Nchi nzima wananchi wameongeza chuki dhidi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)

Nchi nzima wananchi wameongeza chuki dhidi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)

Sanaa ya vita haijawahi kuwa wazi kwa kila mtu.

Bila ya kuanza na kibwagizo hiki --- "kwa mawazo yangu ..." Ni wazi kuwa hujajitendea haki.

In war devide them, separate them and don't deny them of an exit strategy.

Vinginevyo, mbona hata panya atakumaliza?

Tafakari chukua hatua.
Mama watamtesa sana wafuasi wa mwendazake. Ikumbukwe kuwa hawa ni watu waliojipanga kutawala nchi milele na milele kifo cha Jiwe kimewauma sana. Na Mama anajipanga taratibu.
 
CCM Asilia ikitaka kurejesha utengamano nchini, inabidi itambue CCM Mpya ilivyokengeuka na ijisahihishe. Ili kurejesha imani kwa waTanzania inapata kuelewa haya yafuatayo :

Katika vyama vyote vya siasa vilivyosajiliwa Tanzania kwa muda huu 2021, CCM ni chama dhaifu kupita vyote hata cha CHAUMA chini ya mwenyekiti mzee Hashim Rungwe ni chama thabiti kuliko CCM.

Sababu ni kuwa mwendazake baada ya kuua mihimili ya dola, mahakama na bunge akamalizia kukimaliza chama kilichomweka madarakani. Muda huu CCM haina Mwenyekiti wa Taifa wala Katibu Mkuu wa chama.

Hali hii imefikiwa kwa vile CCM ilishindwa kumdhibiti mwendazake kufanya mambo yake ya kuwaondoa vigogo tishio ndani ya CCM na kuleta "wageni" na kuwazawadia vyeo kwa sharti wamuimbie mapambio anayopenda kusikia.

Kina Bashiru Ally Kakurwa, Humphrey Polepole ni aina ya viongozi ambao viongozi walikuwa hawawezi kumuambia chochote Mwenyekiti ambacho wao wanaamini kinyume na kama kina Nape Nnauye , January Makamba na hata wazee kama Yusuf Makamba, Abdulrahman Kinana.

Tukija katika dola, mwendazake aliiyumbisha na kuivuruga kabisa mfumo wa utumishi serikalini yaani civil service. Aliwachukua watu wasio na ujuzi wa utumishi serikalini na kuwapachika vyeo vya u DED, Makatibu Wakuu na kujaribu kuhitimisha pigo kuu la kuua utumishi serikalini kwa kumuapisha Dr. Bashiru Ally Kakurwa kama Katibu Mkuu Kiongozi ambaye ktk historia ndiye Katibu Mkuu aliyekuwa hana uzoefu kabisa ktk utumishi wa serikali kuu.

Tukija katika mhimili wa Mahakama tuliona alivyouburuza na kuwapa vyeo vya ujaji kwa vigezo dhaifu mfano kuandika hukumu kwa kiSwahili huku kesi hiyo ikiwa ni nyepesi mno.

Bunge pia lilipelekeshwa kwa Spika kuelekezwa kuwashughulikia wabunge wake kwa kuwatoa nje ili waje kushughulikiwa na mwendazake nje ya Bunge. Wabunge wa CCM pia hawakuepuka kipigo cha kisiasa toka kwa mwendazake, ktk kuelekea uchaguzi wa 2020 walishughulikiwa na 'wajumbe' na kama waliweza kupenya walikutana na rungu la Mwenyekiti wa CCM.

Vyeo katika ngazi za uwaziri tumeona waliojiunga mwishoni ktk CCM toka vyama mbadala walitunikiwa vyeo huku wale waliokulia ktk UVCCM na Jumuiya za CCM toka utotoni wakiambulia kuwa backbenchers. Yote hii ilikuwa kuonesha CCM imekufa na sasa mtu mmoja ndiyo kila kitu hivyo wasifurukute au kuwashwa kuhoji au kutoa mawazo mbadala.

Tanzania ilikuwa inaelekea kubaya, lakini kama uzi huu ulivyotabiri wa mwana JF Mvuv, inaonekana ndani ya CCM ndiyo kulikuwa na fukuto kubwa la kutokubaliana na kinachoendelea na sasa tunasikia baada ya mwendazake kuondoka, wabunge wa CCM na SPIKA mwanaCCM wanaanza kutoa maoni ambayo yanaonekana na waimba pambio wa mwendazake kuwa ni unafiki.

Ili kuirejesha Tanzania katika mstari wa haki ikiwemo na CCM yenyewe Asilia kuweza kuaminika kusimamia haki na katiba ya nchi, Tume ya Kijaji lazima iundwe.

Tume ya KiJaji ipewe hadidu rejea Kuchunguza ukiukwaji mkubwa wa katiba, haki za binadamu na ukatili uliotendeka ktk utawala wa CCM iliyojiita CCM Mpya.
CCM asilia ni ipi na imeofanyia nini Tanzania
 
Kwa sisi tuliofatilia hali ya kisiasa na kijamii kuanzia kuingia kwake madarakani 2015 na uchaguzi wa muhula wa pili 2020 tulijua kabisa na kubashiri janga linaloenda kuikabiri nchi yetu.

Kwa sisi tulioona na kushuhudi uhuni ule wa uchaguzi, matumizi mabaya ya fedha kudhibiti Haki na demokrasia nchini tulijua kabisa baada ya uchaguzi hali ya kiuchumi itakuwa mbaya sana. Nyote ni mashuhuda sasa.

