Nawezaje kurudishwa kazini baada ya kufukuzwa kazi?

Nawezaje kurudishwa kazini baada ya kufukuzwa kazi?

Pole sana mkuu mimi siwezi kuhukumu mwenye makosa ni nani kati yako wewe na mkuu wa shule kwasababu sijasikiliza upande wa pili ambao ni mkuu wa shule.

Ila kama ulifanya kuondoka kazi kwa jeuri yako pole sana na inawezekana vipi mkuu wa shule anaona tumbo lako limejaa afu yeye akufukuze kazi?

Any way mimi ni mwakilishi wa wahitimu wasio na ajira naomba nikukaribishe mtaani, karbu sana.
 
Hilo ni kosa la utoro kazini na bilashaka Tume ya utumishi wa walimu (T.S.c) walichukua hatua zifuatazo
1.Kukupa notisi ya kueleza kosa lako
2.kukuhitaji kujieleza ndani ya siku 14 Kwa maandishi
3.Kama ulikataa kosa kuundiwa kamati na kukuhojiwa ana Kwa ana
Makosa ya utoro wa kuanzia siku tano na kuendlea ni miongoni mwa makosa makubwa na adhabu yako ndo kma hiyo(kufukuzwa kazi,onyo au kushushwa cheo)



Hatua mpaka Tsc wanachukua uamuzi wa kufukuza kazi inamaana umeshindwa kuwashawishi Kwa maana wewe unakosa lakini kujifanya huna kosa na kujua Sana Sheria, ninvyo jua Mimi TSC ni chombo cha kumtetea mwalimu lakn inategemea unavyo jieleza nidhamu yako na vitu vingne mfano rekodi yako ya matukio yako ya nyuma n.k

Baada ya kufukuzwa kazi utakaa mwaka mmoja na Kama utahitaji kurudi kazini utawafuata TSC watkupa muongozo wa kurudi kazini lakini watahitaji wajiridhishe Kama tabia na mwenendo wako umebadilika njia ya kujua ni kupitisha barua kuanzia serikali za mitaa na sehemu unazofanyia ibada.

Panachangamoto kubwa Kwa watumishi baadhi kutokujua Sheria za kazi au wakt mwingne hata kanuni ndogo ndogo au muongozo inayotolewa na wizara husika japo zipo na zmeandikwa tena Kwa lugha rahisi.

Ushauri wangu teyari umeshatumikia adhabu ya mwaka mmoja fuata hizo taratibu uweze kurudishwa kazini hakuna shortcut zaidi ya barua kutoka tsc ya kurudishwa kazini kwasababu wao ndo chombo kinachosimamia mienendo ya walimu na vitu vingne
Case closed katika wachangiaji wote wewe ndiye uliyeoffer solution kwa tatizo linalomkabili.
Usipozingatia hapa utakuwa mtu mjeuri jeuri tu.
 
Habari zenu wakuu,

Mimi ni mwalimu idara ya sekondari katika mkoa wa Mara. Niliwahi kuugua ugonjwa wa tumbo kujaa na kuvimba ambao kule Mara ni maarufu kwa jina la passport size huwa inatokana na kulogwa.

Nilihangaika kutafuta uponyaji wake kwa njia ya hospitali hali ikawa sivyo hadi niliporudi kwa wenyeji wakanipeleka kwa mtaalam mmoja (kalumanzila) aliyekuwa anaishi nchi ya Kenya akanipa dawa kwenye kikombe, yeye kutibu kwake anatumia hiyo dawa yake tu kama alivyo yule babu wa Loliondo.

Nilipona lakini nilipewa masharti ya kutokula chapati kwani ilidaiwa kuwa nililogewa kupitia chapati.

Maisha yalisonga lakini nikajikuta nimekula chapati tena na kuja kuugua tena ule ugonjwa, nikapelekwa tena na tena kwa ajili ya dawa kwa kweli maisha yangu yalikuwa na mitihani kwa staili hiyo.

Nilitamani kuhama lakini nilipofika halmashauri kulikuwa na tangazo kuuubwa lililosema UHAMISHO UMESITISHWA. Baada ya muda tena niliugua safari hii nilichukia na morali ya kazi ilikatika nikaamua kwenda kwetu Tanga nikahangaika huko mpaka nikaweza kupona kabisa.

Tatizo likaja namna nilivyoondoka kwani mkuu wangu alikataa kunipa ruhusa nikaondoka kwa kulazimisha maana niliona kama wanafurahia kuugua kwangu.

