Nauli mpya za Mabasi zimeanza kutumika, vipi Mdau ulishirikishwa kupanga nauli hizo?

Hii imekaa vizuri, NAULI ZA SAMIA.
 
Serikali ifike wakati iangalie hali ya kipato ya wananchi wanao sababisha mzunguko wa pesa maana nchi yetu inawadundulizaj wengi kuliko wenye biashara kubwa sasa wanapigana maeneo ya msingi kama haya tunajikuta watu tunafeli safirishi vibiashara vyetu kutafuta masoko mkoani huku ni kuuita umaskini kwa wananchi tatizo serikali yetu inamuangalia sana mwenye nacho ili wamuonhezee lakin maoni yangu sakata la nauli lijadiliwe upya litaludisha nyuma wadundulizaji.
 
 
Kama ilivyo ada kwa UVCCM kupongeza mazuri ya serikali, basi ni wakati muafaka UVCCM waandae maandamano ya kumpongeza Raisi kwa kupandisha bei ya nauli, ili wabunge wenye mabasi akina Abood, Msukuma na wengine akina Super Feo watajirike.

UVCCM itapendeza kama maandamano ya kupongeza nauli mpya yatafanyika jumatatu 11-12-2023.

USAFIRISHAJI: Leo Desemba 8, 2023 Watumiaji wa huduma za Usafiri za Mabasi ya Masafa Marefu (Mabasi ya Mikoni) na Mafupi (Daladala) wanakutana na gharama mpya za Nauli.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), nauli za Mabasi yote zimepanda baada ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya Watoa Huduma na Wadau wa Usafiri (Wananchi).

Mama toka aingie madarakani, si mafuta, si tozo, si nauli zinapanda tu na hata mafuta soko la dunia yapo chini sana sema hizi kodi ni zaidi ya nusu ya bei.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…