvo kwa kuwa hapa home tuna Scania tatu na Fuso mbili ila Fuso ndio zinapiga kazi kuliko Scania.

Na pia km ni Scania kwa wewe unaeanza sikushauri kwa kuwa ni sumbufu sana hasa ikishaanza kuchoka. Scania za kukutoa umaskini ni zile model za kizaman.

Na pia wanaokushauri kuhusu magari ya abiria naomba usiwasikilize kabisaa, maana yana changamoto nyingi sana. Mie binafsi nina Nissan Caravan mbili ila ni kichefu chefu kitupu.

NB: nimekushauri kutokana na uzoefu wangu wa kuishi na hayo magari kwa muda mrefu.
Hizo fuso tandam unakodisha? If yes Moshi Dar sh ngapi? Na makubaliano yakoje?
 
113 & 124 spare zapatikana kiurahisi na gharama nafuu. Kuliko hizi P.G.R. series gharama na ufundi ni pasua ukichwa usipo kuwa makini
Lakini kwa nini mnawakatisha watu tamaa kwamba R hazifai achani hizo wewe mwambie tu kama ana nunua mtumba achague mzuri tu sasa hizo 113 zenyewe zinapotea saa hizi kuzipata kwenyewe kwa shida
 
Back
Top Bottom