Niliporudi nikakutana na barua ya kufukuzwa kazi na nilipofuatilia wakawa wakali kama mbogo sikukata tamaa nikaenda tena na tena hadi kufika mwaka huu wakaniambia ili niweze kurudi kazini natakiwa niandike barua ya kuomba kuajiriwa upya katika halmashauri nyingine tofauti na ile niliyokuwa nimeajiriwa mwanzo nikiambatanisha vitu vifuatavyo
  1. Nakala ya barua ya kufukuzwa kazini
  2. Nakala ya barua ya kuomba kuajiriwa upya iliyoandikwa kwenda katika halmashauri niliyokubaliwa kuwa nitapata nafasi (yaani hapa inatikiwa niombe kwanza nafasi nikubaliwe kwa maandishi ndio niandike tena barua hiyo nikiambatanisha hiyo nakala)
  3. barua za wadhamini watatu wanaonishuhudia kuwa mwenendo wangu ni wa kukubalika katika jamii, wadhamini hao watatu kila mmoja atoke katika mojawapo ya makundi yafuatayo:
    • Kiongozi wa kisiasa - Mbunge/Diwani
    • Kiongozi wa kiroho - Mchungaji, shehe, padri, askofu
    • kiongozi wa kiutawala - DAS, Afisa tarafa, DC
Baada ya hapo TSC atawasilisha maombi hayo kwa kamati ya TSC wilaya na kamati ya wilaya ikiridhia maombi hayo yatawasilishwa TSC makao makuu kwa hatua zaidi ya kuniombea kibali kwa katibu mkuu utumishi cha kuajiriwa upya kazini, baada ya hapo kama katibu mkuu akiridhia ndio niajiriwe upya.

Nimefuatilia huu mlolongo nikaona kama vile ni mgumu mno kufanikisha naomba kwenu wanabaraza kujuzwa kama ndio utaratibu au wameamua tu kuniwekea vikwazo ili nisifurahie mkate pamoja na familia yangu pia nilitaka usaidizi kwa aliye mjuzi namna rahisi ya kuweza kurudishwa kazini.

Natanguliza shukrani.
Ulilishwa dawa na wajita ile ya kuvimbisha tumbo.

Duh, pole sana mkuu
 
Kwani wewe ni jinsia gani. Kama ni mwanamke na hujawai mpa boss sukari basi mpelekee atakurudisha ila kama ulikuwa unampa bac jua kapata sukari tamu zaidi kaamua nafasi yako kuweka mwingine.

Kwa part ya mwanaume binafsi huwa sirecommend mwanaume kufanya kazi za kuajiriwa. Hivi uloshajiuliza, siku ukifa wanao unawaachia nini. Mwanaumeunatakiwa utengeneze business empire ambayo hata watoto wako wataridhi. Tijaribu kuiga hawa wahindi na waarabu.
 
Hujamuahidi demu kumuowa alaf ukamtema kweli? Maana huko Kanda ya ziwa kula demu ila usifanye kosa la kumuahidi kumuowa alaf umuache haki ya nani unalogwa Kuna mmoja nywele hazioti na asimamishi
 
Zile mbinu ulizotumia kumteka dada wa kazi nenda kazitumie kumteka boss
 
kuwa makini usije ukatumia akiba yako kuhonga ili urudi kazini maana huenda ukabaki mtupu huna hata 100 na kazini usirudi, kama unao mtaji kidogo bora uanzishe biashara na nguvu zako uziweke huko pengine rizk yako iliyokua serekalini imeisha fanya biashara nyingine na Mungu atakusaidia mkuu
 
Ni PM nkushauri, ila usiondoke hapo kituoni. Je una nakala ya barua ya ruhusa?
Alilazimisha kuondoka inaonekana huyu hakuruhusiwa, pia inaonekana wakuu wake aliwaambia hapaswi kula chapati, na akawa anakula!
Lazima walimjaji kuona anafanya makusudi apate ruhusa.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Habari zenu wakuu,

Mimi ni mwalimu idara ya sekondari katika mkoa wa Mara. Niliwahi kuugua ugonjwa wa tumbo kujaa na kuvimba ambao kule Mara ni maarufu kwa jina la passport size huwa inatokana na kulogwa.

Nilihangaika kutafuta uponyaji wake kwa njia ya hospitali hali ikawa sivyo hadi niliporudi kwa wenyeji wakanipeleka kwa mtaalam mmoja (kalumanzila) aliyekuwa anaishi nchi ya Kenya akanipa dawa kwenye kikombe, yeye kutibu kwake anatumia hiyo dawa yake tu kama alivyo yule babu wa Loliondo.

