Uchaguzi 2020 Nawashauri CHADEMA wamtulize kwa sasa Tundu Lissu aache kufanya mashambulizi makali kwa Rais Magufuli

Uchaguzi 2020 Nawashauri CHADEMA wamtulize kwa sasa Tundu Lissu aache kufanya mashambulizi makali kwa Rais Magufuli

Tusiendekeze matapeli wa kisiasa, huyu Lissa haaminiki toka kipindi
- Amkashifu vibaya Lowassa na baadae kumkumbatia na kumnadi.
- Kupambana name Zitto kisa anataka kugombea uenyekiti cdm.
- Alipinga madini kuibwa nabaadae kupinga jitihada za kuzuia wizi hip.
- Aliponda marais wastaafu ikiwamo Nyerere nasasa anawasifu.
- Anatokea chama kisicho namfano mzuri wa matumizi yafedha, demokrasia na haki katika kuchaguliwa/kupewa nafasi.
- Anamaneno ya kashfa, kejeli,dharau name yaliyokosa utu, uungwana na shukurani!!
pamoja na mengi mengine Lissu sio candidate bora bali mbele nyuma yaani bora candidate
 
Tundu Lisu amefanya mashambulizi makali kwa Magufuli leo mara baada ya kuchukua fomu, amemsema Magufuli kwa namna amabavyo hajawahi kusemwa kwa miaka mingi huku wananchi wakishangilia
kwa mwendo huu Tume ya Uchaguzi na System nzima Tanzania huenda wakamuengua asigombee maana itakuwa hatari kwa mashambulizi anayoyafanya, Chadema na yeye mwenyewe wangejizuia kwanza wafanye kila kitu kwa upole kisha kampeni zikikolea mashambulizi ndio yakolee kiasi




Watu mmeishi chini ya udikteta uchwara miaka 5 mmegeuka waoga wakubwa! Kwani TL kasema nini cha ajabu ambacho wapinzani walikuwa hawasemi wakati wa kampeni za Urais kama hizi tangu 2010 had 2015?

Tofauti ni kwamba Watanzania wamekaa chini ya hofu ya kuongea hasa dhidi ya serikali kiasi cha kudhani kumsema Rais na serikali yake ni kosa la jinai.

MSIOGOPE! TL amelipia demokrasia ya nchi hii kwa damu yake mwenyewe. Hata Nyerere hakutoa damu yake kuununua uhuru wa nchi hii. Hiyo hofu yenu ya kuikosoa serikali na kutamani wapinzani wapotezwe imelipiwa kwa damu iliyotaka kugharimu uhai wa TL alipopigwa risasi 16 mwilini na bado kapona.

Relax. The best is yet to come.
 
Tundu Lisu amefanya mashambulizi makali kwa Magufuli leo mara baada ya kuchukua fomu, amemsema Magufuli kwa namna amabavyo hajawahi kusemwa kwa miaka mingi huku wananchi wakishangilia
kwa mwendo huu Tume ya Uchaguzi na System nzima Tanzania huenda wakamuengua asigombee maana itakuwa hatari kwa mashambulizi anayoyafanya, Chadema na yeye mwenyewe wangejizuia kwanza wafanye kila kitu kwa upole kisha kampeni zikikolea mashambulizi ndio yakolee kiasi


mkuu ndo siasa hapa nami nishauri ccm sasa hakuna namna ni lazima wasijili viungo vipya au viungo vilivyokuepo virudishwe mfano mzee makamba anaitajika , nape anaitajika sijajua wengine ndani ya ccm maana sikijui chama vizuri ila kwa spana hizi nafikili ni rasharasha bado mvua maana chadema mnyika ,matiko, bulaya, heche ,msigwa ,lema , mdee, sugu, mwalim , achana na mbowe, bado wana pasha sasa achana na wengine wakiliamsha dude inakuaje ,maana nimewai shudia uchaguzi wa marudio wa udiwani peramiho kwa mwagama kule dada mmoja na inasemekana alikua anafanya biashara ya baa but aliwsha moto na kirikuu na spika za kawaida tu ila uchaguzi ulikua zaidi wa jimbo , ccm ililazimika piga kampen za kitongoji kwa kitongoji sitokuja sahau uchaguzi huo ,ilikua mwaka juzi kama sikosei sijui vyama pinzani hupataje watu kama hawa , hatari sana
 
Kwa Mara ya kwanza kuona wapinzani wakipinga maendeleo hadharani yani mtu anaeitwa wakili msomi anasema eti ukisema umejenga bwawa na kidatu je mh yani hizi ndo sera za wapinzani ni mpuuzi pekee atakaewapigia kura kwa sera za namna hii

