Nawachukia sana hawa matapeli wanaouza dawa mbele ya misikiti

Nawachukia sana hawa matapeli wanaouza dawa mbele ya misikiti

Hivi kuna dawa ya kienyeji iliyouzwa kama ile ya kuitwa ngetwa? Mwenyewe alipoona mzigo unakubalika sokoni akawa anatoa matoleo tu ngetwa 1,ngetwa 2 nk😅
Yule mhuni alipiga sana hela; babu wa Loliondo anasubiri.
 
Kila baada ya swala ya Ijumaa utawakuta watu mbele ya misikiti wametundika tunguli, vibuyu na dawa wanazozinadi kuwa zinatibu maradhi mbalimbali ya binadamu. Mara nyingi wanaenda kwenye misikiti ya BAKWATA; ni nadra kuwakuta kwenye misikiti ya Sunni.
View attachment 2935829
Nimebaini hawa watu si waganga wala waganguzi bali ni matapeli wa kutupwa. Baadhi ya magonjwa wanayojinadi kutibu ni nguvu za kiume, bawasili, ngiri, mshipa, kukojoa kitandani, figo, kumrudisha mpenzi aliye mbali, nk. Kabla sijaenda mbali, naomba kuweka wazi kuwa mimi ni mhanga mmojawapo niliyewahi kutapeliwa mchana kweupe.

Siku moja nilipita mbele ya msikiti nikakuta watu wamekusanyika huku katikati yao kukiwa na mwanaume wa makamo aliyekuwa anaongea kwa uhodari sana. Nikasogea karibu kuchungulia kulikoni. Nikamsikia yule mwanaume akijinadi kuuza dawa mbalimbali za asili. Baada ya ushawishi wa kutosha nikanunua dawa moja iliyokuwa katika umbo la unga nikaenda kuitumia kwa mujibu wa masharti ya mganga yule. Baada ya kuitumia ile dawa nakuona haileti matokeo chanya, nikaamua kuifanyia uchunguzi wa kina. Lahaula! Kumbe haikuwa dawa bali unga wa muhogo.

Kwa kweli kitendo kile kiliniuma sana. Fikiria nimelipa fedha nyingi kununua dawa initibu maradhi yangu na usiku ule tayari nilishajiandaa kutest mitambo halafu nakuja kudhalilika mbele ya mpenzi wangu. Tangu siku ile niliwachukia sana hawa matapeli wanaofanya utapeli wao mbele ya misikiti.

MAONI YANGU
Inasikitisha sana jinsi watu wanavyotumia udhaifu wa maradhi kuwatapeli raia kwa kuwauzia dawa bandia misikitini. Hapa asilauimiwe shehe, imamu wala mwadhini. Hawa watu wanauza dawa feki kwa tamaa zao wenyewe. Hawatumwi msikiti, shehe au mtu yeyote.

Aidha, wagonjwa wanaonunua dawa hizi wanasukumwa na maradhi yao na kiranga chao wenyewe. Bawasili ilishakomaa unadanganywa kwamba itapakwa dawa iishe? Umerogwa. Nenda hospitali ukfanyiwe upasuaji. Ni muhimu kabla ya kununua dawa ukajiridhishe kama inafanya kazi au la.

Nawasilisha.
Ulichukua hatua gani? Ulirudi pale na kumchana live kwamba dawa yake ni feki na ni unga wa muhogo?
 
Pole Sana.

Dawa za kienyeji hazina uwezo wa kutibu matatizo yako kwa 100% Ila zinaweza kulituliza tatizo tu.


nguvu za kiume ni mzunguko mzuri wa damu hivyo haikuhitaji kununua mitishamba bali kuhakikisha unazingatia mlo kamili, na Kuwait stress free.
Umewahi kukutana na dawa ya kienyeji inaitwa MKUYATI?? Acha kabisa... Dawa zipo, tatizo ni utapeli.
 
Kila baada ya swala ya Ijumaa utawakuta watu mbele ya misikiti wametundika tunguli, vibuyu na dawa wanazozinadi kuwa zinatibu maradhi mbalimbali ya binadamu. Mara nyingi wanaenda kwenye misikiti ya BAKWATA; ni nadra kuwakuta kwenye misikiti ya Sunni.
View attachment 2935829
Nimebaini hawa watu si waganga wala waganguzi bali ni matapeli wa kutupwa. Baadhi ya magonjwa wanayojinadi kutibu ni nguvu za kiume, bawasili, ngiri, mshipa, kukojoa kitandani, figo, kumrudisha mpenzi aliye mbali, nk. Kabla sijaenda mbali, naomba kuweka wazi kuwa mimi ni mhanga mmojawapo niliyewahi kutapeliwa mchana kweupe.

Siku moja nilipita mbele ya msikiti nikakuta watu wamekusanyika huku katikati yao kukiwa na mwanaume wa makamo aliyekuwa anaongea kwa uhodari sana. Nikasogea karibu kuchungulia kulikoni. Nikamsikia yule mwanaume akijinadi kuuza dawa mbalimbali za asili. Baada ya ushawishi wa kutosha nikanunua dawa moja iliyokuwa katika umbo la unga nikaenda kuitumia kwa mujibu wa masharti ya mganga yule. Baada ya kuitumia ile dawa nakuona haileti matokeo chanya, nikaamua kuifanyia uchunguzi wa kina. Lahaula! Kumbe haikuwa dawa bali unga wa muhogo.