Nilipona lakini nilipewa masharti ya kutokula chapati kwani ilidaiwa kuwa nililogewa kupitia chapati.

Maisha yalisonga lakini nikajikuta nimekula chapati tena na kuja kuugua tena ule ugonjwa, nikapelekwa tena na tena kwa ajili ya dawa kwa kweli maisha yangu yalikuwa na mitihani kwa staili hiyo.

Nilitamani kuhama lakini nilipofika halmashauri kulikuwa na tangazo kuuubwa lililosema UHAMISHO UMESITISHWA. Baada ya muda tena niliugua safari hii nilichukia na morali ya kazi ilikatika nikaamua kwenda kwetu Tanga nikahangaika huko mpaka nikaweza kupona kabisa.

Tatizo likaja namna nilivyoondoka kwani mkuu wangu alikataa kunipa ruhusa nikaondoka kwa kulazimisha maana niliona kama wanafurahia kuugua kwangu.

Niliporudi nikakutana na barua ya kufukuzwa kazi na nilipofuatilia wakawa wakali kama mbogo sikukata tamaa nikaenda tena na tena hadi kufika mwaka huu wakaniambia ili niweze kurudi kazini natakiwa niandike barua ya kuomba kuajiriwa upya katika halmashauri nyingine tofauti na ile niliyokuwa nimeajiriwa mwanzo nikiambatanisha vitu vifuatavyo
  1. Nakala ya barua ya kufukuzwa kazini
  2. Nakala ya barua ya kuomba kuajiriwa upya iliyoandikwa kwenda katika halmashauri niliyokubaliwa kuwa nitapata nafasi (yaani hapa inatikiwa niombe kwanza nafasi nikubaliwe kwa maandishi ndio niandike tena barua hiyo nikiambatanisha hiyo nakala)
  3. barua za wadhamini watatu wanaonishuhudia kuwa mwenendo wangu ni wa kukubalika katika jamii, wadhamini hao watatu kila mmoja atoke katika mojawapo ya makundi yafuatayo:
    • Kiongozi wa kisiasa - Mbunge/Diwani
    • Kiongozi wa kiroho - Mchungaji, shehe, padri, askofu
    • kiongozi wa kiutawala - DAS, Afisa tarafa, DC
Baada ya hapo TSC atawasilisha maombi hayo kwa kamati ya TSC wilaya na kamati ya wilaya ikiridhia maombi hayo yatawasilishwa TSC makao makuu kwa hatua zaidi ya kuniombea kibali kwa katibu mkuu utumishi cha kuajiriwa upya kazini, baada ya hapo kama katibu mkuu akiridhia ndio niajiriwe upya.

Nimefuatilia huu mlolongo nikaona kama vile ni mgumu mno kufanikisha naomba kwenu wanabaraza kujuzwa kama ndio utaratibu au wameamua tu kuniwekea vikwazo ili nisifurahie mkate pamoja na familia yangu pia nilitaka usaidizi kwa aliye mjuzi namna rahisi ya kuweza kurudishwa kazini.

Natanguliza shukrani.
Pole sana mkuu.

Mimi nakushauri kuwa utangaze mgogoro kwa kuwasilisha malalamiko yako kwa tume ya usuluhishi wa migogoro makazini (Commission for Mediation and abitration-CMA). Wa contact kwanza hawa jamaa uwaelezee issue yako namna ilivyokaa, then wao watakupa ushauri wa nini cha kufanya hatua kwa hatua, na ni namna gani ya kujaza fomu zao za kutangaza mgogoro na kuanzia hapo muajiri wako ataitwa na shauri litaanza kusikilizwa.

Hawa huwa ni watu useful sana kwa waajiriwa, sema wabongo wengi bado hatujawajua na hatujajua kazi zao.

Hatua ya kwanza, cheki na muwakilishi wa ofisi ya CMA hapo Musoma, contacts zake hizi hapa;
CMA MUSOMA, MARA

Mukendo Street, Near Post Office, P.o.Box 260, Musoma. In charge Honourable Haruna Soleka Mobile No: 0759272218.


Pia kwa maelezo zaidi unaweza ingia kwenye website yao Home | Commission for Mediation and Arbitration kuna maelezo mbalimbali huko wametoa kuhusu namna ya kufungua malalamiko ya kuachishwa kazi isivyo halali, etc.
Ila, cha muhimu zaidi wasiliana na hao jamaa wa CMA wa Musoma, utapata mwanga na watakufungua macho sana.
Erickford4
 
Kwa wenyeji wanafahamu kule ukila chakula hadharani ujue upo hatarini kupigwa kipapai.. mimi nilikuwa bachela nikawa napenda kunywa chai mgahawani ndio wakaniotea hukohuko.
Pole sana mkuu,najaribu kulibeba tatizo lako lakini nashindwa,Mungu akupiganie.

Najaribu kuwaza kwa sauti sasa kinachowufanya wakupige kipapai ni nini??

Au kuna vitu unawakera?
 
Kawaida yenu wanaJF mtu akifungua uzi mnafukua makaburi kuanza kuchunguza nyuzi za nyuma... Kifupi suala la biashara nililifanya kama mbadala kwa sababu nilikatishwa moyo kuwa siwezi kurudi katika nafasi yangu nikatafuta pakujishikiza ili niweze kujikwamua na ugumu wa maisha... Kuhusu suala la Yesu nimefurahi kuwa niliwahi kukuhubiria na nimekuwa mmoja wa washauri wako waliokufanya ukaacha mambo ya waganga
Unamhubiri yesu huku unaenda kwa mganga crazyyyyy!!!

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Pole sana mkuu.

Mimi nakushauri kuwa utangaze mgogoro kwa kuwasilisha malalamiko yako kwa tume ya usuluhishi wa migogoro makazini (Commission for Mediation and abitration-CMA). Wa contact kwanza hawa jamaa uwaelezee issue yako namna ilivyokaa, then wao watakupa ushauri wa nini cha kufanya hatua kwa hatua, na ni namna gani ya kujaza fomu zao za kutangaza mgogoro na kuanzia hapo muajiri wako ataitwa na shauri litaanza kusikilizwa.

Hawa huwa ni watu useful sana kwa waajiriwa, sema wabongo wengi bado hatujawajua na hatujajua kazi zao.

Hatua ya kwanza, cheki na muwakilishi wa ofisi ya CMA hapo Musoma, contacts zake hizi hapa;
CMA MUSOMA, MARA

Mukendo Street, Near Post Office, P.o.Box 260, Musoma. In charge Honourable Haruna Soleka Mobile No: 0759272218.


Pia kwa maelezo zaidi unaweza ingia kwenye website yao Home | Commission for Mediation and Arbitration kuna maelezo mbalimbali huko wametoa kuhusu namna ya kufungua malalamiko ya kuachishwa kazi isivyo halali, etc.
Ila, cha muhimu zaidi wasiliana na hao jamaa wa CMA wa Musoma, utapata mwanga na watakufungua macho sana.
Erickford4
Brother usichanganye mambo huyo mgogoro ushafunguliwa na muajiri wake ambae ni halmashauri yake husika(mkurugenzi)

Mkurugenzi alimpeleka Tsc ambao wao ndo watatuzi wa mgogoro baina ya walimu na muajiri ( kumbuka mkurugenzi Hana mamlaka kisheria kumfukuza mwalimu kazi au kutoa adhabu yoyote) chombo chenye mamlaka ya kutoa adhabu au kutatua mgogoro Kwa walimu ni tume ya utumishi wa walimu (TSC) ambapo katibu wake ni presidential appointee kuna ngazi ya Kwanza ya wilaya harafu kuna Tsc taifa
Zamani kulikuwa na tsc wilaya ,taifa na mkoa lakini tsc mkoa
Iliondolewa baada ya kubadilishwa toka tsd kwenda tsd

Uamuzi ukitolewa na TSC wilaya Kama usipo ridhia maamuzi utakata rufaa ndani ya siku 40 kwenda ngazi ya Tsc taifa.

Kwakifupi Sana maana katika hili kuna mengi ya kuelekeza lakini ngoja nimshauri tena

Hakuna chombo kinaweza kutengua uamuzi wa TSc kwasababu hawa ni chombo huru na kinafanya uamuzi pasipo kupendelea au kuonelea

Pili baada ya adhabu kutolewa ulipewa nafasi ya kukata rufaa ulikata?

Tatu uamuzi ulikuwa umefukuzwa KAZI lakni baada ya mwaka mmoja umepewa taratibu za kurudi kazini
Sasa hapo shida ipo wapi?

