Nchi kumi za kutembelea katika kipindi cha miaka mitano

Nchi kumi za kutembelea katika kipindi cha miaka mitano

Aisee mm Namibia ndo nchi naham sana nikaitembelee nchi kubwaaa harafu watu kiduchu.Nimetokea kuipenda tu ile nchu japo sehem kubwa ni jangwa ila ni nchi poa sana maana hua naangalia sana youtube.Mungu ani bless nikatimize ndoto zangu.
Yes mkuu Namibia ipo super, Windhoek jiji dogo ila lipo safi sana, wajerumani waliijenga vema,tembelea pia Katutura township, walvis bay(bandari hii ni mshindani wetu,Dar Port),katima mulilo, Rundu, etc etc ,na nchi ipo peace ya kweli SIO YA LAZIMA
 
Hapo labda DUBAI, uturuki na china(macau) huko tutaenda sote
ila haswa haswa nina mpango wa kwenda Brazil, hapa unisamehe sintokwenda na wewe..
Hata mimi sitaki safari yoyote ya kwenda na wewe🤣🤣🤣
 
Wiki mbili za mwanzo za mwaka ujao 2024 nimepanga kuchukua likizo fupi itakayoniwezesha kutembelea nchi jirani tatu.
Nitaanza na Bujumbura Burundi, nivuke DRC- Bukavu na Goma, Kisha nirudi kupitia Kigali Rwanda.
Mwaka 2025 nimepanga kutembelea Namibia na Zimbabwe. Inshallah!.
 
Kabla ya kwenda nje ya Tanzania natamani nimalize kuizinguka Tanzania yote Kwa gari binafsi.
Napenda kusafiri safari ndefu kuliko kitu kingine chochote duniani huwa moyo wangu unapata Amani sana
Upo kama mimi, napenda kusafiri sana kuijua nchi yangu kwanza halafu huko kwingine nitaenda tu
 
Hata mimi sitaki safari yoyote ya kwenda na wewe🤣🤣🤣
Ewaa, AFAZALI...
😂😂

kanuni za kutembea, bar, club au kusafiri kwenda kula burudani huendi na mchumba, usije kosa mambo mazuri huko buree😂🤣
 
Kuna nini cha kwenda kutalii Nigeria?

Kwenye hiyo list naondoa Nigeria na Canada naweka Madagascar na Brazil
Muda ukiruhusu, nitapenda kukaa Nigeria kwa muda kama mwezi mmoja hivi. Nataka nijue siri ya wao kutapakaa dunia nzima kwa wingi.

Wakenya ni wajasiri, lakini nafikiri Wanigeria wametia fora.
 
Mkuu, wewe umeshafika mikoa mingapi?

Kwa Zanzibar niliishia Unguja. Pemba nitaenda wakati mwingine nipatapo fursa.

Kwa upande wa Tanganyika, nimebakiza mikoa miwili tu, Mtwara na Lindi. Nilikuwa na mpango wa kufika huko mwaka huu lakini nimeamua kuahirisha hadi mwakani. Muda kama hautaniruhusu.
Wewe umetisha sanaaa!! Kama umebakiza mikoa miwili Tanzania umejitahidi Sana na Una haki ya kusafiri nje ya nchi..
Mimi bado mikoa mingi Sana sijafika hasa nyanda za juu kusini iringa,mbeya na songea Ila Kwa mikoa ya kusini naijua vichochoro vyote
 
We umetembelea ipi kati ya hizo? Au
Umepanga kutembelea nchi ngapi katika kipindi cha miaka 5 ijayo?

Binafsi, ninapenda sana kusafiri, lakini kwa sababu ya kiwango cha kipato, bado sijazimaliza hata nchi za Afrika Mashariki.

Mpaka sasa, nchi nilizokwishatia miguu yangu ni Kenya, Uganda na Burundi.

Ikimpendeza Mungu, mwishoni mwa mwaka huu nitaenda Rwanda na South Africa.

Kwa sababu safari ya South Africa itakuwa kwa basi, nitaweza kupitia nchi kadhaa, labda Zambia, Zimbabwe, n.k. Bado sijaamua route, lakini huenda nikaenda kwa basi nikarudi kwa ndege, au vinginevyo.

Kwa hiyo, nimeziengua Rwanda na S. A kwenye nchi za kuzitembelea katika miaka mitano ijayo. Ninahesabu nimeshazitembelea.

Hizi ndizo nchi nitakazozitembelea katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2024:
1. Misri

2. Nigeria

3. Dubai - ( UAE)

4. Israel

5. Ugiriki

6. Uturuki

7. China

8. Uingereza

9. Marekani

10. Canada.

Natamani kwamba ifikapo Disemba 2028, niwe nimeshazitembelea nchi zote hizo hapo juu, na zaidi, ikiwezekana.

Wewe umepanga kutembelea nchi zipi?
Copy and paste? Oga
 
Wewe umetisha sanaaa!! Kama umebakiza mikoa miwili Tanzania umejitahidi Sana na Una haki ya kusafiri nje ya nchi..
Mimi bado mikoa mingi Sana sijafika hasa nyanda za juu kusini iringa,mbeya na songea Ila Kwa mikoa ya kusini naijua vichochoro vyote
Ni hatua! Kama ingelikuwa ni darasa, nina uhakika umeshavuka level ya kalamu ya mkaa na sasa unatumia ya wino.
 
Wewe umetisha sanaaa!! Kama umebakiza mikoa miwili Tanzania umejitahidi Sana na Una haki ya kusafiri nje ya nchi..
Mimi bado mikoa mingi Sana sijafika hasa nyanda za juu kusini iringa,mbeya na songea Ila Kwa mikoa ya kusini naijua vichochoro vyote
Siyo Tanzania mkuu, bali upande wa bara pekee. Pemba bado sijatia mguu kiongozi.
 
Back
Top Bottom