Nauza Bata Bukini wenye miezi 8 wakiwa wamepatiwa chanjo zote

Nauza Bata Bukini wenye miezi 8 wakiwa wamepatiwa chanjo zote

Status
Not open for further replies.
Natamani Sana kuwafuga Hawa viumbe ila nachemka kwenye Bei TU...
Tafuta vifaranga uwafuge. Ila ununue kwa mtu aliyewapa chanjo za mwanzo
Bata hawa ni wazuri sana hutojutia hata kidogo kuwafuga
 
Acha ujinga hao bata wanauzwa hadi 200,000 kwa mmoja na soko kubwa ni kwa wachina
Kwa mambo kama haya ndio maana tukiunganika East Africa wabongo hawatoboi. Wana roho za ajabu na kitu hakijui, nilityegemea angeuliza kwa nini wanauzwa ghali ivyo 🤣
 
Hawa bata wanauzwa bei kwasababu wanasize kubwa sana. Bata m'moja tena dume, ukichinja sikukuu nyama yake ni nyingi kama mbuzi tu.

Sasa faida ya bata ni mayai yake pia anataga mayai ambayo unaweza benefit nje ya nyama. So faida ni nyingi kwa huyu bata. Wana nyama nyingi sana hawa na bata mzinga.
Tokapa na wewe. Wewe huwajui bata bukini. Wewe na mtoa thread wte mnashida.
Mara oonh wanafugwa na matajiri. Huyu mtoa thread kashindwa kumaliza nyumba anauza vitu anajiita tajiri.
 
Hawa bata wanakula sana mbuzi haoni ndani
Mimi ni mchaga wa Rombo, plus mzee wangu anafuga mbuzi kibaha wa kutosha tu
Kilimo cha mbuzi naona hakina faida sana kwa sababu mbuzi tu wenyewe hana nyama alafu wanakula hatari

Hawa bata bukini ni wanatoka Japan na Canada, wanakuwa wakubwa tu
Kabla hawajaingia nchini sasa watu wanafuga kwa wingi mmoja alikuwa anauzwa laki 3, bata mmoja tu
Ni bata wazuri sana wanapendezesha majumba ya kitajiri

Bata hawa wengine wanakuwa wakali kama mbwa, hivyo kama mtu hapendi mbwa basi unakuta wanakuwa wakali kama unavyoona mbwa anavyokuwa mkali
Wafugaji wengi wanaamini pia wanafukuza wachawi
Wazuri sana, ni kivutio kikubwa ndani ya nyumba, na sio bata hawa wa kawaida tunaowaona huku mtaani. .
20220415_144712.jpg
 
Tokapa na wewe. Wewe huwajui bata bukini. Wewe na mtoa thread wte mnashida.
Mara oonh wanafugwa na matajiri. Huyu mtoa thread kashindwa kumaliza nyumba anauza vitu anajiita tajiri.
Shida yako nini ndugu?
Labda nimekukosea sehemu naona unanishambulia sana.
 
Ni wazuri ila wanaishi miaka mingapi isije nikatoa million halafu ndani ya mwaka wakazeeka wakafa huku hawajataga
Hata miaka 20 hawa wanatoboa. .
Watu wengi wanashindwa bei tu ila wanawapenda sana. .
 
Hauwezi kusema kirahisi kuwa wanauzwa mil 1 wengine ukitaja bata tunawajua ni kama hawa bata wetu wanaokula mimavi.
Tutajie sifa kuu za hao bata kupelekea kuuzwa bei kubwa hivyo ili tushawishike kununua.
 
Hauwezi kusema kirahisi kuwa wanauzwa mil 1 wengine ukitaja bata tunawajua ni kama hawa bata wetu wanaokula mimavi.
Tutajie sifa kuu za hao bata kupelekea kuuzwa bei kubwa hivyo ili tushawishike kununua.
Google sifa za bata bukini au soma huu uzi toka mwanzo. Kwa kizungu anaitwa Goose (au Geese kwa wingi). .
 
Wanaliwa hawa wadudu??
Natamani tu nijue why wanauzwa ghali sana??
Niliwaona kule kigoma siku moja, madume yao yana wivu balaa

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Wanaliwa sana na wahindi na wachina kwa huku bongo
Binafsi sijawahi kula bata bukini
Hawa bata wanapendelea sana kula mboga za majani mfano spinach, kabichi nk
Wanakula vyakula vya kuku vya kuchanganya ila wanapenda sana kula mboga za majani
Upatikanaji wao ni adimu na wana gharama sana kwenye chakula, piga hesabu kununua mboga za majani tu kwa miezi nane niliowafuga. Wanakunywa maji 20 liters everyday
Wazuri sana na walinzi kama mbwa. .
 
Kila pair 350000 maana yake dume na jike anauza 350000 wote jumla ni laki 7. .
Ina maana wa kwangu ningeuza kama anavyouza huyu ningetakiwa niuze 1,050,000/-
Tokapa. Hao wanauza pair 350,000.
Dume na jike.
Na saiv yupo jamaa anauza 150,000 kwa mmoja.
Mimi nimefuga sana mataka taka hayo kama urembo. Nilipohama nyumba sikuwawekea uzio wao. Wanachafua parving zote hao. Nawajua A-Z .
 
Tokapa. Hao wanauza pair 350,000.
Dume na jike.
Na saiv yupo jamaa anauza 150,000 kwa mmoja.
Mimi nimefuga sana mataka taka hayo kama urembo. Nilipohama nyumba sikuwawekea uzio wao. Wanachafua parving zote hao. Nawajua A-Z .
Nimeandika kuwa hao wanauzwa pair wawili 350000 au wewe unasomaje?
Ni mifugo yake ana uhuru wa kuwauza hata mia
Huna kazi za kufanya zaidi ya kukaa kwenye keyboard na kushindana na watu bila sababu ya msingi?
Kwani we jamaa tulishawahi kukutana kwenye nyuzi huku tukakwaruzana au? Naona kama unataka ugomvi usio kuwa na maana nakuomba ufatilie mambo yako ndugu binafsi sipendi kupoteza mda kukwaruzana na watu mitandaoni maisha ni mafupi sana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom