Nawaheshimu sana walimu, lakini mwalimu yeyote akimfanyia mtoto wangu kama inavyoonyesha picha hii nitamtafuta kokote alipo tumalizane

Miaka ya nyuma tumekula sana hizo stiki tena walimu walikua na misuli kweli kweli πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€, kwa vitoto vya miaka ya karibuni sishauri sana vichapwe fimbo nyingi afya zao ni mgogoro
Unaona sasa licha ya wewe kukutana na adhabu za kikatili lakini haikukusaidia chochote badala yake ukaishia tena kuwa mwalimu.πŸ˜’

Kama adhabu za viboko zingekusaidia maana yake leo ungekuwa hata daktari mwanasheria ama injinia.

Kwahiyo tunarudi kwenye makubaliano kwamba viboko haviwezi kumsaidia mtoto kufikia ndoto zake badala yake kuzungumza kwa smooth language pengine ingemsaidia zaidi mtoto.
 
Ebu nikupe kisa wakati tupo advance kuna bwana alikua na miaka 22 yule jamaa bwana akawa na analala nyumbani kwa mke wa mtu, siku hiyo wapangaji wakamsanua jamaa aje afumanie, oya jamaa alikua na panga, huyo dogo ashukuru ngumu aliyompiga yule mume wa yule mwanamke ilmkalisha jamaa sekunde kadhaa dogo akakimbia, mbio

Basi jamaa aliporudi skuli ikapigwa tafutwa skul nzima na mgoni wake hadi akapatikana Huyu, watu kama lazima kidogo utumie brutal way mkuu
 
Kwasasa katika jamii kuna kiwango kikubwa cha mmomonyoko wa maadili, kuna watoto shuleni ni wakorofi sana. Wengine wanafikia hatua hata ya kuwatukana walimu wao pamoja na watu waliowazidi umri, heshima hakuna kabisa. Mtoa mada kwa taarifa yako adhabu nyingi zinazotolewa shuleni hazihusiani na mtoto kutokuwa na akili darasani bali ni ukorofi wa watoto kama vile upigaji kelele, uchelewaji, kiburi, kutotii maagizo/maelekezo wanayopewa na walimu, wizi, kutofanya usafi, kutofanya home work, kutoandika notes, kuja na redio na simu shuleni na kusikiliza muziki kwa kupitia earphone wakati wa vipindi. Mwalimu anapoona mwanafunzi anarudia rudia makosa haya anahisi kudharauliwa, hii inapelekea hasira inayosababisha adhabu ya viboko.
Watoto wengi japo sio wote ambao huwa wanachapwa mara kwa mara shuleni ukifatilia mienendo yao hata nyumbani kimaadili hawako vizuri.
Hivyo wazazi tujitajidi kuwalea watoto wetu katika maadili mema, ukiwalea vema hiyo tabia itakuwa reflected hata huko nje.
Tupunguze mihemko, lea watoto wako katika maadili mema ili wawe na nidhamu, fuatilia mienendo ya mwanao, pia fuatilia maendeleo yake kitaaluma. Hutasikia wamechapwa huko shuleni.
 
Umefanya nicheke tu mkuu.
 
Siku hizi hatuwachapii kivilee wengi broiler, mtawachapa nyinyi wenyewe ,unatoka jasho alfu unaua unafungwa kisa toto tundu wa mtu aaghr
Afadhali wewe umeshtukia mchezo mapema.

Ukijeruhi ama kuuwa hilo ni lako peke yako kila mtu atakushambulia ikiwemo serikali.

Jela utaenda peke yako hakuna mwalimu atakayekuja kukusaidia kifungo hata kama alikuwa anakushangilia unavyochapa watoto hovyo.

Ni vema kujiepusha na kutoa adhabu kiholela maana watoto wengi siku hizi afya sio imara anaweza kuwa na magonjwa yake ya muda mrefu lakini siku unamchapa tu ndiyo unammalizia hatimaye msala unakuandama wewe.
 
Yote hayo makosa si yameorodheshwa kwenye sheria za shule na hukumu anayostahili kupewa anayezivunja? Ina maana walimu uwa mnatupa form ambazo hata nyie hamzisomi?
 
Inabidi na wao waanze kupewa adhabu wakikosea kama kuita mvua kuchimba visiki, kushika masikio ikibidi na mboko wacharazwe
 
Unaona sasa licha ya wewe kukutana na adhabu za kikatili lakini haikukusaidia chochote badala yake ukaishia tena kuwa mwalimu.πŸ˜’
Id za jf zisikichanganye bwashee nina kazi nyingine tofauti na ualimu πŸ˜€πŸ˜€, nawafundisha wakubwa na fimbo wanakula kisawasawa
 
Oya Watoto watachapwa na hufanyi kitu.

Hata miaka yetu Wanafunzi walichapwa.
 
Yote hayo makosa si yameorodheshwa kwenye sheria za shule na hukumu anayostahili kupewa anayezivunja? Ina maana walimu uwa mnatupa form ambazo hata nyie hamzisomi?
mimi ni mzazi sio mwalimu.

Tuwalee watoto wetu kwa kuzingatia maadili, wanapostahili kuchapwa viboko wachapwe si shuleni tu hata nyumbani.

Shida inakuja pale mtoto anapochapwa kwenye matako yeye akajihami kwa kuweka mikono, fimbo inapopiga kwenye mkono/vidole vikivimba halafu akatokea mtu akachukua picha au video kwa kutumia simu then akaisambaza kwenye mitandao yani inakuwa gumzo nchi nzima.
Yani siku hizi tunaleo watoto kimayai mayai tu, hatutaki waguswe. Hi ni shida kubwa mno. Kwa mwendo huu baada ya hiki kizazi chetu kupita kikija kile cha pili (yani cha wajukuu wetu) kitakuwa kizazi cha ajabu sana.
 
Wanadhani kuwalea kimayai ndo kuwasaidia kumbe wanawaharibu
 
Hakuna mwalimu mtabe sababu ya uduni wa mishahara, no disrespect nawaheshimu walimu wote tz.
inabidi tujitokeze kuwatetea walimu kama wao hawawezi kujitetea huku wakijia misingi ya elimu na kanuni za ufundishaji pamoja na haki za watoto
 
Shule za Serikali hizo.
Ofisi imejaa mianzi vitabu Hakuna.
Yani unapiga Mtoto kwa Miguvu ambayo yaweza kutoa nishati ya Umeme vijiji vinne.

Kuna mda nawazaga kazi ya kufunza Mtoto imekaa Sawa kwa KE ...Njemba mje Huku tupike zege Mana kila mauaji ya wanafunzi ME ndio masteringi.
 
Mmh!
 
You are Stupid...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…