Erickford4
JF-Expert Member
- May 22, 2017
- 1,133
- 1,098
Habari zenu wakuu,
Mimi ni mwalimu idara ya sekondari katika mkoa wa Mara. Niliwahi kuugua ugonjwa wa tumbo kujaa na kuvimba ambao kule Mara ni maarufu kwa jina la passport size huwa inatokana na kulogwa.
Nilihangaika kutafuta uponyaji wake kwa njia ya hospitali hali ikawa sivyo hadi niliporudi kwa wenyeji wakanipeleka kwa mtaalam mmoja (kalumanzila) aliyekuwa anaishi nchi ya Kenya akanipa dawa kwenye kikombe, yeye kutibu kwake anatumia hiyo dawa yake tu kama alivyo yule babu wa Loliondo.
Nilipona lakini nilipewa masharti ya kutokula chapati kwani ilidaiwa kuwa nililogewa kupitia chapati.
Maisha yalisonga lakini nikajikuta nimekula chapati tena na kuja kuugua tena ule ugonjwa, nikapelekwa tena na tena kwa ajili ya dawa kwa kweli maisha yangu yalikuwa na mitihani kwa staili hiyo.
Nilitamani kuhama lakini nilipofika halmashauri kulikuwa na tangazo kuuubwa lililosema UHAMISHO UMESITISHWA. Baada ya muda tena niliugua safari hii nilichukia na morali ya kazi ilikatika nikaamua kwenda kwetu Tanga nikahangaika huko mpaka nikaweza kupona kabisa.
Tatizo likaja namna nilivyoondoka kwani mkuu wangu alikataa kunipa ruhusa nikaondoka kwa kulazimisha maana niliona kama wanafurahia kuugua kwangu.
Niliporudi nikakutana na barua ya kufukuzwa kazi na nilipofuatilia wakawa wakali kama mbogo sikukata tamaa nikaenda tena na tena hadi kufika mwaka huu wakaniambia ili niweze kurudi kazini natakiwa niandike barua ya kuomba kuajiriwa upya katika halmashauri nyingine tofauti na ile niliyokuwa nimeajiriwa mwanzo nikiambatanisha vitu vifuatavyo
Nimefuatilia huu mlolongo nikaona kama vile ni mgumu mno kufanikisha naomba kwenu wanabaraza kujuzwa kama ndio utaratibu au wameamua tu kuniwekea vikwazo ili nisifurahie mkate pamoja na familia yangu pia nilitaka usaidizi kwa aliye mjuzi namna rahisi ya kuweza kurudishwa kazini.
Natanguliza shukrani.
Mimi ni mwalimu idara ya sekondari katika mkoa wa Mara. Niliwahi kuugua ugonjwa wa tumbo kujaa na kuvimba ambao kule Mara ni maarufu kwa jina la passport size huwa inatokana na kulogwa.
Nilihangaika kutafuta uponyaji wake kwa njia ya hospitali hali ikawa sivyo hadi niliporudi kwa wenyeji wakanipeleka kwa mtaalam mmoja (kalumanzila) aliyekuwa anaishi nchi ya Kenya akanipa dawa kwenye kikombe, yeye kutibu kwake anatumia hiyo dawa yake tu kama alivyo yule babu wa Loliondo.
Nilipona lakini nilipewa masharti ya kutokula chapati kwani ilidaiwa kuwa nililogewa kupitia chapati.
Maisha yalisonga lakini nikajikuta nimekula chapati tena na kuja kuugua tena ule ugonjwa, nikapelekwa tena na tena kwa ajili ya dawa kwa kweli maisha yangu yalikuwa na mitihani kwa staili hiyo.
Nilitamani kuhama lakini nilipofika halmashauri kulikuwa na tangazo kuuubwa lililosema UHAMISHO UMESITISHWA. Baada ya muda tena niliugua safari hii nilichukia na morali ya kazi ilikatika nikaamua kwenda kwetu Tanga nikahangaika huko mpaka nikaweza kupona kabisa.
Tatizo likaja namna nilivyoondoka kwani mkuu wangu alikataa kunipa ruhusa nikaondoka kwa kulazimisha maana niliona kama wanafurahia kuugua kwangu.
Niliporudi nikakutana na barua ya kufukuzwa kazi na nilipofuatilia wakawa wakali kama mbogo sikukata tamaa nikaenda tena na tena hadi kufika mwaka huu wakaniambia ili niweze kurudi kazini natakiwa niandike barua ya kuomba kuajiriwa upya katika halmashauri nyingine tofauti na ile niliyokuwa nimeajiriwa mwanzo nikiambatanisha vitu vifuatavyo
- Nakala ya barua ya kufukuzwa kazini
- Nakala ya barua ya kuomba kuajiriwa upya iliyoandikwa kwenda katika halmashauri niliyokubaliwa kuwa nitapata nafasi (yaani hapa inatikiwa niombe kwanza nafasi nikubaliwe kwa maandishi ndio niandike tena barua hiyo nikiambatanisha hiyo nakala)
- barua za wadhamini watatu wanaonishuhudia kuwa mwenendo wangu ni wa kukubalika katika jamii, wadhamini hao watatu kila mmoja atoke katika mojawapo ya makundi yafuatayo:
- Kiongozi wa kisiasa - Mbunge/Diwani
- Kiongozi wa kiroho - Mchungaji, shehe, padri, askofu
- kiongozi wa kiutawala - DAS, Afisa tarafa, DC
Nimefuatilia huu mlolongo nikaona kama vile ni mgumu mno kufanikisha naomba kwenu wanabaraza kujuzwa kama ndio utaratibu au wameamua tu kuniwekea vikwazo ili nisifurahie mkate pamoja na familia yangu pia nilitaka usaidizi kwa aliye mjuzi namna rahisi ya kuweza kurudishwa kazini.
Natanguliza shukrani.