Nawaheshimu sana walimu, lakini mwalimu yeyote akimfanyia mtoto wangu kama inavyoonyesha picha hii nitamtafuta kokote alipo tumalizane

Ukatili kwa watoto! Jiulize,hapo anamchapamtoto sehemu gani ya mwili? Anaweza kumpasua ini au figo. Utakuta kosa lake kakosea hesabu mbili, mwalimu anamwadhibu utafikiri yeye kwenye darasa lake akiwa mwanafunzi alikuwa ndio kipanga wa darasa!
Ingekuwa ni video tungeweza kujudge vzr. Mtoto lazima achapwe kwa kiasi
 
Kumbe una makasiriko, una hasira na walimu. Umejificha kwenye kivuli cha utetezi wa haki za watoto.

Kama ulichapiwa na mwalimu, kubali ni maisha. Pole kwa kuchapiwa.
 
Unataka kusema nini yaani? Kwa kipindi chake ulitarajia asome kozi gani nyepesi zaidi ya ualimu?

Hiyo ndiyo kozi pekee ambayo binadamu yeyote anaweza kusoma na usipate Supplementary wala discontinuation hadi unahitimu.
Kwa hiyo kwamba alikuwa hana akili
Unajua Magufuli nae alikuwa mwalimu ?
 
Mimi kama mwalimu ukiniletea ushenzi wako tunamalizana kama unavyotaka. Huwa nawataka sana wazazi wapuuzi kama wewe waje shuleni tumalizane. Kama vipi chukua toto lako kalifundishe mwenye nyumbani kwako, sipendagi ujinga
Una tatizo la afya ya akili sababu unamshindilia ugali Kila siku
 
Sio kweli mkuu Kuna watu walisomea ualimu kwasababu ya priority ya kubwa ya kupata mkopo na unafuu wa Ada hata hivyo fuatilia asilimia kubwa za maTO wapo wapi
 
Hehehe...Mimi ni miongoni mwa watu wachache waliobahatika kusoma noble course ambayo kwa mtu kama wewe mwalimu mwaka wa kwanza tu una disco.
hakuna ku disco eti nina misimamo mikali juu ya watoto watukutu, watanyukwa tu, elewa class control action, hiyo ni kanununi yangu kudhibiti vurugu darasani, The Loth Doctrine
 
Ingekuwa ni video tungeweza kujudge vzr. Mtoto lazima achapwe kwa kiasi
Kuchapwa ndiyo njia pekee ya mtoto kuelewa?

Hakika watumwa ni wengi barani Afrika.

Mimi sijawahi kumchapa mtoto wangu lakini nikimuelekeza jambo analifanya kwa haraka kwasababu nimemlea kama rafiki nazungumza naye namna nzuri ya kuishi na wazazi pamoja na jamii kwa ujumla.

Lakini hali ni tofauti kwa watoto wa majirani maana wazazi wao ni aina yako wanaoamini kwenye kuchapa. Wamekuwa wakiwachapa lakini ndiyo kwanza watoto wamekuwa sugu.

Kilichomsababisha achapwe jana anakirudia leo kitu kile kile.

Kama wewe ni mwalimu mfanye mwanafunzi awe rafiki atakusikiliza kwa umakini na kwa upendo mkubwa na hata kuelewa darasani anakuelewa vizuri zaidi kuliko mwalimu chapa chapa ambaye anachukiwa na watoto.

Halikadhalika ukiwa mzazi mfanye mtoto awe rafiki uta enjoy maisha maana hatokuficha kitu chochote kiwe kibaya ama kizuri.
 
hakuna ku disco eti nina misimamo mikali juu ya watoto watukutu, watanyukwa tu, elewa class control action, hiyo ni kanununi yangu kudhibiti vurugu darasani, The Loth Doctrine
Kanuni zako haziwezi kwenda kinyume na sheria/kanuni kuu ambazo zinatambuliwa na mamlaka.

Ukiwa na kanuni zako zinazokiuka kanuni mama basi hizo kanuni zako ni null and void ab initio.
 
Maticha wanastress sana😀, kama anaua nyoka!
 
Nimecheka sana, dogo sijui alikosea nini?!
 
Hayo yote unayo yaona ni matokeo ya Sera Mbovu ya Elimu.

Mtakomaa na waalimu mpaka muwauwe, Lkn shida ni sera mbovu ya Elimu.

Imagine Unafundisha biology & Chemistry. Form 2 wako 200, Form four wako 200, Jumla una wanafunzi 400 wa kuwaagalia kila siku.

bado Pia, Mishahara duni, Nyumba za walimu hakuna, Office nzuri hakuna, Vitabu hakuna, Internent hakuna, Umeme sua sua vijijini, Posho hakuna

Hayo yote ya nazaa frustration kwa mwalimu, Kupelekea kua na Service mbovu kwa wateja wake ambao ni wanafunzi
 
Una tatizo la afya ya akili sababu unamshindilia ugali Kila siku
kama we unashindia chipsi mayai ziko wapi akili zako murua? Ugali nakula sana tu tena ugali wa uwele, huo hapo kwenye avator na afya ya akili ipo imara unajibiwa vema upuuzi wako. Una hoja nyingine kuhusu kuchapawa watoto nikujibu? Wazazi wakorofi huwa nawapenda sana wakiingia kwenye anga zangu shuleni nakabiliana nao mpaka wanashika adabu na kuwa na heshima kwa walimu wanaowalelea watoto wao wakati wakiwa vibaruani mwao. Heshimu walimu
 
Shukuru tu kwamba umepata mtoto muelewa, anae kuelewa kirahisi. Mimi pia mtoto wangu nilimchapa mara moja tu akiwa na miaka 5 na sikuwahi kurudia tena.
Ila kuna aina ya watoto viboko ni muhimu, bila fimbo hawaelewi chochote
 
hakuna ku disco eti nina misimamo mikali juu ya watoto watukutu, watanyukwa tu, elewa class control action, hiyo ni kanununi yangu kudhibiti vurugu darasani, The Loth Doctrine
Na juzi serikali imewakumbusha na kuwasisitiza walimu juu ya kufuata miongozo mbalimbali ya elimu ikiwemo muongozo wa utoaji adhabu mashuleni.

Serikali imesisitiza kwamba mwalimu yeyote atakayeenda kinyume na utaratibu wa utoaji adhabu basi serikali haitasita kumchukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kumfuta kazi.

Fuatilia maagizo ya serikali uwe safe zone usije kuwa mbuzi wa kafara ukakosa stahiki zako ulizohangaikia kwa miaka kadhaa.

Kumbuka mwalimu unaposababisha majeraha ama kifo kwa mtoto kuanzia serikali hadi jamii kwa ujumla wanakushughulikia hakuna hata mmoja atakayekuwa upande wako.

Class management shouldn't be contrary to the given laws, regulations and guidances.

Hasira hasara ndugu mwalimu. Omba yasikukute maana wapo walimu wanajutia vitendo vyao vya ukatili dhidi ya mtoto wanatamani wapewe japo dakika ya kujirekebisha lakini ndiyo haiwezekani tena.
 
hakuna ku disco eti nina misimamo mikali juu ya watoto watukutu, watanyukwa tu, elewa class control action, hiyo ni kanununi yangu kudhibiti vurugu darasani, The Loth Doctrine
Mtu unastress zako halafu mtoto wa mtu anakuletea mambo ya kishwain, lazima lazima utembeze mkono.
 
Unataka kusema nini yaani? Kwa kipindi chake ulitarajia asome kozi gani nyepesi zaidi ya ualimu?

Hiyo ndiyo kozi pekee ambayo binadamu yeyote anaweza kusoma na usipate Supplementary wala discontinuation hadi unahitimu.
achaga uongo, walimu wanafeli sana tu, nani kakuambia kozi ya ualimu ni rahisi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…