Kwa kweli kitendo kile kiliniuma sana. Fikiria nimelipa fedha nyingi kununua dawa initibu maradhi yangu na usiku ule tayari nilishajiandaa kutest mitambo halafu nakuja kudhalilika mbele ya mpenzi wangu. Tangu siku ile niliwachukia sana hawa matapeli wanaofanya utapeli wao mbele ya misikiti.

MAONI YANGU
Inasikitisha sana jinsi watu wanavyotumia udhaifu wa maradhi kuwatapeli raia kwa kuwauzia dawa bandia misikitini. Hapa asilauimiwe shehe, imamu wala mwadhini. Hawa watu wanauza dawa feki kwa tamaa zao wenyewe. Hawatumwi msikiti, shehe au mtu yeyote.

Aidha, wagonjwa wanaonunua dawa hizi wanasukumwa na maradhi yao na kiranga chao wenyewe. Bawasili ilishakomaa unadanganywa kwamba itapakwa dawa iishe? Umerogwa. Nenda hospitali ukfanyiwe upasuaji. Ni muhimu kabla ya kununua dawa ukajiridhishe kama inafanya kazi au la.

Nawasilisha.
Uzi wako umeusuka kitaalam Sana, lengo sio ku adress kutapeliwa. Lengo lilikuwa kutaka kuonyesh connection yao , ushirikina na huko wanako swali watu.

But umeuwek fresh ili upate hata mchango wao. Ngoja tuone
 
Ulichukua hatua gani? Ulirudi pale na kumchana live kwamba dawa yake ni feki na ni unga wa muhogo?
Hawa jamaa wanaishi kama digidigi mkuu. Wanahama mkoa hadi mkoa na msikiti hadi msikiti. Kwa utapeli wao, kama wangekaa mahali pamoja kwa muda mrefu, wateja wangewashusha mshipa.
 
Asante mkuu. Kivumbasi ni nn na nachanganya kwa ratio gani mkuu?
Matapeli wa dawa hawako mbele ya misikiti tu. Wamejaa kila mahali na pengine wale wa sehemu nyingine ndiyo hatari zaidi. Ogopa wale wanaotangaza au kuwa na vipindi kwenye TV... sijui mnawaita kina dr Mwaka....
 
Uzi wako umeusuka kitaalam Sana, lengo sio ku adress kutapeliwa. Lengo lilikuwa kutaka kuonyesh connection yao , ushirikina na huko wanako swali watu.

But umeuwek fresh ili upate hata mchango wao. Ngoja tuone
Hiyo ni tafsiri yako mkuu. Mimi nimeshusha uzi kama ulivyo na watu wote wanaruhusiwa kureply bila kuzingatia itikadi zao including FaizaFoxy
 
Matapeli wa dawa hawako mbele ya misikiti tu. Wamejaa kila mahali na pengine wale wa sehemu nyingine ndiyo hatari zaidi. Ogopa wale wanaotangaza au kuwa na vipindi kwenye TV... sijui mnawaita kina dr Mwaka....
Wale wa kwenye TV na redio ndio wezi na matapeli kuliko maelezo. Jana nilisikia mmoja akiongea redioni kuwa UTI inasababisha upungufu wa nguvu za kiume. Na alisisitiza kuwa bakteria wanaosababisha UTI hushambulia red blood cells na kupelekea upungufu wa nguvu za kume. Hili ni janga la kitaifa.
 
Sijawahi kuona tunguli mbele ya msikiti zaidi ya kuwepo dawa za asili. Acha kuongeza chumvi mkuu. Umeweka na picha kabisa Ili kuthibitisha uongo wako.
 
Wale wa kwenye TV na redio ndio wezi na matapeli kuliko maelezo. Jana nilisikia mmoja akiongea redioni kuwa UTI inasababisha upungufu wa nguvu za kiume. Na alisisitiza kuwa bakteria wanaosababisha UTI hushambulia red blood cells na kupelekea upungufu wa nguvu za kume. Hili ni janga la kitaifa.
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
 
Sijawahi kuona tunguli mbele ya msikiti zaidi ya kuwepo dawa za asili. Acha kuongeza chumvi mkuu. Umeweka na picha kabisa Ili kuthibitisha uongo wako.
Mkuu hebu fanya uchunguzi. Hawa watu wanakuwa na tunguli, vibuyu na vifaa vingine vya ajabu ajabu.

Siku niliyotapelewa, yule tapeli alikuwa na vifaa hivyo vyote pamoja na miti na matunda yenye shape za ajabu ajabu ambayo ameyaokota huko mwituni na kuyatumia kama.vifaa vya utapeli.
 
Waislamu wanauziana mambo ya kichawi wenyewe kwa wenyewe
 
Back
Top Bottom