Ww ni HR by professional au imetokea tu kujikuta na icho cheo?
Kama ww ni professional HR washauri mabosi zako kisheria ilo suala limekaaje na possible outcome iwapo utafanya wanachotaka kukifanya.
Kama umejikuta kwenye icho cheo ni hivi kabla ya kufika hatua ya termination mfanyakazi yeyote alietenda kosa lolote ni lazima apate nafasi ya kusikilizwa, kujitetea, kuonywa na kupata uwakilishi kwenye vikao halali vya kinidhamu. Kinyume na hapo akienda CMA na kudai kafukuzwa kazi bila kufata utaratibu lazima ashinde. Ukiwa kama HR na ukaona uwezi kufata huo mlolongo wa vikao vya kinidhamu basi unampunguza kazi kwa kumpa notice au kumlipa mshahara in lieu of notice na kumlipa stahiki zake nyingine zote. Sababu ya kumpunguza kazi lazima iwe genuine. Pia kumbuka kisheria mwajiri akiwa na lengo la kupunguza wafanyakazi ni lazima awasiliane na chama cha wafanyakazi.