Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

Bi Tozo atakuja kutetea hizo nauli kama alivyoitetea Tanesco na ujambazi wao wa kuunganishiwa umeme... yaani nalipa kila kitu halafu bado sio mali yangu. Na bado nakuwa mteja nisiye na mamlaka na bidhaa zangu. Kaujinga amaizing
 
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.

--

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imepokea maombi kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuhusu nauli za abiria kwa treni ya njia ya Reli ya Kisasa – ‘Standard Gauge Railway’ (SGR) zitakavyotumika kwa huduma ya usafiri wa treni za abiria.

Kwa mujibu wa Kifungu Na. 21 cha Sheria Na. 3 ya LATRA, 2019 Mamlaka inapaswa kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi wa kuridhia viwango vya nauli kwa huduma zinazodhibitiwa na Mamlaka ikiwemo nauli za treni.

Katika kulitekeleza hilo, Mamlaka imeandaa mkutano wa kupokea maoni ya wadau wa usafirishaji, ikiwa ni pamoja na watoa huduma, watumiaji wa huduma na wananchi kwa ujumla. Mkutano utafanyika tarehe 19 Disemba 2022 jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Anatorglo.

Nauli zinazopendekezwa na TRC ni Kama ifatavyo:

View attachment 2440636

View attachment 2440637

Kutokana na umuhimu wa mkutano huo, LATRA inawaalika wadau wa sekta ya reli na wananchi kwa ujumla kushiriki katika mkutano huo wa kukusanya maoni ya wadau.

Vilevile, wadau wanaweza kuwasilisha maoni yao kwa Mkurugenzi Mkuu kwa maandishi kupitia LATRA Makao Makuu, Mtaa wa Tambuka Reli, Dodoma au ofisi za LATRA zilizopo Makao Makuu ya kila mkoa Tanzania Bara kabla ya tarehe 3 Januari 2023.

Aidha, maoni ya wadau yanaweza kutumwa kwa barua pepe kupitia anuani hizi: info@latra.go.tz na dg@latra.go.tz

Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano – LATRA
06 Disemba, 2022​
Wapanga bei wana mabasi yao. Je wakiweka bei ndogo ya treni nani atapanda basi?
 
Naisubiria na Bwawa la Nyerere likamilike niyakumbuke maneno ya wanasiasa yalivyo matamu kama asali ila matendo machungu kama shubiri. Wakati wanaanzisha hizo harakati ilisemekana SGR ikikamilika bei yake itakuwa nafuu sana hata kushinda nauli za mabasi, Hilo limetoka tusubirie umeme kwa sababu huo tuambiwa unit moja haitozidi 150tsh tofauti na Sasa inauzwa karibia 380tsh ili tuweze kuzalisha bidhaa viwandani kwa gharama nafuu. Tulitolewa mpk na mfano baadhi ya nchi km marekani wao unit moja mpk inamfikia mlaji hifiki hata 100 ya kitanzania ndio maana wanazalisha bidhaa kwa gharama nafuu
 
Hapa au hii ni kutaka kuwaonyesha wananchi kwamba kuendesha huu mradi ni garama kubwa au wananchi kutumia treni ni anasa.

Yaani kwenda Dodoma -60,000/-!.

Treni kwa waliostaarabika huko ni usafiri wa garama nafuu sana sisi unaenda kuonekana ni anasa.

Hadi mwenyewe wameni surprise.
 
Au wanafanya kama kampuni ya apple walivyo tufanyia??wanataja kua simu zetu tutaziuza millioni 3,mtapaniki mtasonya mtapaza sauti kua gharama kubwa,but siku ya uzinduzi wanatangaza wanawapenda na wamepokea maoni yenu,wanauza million 1...hapo mind games inachezwa MTU anaenda kupunguza nauli ili aombe Kura...na bado haitakua reasonable price..
 
sasa utashangaa yanavyojaza, rejea mwendokasi,
Tatizo la tanzania tunatukuza Umasikini mno.

Binafsi naona bei iko sawa, kuna watu wanakereka na muda mrefu kutumika barabarani yaani km 450 masaa 7-9
Wakati kwa treni unaweza kutumia masaa 4
Na pia ni adventure

Kikifanyika kitu utasikia sisi wanyonge itakuwaje
 
Kwa nauli ya elfu 29 kama ni muda wa saa moja tu iko vizuri kuliko.kutumia karibu masaa saba kwa basi ma spidi limit barabarani kibao

Mabasi ya kwenda nyanda za juu kusini wajiandae kuwa na route za kuanzia morogoro kwenda mikoa hiyo sababu mtu akiua masaa sita ya barabara akishuka morogoro anapanda basi la kutoka Moro kwenda Iringa ,mbeya na Ruvuma anafika mapema tu

Treni hiyo iondoke mapema mfano saa 12 na nusu ifike morogoro saa moja na nusu watu wa mikoa ya nyanda za juu kusini wapande.mabasi yao kuanzia morogoro saa mbili yaondoke kwenda mikoani

Vivyo hivyo liwahi Dodoma wa mikoa ya kanda ya Ziwa wapandie mabasi Dodoma kwenda Kagera nk yawezekana kabisa watu wa kagera kufika siku hiyo hiyo bila kulala kahama

TRC wajipange kuhakikidha watu wana move faster kwa kushirikiana na wadau wa mabasi ya abiria

Ratiba zao wa consider hilo na Latra wajipange kupanga ratiba zao vizuri za mabasi ya Moro kwenda nyanda za juu kusini nk na Ya Dodoma kwenda kanda ya ziwa na kigoma nk

Treni ikimwaga mabasi yanapokea mbio yanakimbiza abiria
Mkuu ili wazo ni nzuri, tatizo mfumo wa maisha yetu waafrika hasa viongozi siyo wa kutatua changamoto+ kama hiyo bali wao wataongeza matatizo.
 
Mbona ndogo sana hio nauli. Ishu sio nauli ishu na mda. Kukaa masaa manne kwenye basi na kukaa Saa moja kwenye treni kipi bora
 
Huwezi kapande bus, huwezi kanyaga Moro sio mbali siku nne tu umefika kwa mguu.
 
Iwapo CHADEMA tutapewa ridhaa ya kuongoza Nchi hii tutashusha nauli za Treni ya SGR.
 
Back
Top Bottom