Nikimuangalia Lissu sasa hv si Lissu yule mwenye kujenga hoja si lissu yule wa Richmond si Lissu yule aliekuwa tunamfahamu
Wewe ndiyo mpuuzi kabsa? Maendeleo yapi? Maendeleo siyo Hisani za CCM maendeleo hayaletwi na pesa binafsi toka mfukoni mwa mtukufu , wewe mwenyewe hujielewi unawaje kumwelewa Tundu lisu? Kule Africa kusini kuna maendeleo makubwa zaidi ya Tanzania ambayo yaliletwa na makaburu lakini wapigania uhuru walikataa kuishi kama mashetani wakadai uhuru wao na maisha yanaendelea vizuri
 
Lisu ni sawa na mwanamke anayetoa nje siri ya ndani ya nyumba.. Ameichafua sana nchi huko Ulaya na Marekani, hovyo kabisa, haifai hata kuwa balozi wa nyumba 10!!
Lisu hajachafua nchi.
Haja ficha takwimu za corina.
Hajaminya demokrasia
Haja bana vyombo vya habari.
Hajapoteza raia.
Hajapiga mtu risasi.
Hajazuia CAG kufanya kazi yake
Wanaofanya hayo ndio wanachafua nchi. Wewe mwenyewe unjua ukweli ila umeamua kujitoa ufahamu.
 
Lisu ajikite kutuambia atakayoyafanya, kila mtu anajua strength na weakness za Magufuli hivyo tumechoka kuzisikia.

Ni wakati muafaka sasa upinzani hasa Lisu kuanza kutumegea mikakati waliyo nayo katika kutuvusha kutoka hapa tulipo kwenda pazuri zaidi.

Tumechoka kila siku kusimuliwa blunder za Magufuli
Sio muda wa kutangaza ilani hadharani huh. Huo ni mtego.
 
AHSANTE MUNGU KWA KUMUWEKA LISSU HAI.
 
Kwa mtazamo naona inamfanya Lisu aonekane ana personal hatred na Magufuli

Ni kweli kabisa usemayo, ila Lisu alipigwa kabisa risasi, na anamnyooshea kidole huyo huyo, na mpaka sasa hakuna uchunguzi wowote.
 
Magufuli lazima ashinde, je upinzani tumejiandaaje kumlinda Tundu lisu kwa miaka mitano ijayo, akiwa hana nafasi yoyote serikalini ?
Suala la ulinzi wa raia ni jukumu la serikali kwa kutumia vyombo vyake vya ulinzi!
 
Tundu Lisu amefanya mashambulizi makali kwa Magufuli leo mara baada ya kuchukua fomu, amemsema Magufuli kwa namna amabavyo hajawahi kusemwa kwa miaka mingi huku wananchi wakishangilia
kwa mwendo huu Tume ya Uchaguzi na System nzima Tanzania huenda wakamuengua asigombee maana itakuwa hatari kwa mashambulizi anayoyafanya, Chadema na yeye mwenyewe wangejizuia kwanza wafanye kila kitu kwa upole kisha kampeni zikikolea mashambulizi ndio yakolee kiasi


Mbona yeye alipewa mashambulizi makali Sana ya risasi akavumilia awe mpole Hakuna aliye juu ya dunia, ukimjeruhi mbogo uwe mpole
 
Mashambulizi ndio sera za cdm. Nyie jamaa mkisalitiwa na sanduku la kura msije kulia kua mumeibiwa.
 
Haenguliwi mtu hapa
Mwacheni lissu ajimalize mwenyewe,hatutaki kuwapa watu sababu ya kushindwa.
Sisi ccm tutaongelea issues,lissu muacheni aongelee watu,kura zitaamua
 
Tuweeekeni alichosema wengine simu hizi azifungui clip
 
Tundu Lisu amefanya mashambulizi makali kwa Magufuli leo mara baada ya kuchukua fomu, amemsema Magufuli kwa namna amabavyo hajawahi kusemwa kwa miaka mingi huku wananchi wakishangilia
kwa mwendo huu Tume ya Uchaguzi na System nzima Tanzania huenda wakamuengua asigombee maana itakuwa hatari kwa mashambulizi anayoyafanya, Chadema na yeye mwenyewe wangejizuia kwanza wafanye kila kitu kwa upole kisha kampeni zikikolea mashambulizi ndio yakolee kiasi


Dr. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Aliesababisha yy kwenda ku
Lisu ni sawa na mwanamke anayetoa nje siri ya ndani ya nyumba.. Ameichafua sana nchi huko Ulaya na Marekani, hovyo kabisa, haifai hata kuwa balozi wa nyumba 10!!
Aliesababisha lisu aende kuichafua nchi ni nani? Tuanzie hapo kwanza!
 
Back
Top Bottom