Hebu fuata hizo taratibu uone Kama hutorudi kazini
 
Brother usichanganye mambo huyo mgogoro ushafunguliwa na muajiri wake ambae ni halmashauri yake husika(mkurugenzi)

Mkurugenzi alimpeleka Tsc ambao wao ndo watatuzi wa mgogoro baina ya walimu na muajiri ( kumbuka mkurugenzi Hana mamlaka kisheria kumfukuza mwalimu kazi au kutoa adhabu yoyote) chombo chenye mamlaka ya kutoa adhabu au kutatua mgogoro Kwa walimu ni tume ya utumishi wa walimu (TSC) ambapo katibu wake ni presidential appointee kuna ngazi ya Kwanza ya wilaya harafu kuna Tsc taifa
Zamani kulikuwa na tsc wilaya ,taifa na mkoa lakini tsc mkoa
Iliondolewa baada ya kubadilishwa toka tsd kwenda tsd

Uamuzi ukitolewa na TSC wilaya Kama usipo ridhia maamuzi utakata rufaa ndani ya siku 40 kwenda ngazi ya Tsc taifa.

Kwakifupi Sana maana katika hili kuna mengi ya kuelekeza lakini ngoja nimshauri tena

Hakuna chombo kinaweza kutengua uamuzi wa TSc kwasababu hawa ni chombo huru na kinafanya uamuzi pasipo kupendelea au kuonelea

Pili baada ya adhabu kutolewa ulipewa nafasi ya kukata rufaa ulikata?

Tatu uamuzi ulikuwa umefukuzwa KAZI lakni baada ya mwaka mmoja umepewa taratibu za kurudi kazini
Sasa hapo shida ipo wapi?

Hebu fuata hizo taratibu uone Kama hutorudi kazini
Ahsante kwa mchango wako. Mimi sijui chochote kuhusu haya mambo, nimejaribu tu kumuelekeza jamaa sehemu ambayo anaweza kupata muongozo sahihi. Ndio maana nikamwambia acheki na hao watu wa CMA, kama maelezo yako uliyoyatoa yako sawa ina maana jamaa wa CMA atamwambia hivyo hivyo pia. Ni muhimu apate ushauri wa kitaalamu kutoka kwa huyo mwakilishi wa CMA huko Musoma, ndio maana nimecopy na ku paste details za huyo mwakilishi kutoka website ya CMA ili awasiliane nae. Maana wao watakua na weledi zaidi na uzoefu wa kudeal na hayo mambo.
ngurutu
 
Ahsante kwa mchango wako. Mimi sijui chochote kuhusu haya mambo, nimejaribu tu kumuelekeza jamaa sehemu ambayo anaweza kupata muongozo sahihi. Ndio maana nikamwambia acheki na hao watu wa CMA, kama maelezo yako uliyoyatoa yako sawa ina maana jamaa wa CMA atamwambia hivyo hivyo pia. Ni muhimu apate ushauri wa kitaalamu kutoka kwa huyo mwakilishi wa CMA huko Musoma, ndio maana nimecopy na ku paste details za huyo mwakilishi kutoka website ya CMA ili awasiliane nae. Maana wao watakua na weledi zaidi na uzoefu wa kudeal na hayo mambo.
ngurutu
Tupo pamoja brother lengo kujenga
 
Ulifanyaje biashara wakati ulikua umerogwa tumbo limeshiba ndindiii kiasi kwamba ulishindwa kufundisha darasani? JF haipotezi ushahidi Mkuuu ndio maaana unaona hadi wadau wameanza kupandisha nyuzi zako za zamani hapa hapa kukupa fact jinsi unavyozingua.
Usiache nkakutukana nikafungiwa.. kwa hiyo huyo biashara niliifanya mwaka 2017? We ukiugua unalala tu ndani ndio matatizo ya watoto kujaa jf umezoea kulishwa na baba au kwa shemeji umiza kichwa kuwaza sio makalio
 
Jamaaa mpuuzi sana anaanza kusingizia Oooh amelogwa sjui Rorya, oooh wachawi sana Mara. Utapeli pia unaanza hiv hivi ukiona Member analeta stori za kutunga hapa jamvini ujue anakoelekea ni kupiga watu pesa. Ameboa sana ujue
Uzuri wake nyuzi zangu za nyuma nilijielezea matatizo niliyopataga hadi kupelekea kuacha kazi na kuachana na mwanamke wangu ambaye nilizaa naye mtoto mmoja.. Usipende kukurupuka.. Nimekuomba wapi hela?
 
Back
Top Bottom