Nchi nzima si wanaccm, chadema wala Chauma. Si wanasiasa hadi wasio na siasa wote wameichukia ccm hasa iliyokita mizizi na fikra za John Pombe magufuli, fikra za kikandamizaji.

Kwa wale tuliosikia zile tetesi kwamba Hayati alikodisha vikosi vya cyber kuja kuchakachua mifumo mingi ya kiteknolojia na internet ili kurahisisha mazingira ya kushinda uchaguzi tuliwaza kabisa kuwa kama ni kweli hizo pesa anazowalipa zinatoka wapi? au ndio amekomba pesa zote za hazina? Kuna wengine wanafika mbali na kusema huenda pesa alizokopa world bank na Uchina kwa ajili yanujenzi wa SGR na Stigler ndio hizo zilitumika ktk mikakati michafu ya uchaguzi october 2020 na hivyo tunalipa ghalama.

Sasa Awamu ya sita imetuchanganya. Huwezi kumjua Mpiga mapambio wa zamani na mpinzani wa zamani. Wote wamekuwa kitu kimoja. Adui wao amekuwa mmona tu, naye ni CCM.

Asante sana CCM kqa kutuunganisha. Sasa ongeza na tozo zingine ili tujenge nchi kwa haraka zaidi.

CCM nambali one.
Maendeleo hayapatikani bila ya KUIFUNGA MIKANDA.....

Dr.Mwigulu yu sahihi.....

#KaziIendelee
 
Umeandika upuuzi mtupu! Kwa upinzani upi haswa wa kumfanya Magufuli atumie gharama kupora uchaguzi?? Yaani hata Magufuli asingefanya kampeni ilikuwa wazi kuwa angeshinda kutokana na kupendwa na kukubalika kwake katika mioyo ya watanzania na hakuwa na mpinzani wa kumfikia hata robo.CCM ya sasa ina/itachukiwa na wanaCCM kadhaa kwa kuacha kufuata misimamo ya Magufuli na kukengeuka na kuruhusu juhudi zote zilizofanyika katika kipindi chake katika kuinua uchumi kuwa bure.Mfano takwimu zinaonyesha tangu afariki uchumi umeshuka,Wizi,Uzembe na ubadhirifu umerejea kwa kasi,Hakuna uwajibishaji,Mifumuko ya bei,Mafuta na miamala ya simu,Kuruhusu chanjo ya Covid,Safari zisizo na tija kwa taifa,Ujambazi kurejea ni baadhi tu yatakayowafanya wanaCCM kuchukia serikali iliyopo kwa kushindwa kusimamia fikra za hayati Magufuli na wengine kumpinga hadharani wakati huu ambapo hatupo naye.Watanzania si wajinga,Tuna macho na tunaona yanayoendelea.
Umeandika maelezo mazuri kabisa
 
Vijana wa bavicha ni wajinga sana,!
.
Mlikuwa mnasema Magufuli amewabana na juzi tu haoa nkawa nnafurahia kifo chake mkisema mnapumua!

Alafu ukome kutujumlisha wote! Mimi siyo miongoni mwa hao raia unaosema! Utusitusemee tafadhali
Vijana wa uvccm ni mataahira sana
 
Nachoshukuru polisi nao wapo kwenye tozo wanapelekwa kama mapunda kama wao hawajui kulinda raia na mali zao ni jukumu lao
Na pia Polisi wanatusaidia kuisagia kunguni CCM na Serikali yake kwa kuendeleza ukatili kwa wapinzani
 
Watanzania hawa hawa. Bado sana. Tunapoelekea ni kubaya zaidi. Mtu maskini anatawalika kirahisi zaidi

200864320_4544197945630554_579101476768049775_n.jpg
 
Kwa sisi tuliofatilia hali ya kisiasa na kijamii kuanzia kuingia kwake madarakani 2015 na uchaguzi wa muhula wa pili 2020 tulijua kabisa na kubashiri janga linaloenda kuikabiri nchi yetu.

Kwa sisi tulioona na kushuhudi uhuni ule wa uchaguzi, matumizi mabaya ya fedha kudhibiti Haki na demokrasia nchini tulijua kabisa baada ya uchaguzi hali ya kiuchumi itakuwa mbaya sana. Nyote ni mashuhuda sasa.

Nchi nzima si wanaccm, chadema wala Chauma. Si wanasiasa hadi wasio na siasa wote wameichukia ccm hasa iliyokita mizizi na fikra za John Pombe magufuli, fikra za kikandamizaji.

Kwa wale tuliosikia zile tetesi kwamba Hayati alikodisha vikosi vya cyber kuja kuchakachua mifumo mingi ya kiteknolojia na internet ili kurahisisha mazingira ya kushinda uchaguzi tuliwaza kabisa kuwa kama ni kweli hizo pesa anazowalipa zinatoka wapi? au ndio amekomba pesa zote za hazina? Kuna wengine wanafika mbali na kusema huenda pesa alizokopa world bank na Uchina kwa ajili yanujenzi wa SGR na Stigler ndio hizo zilitumika ktk mikakati michafu ya uchaguzi october 2020 na hivyo tunalipa ghalama.

Sasa Awamu ya sita imetuchanganya. Huwezi kumjua Mpiga mapambio wa zamani na mpinzani wa zamani. Wote wamekuwa kitu kimoja. Adui wao amekuwa mmona tu, naye ni CCM.

Asante sana CCM kqa kutuunganisha. Sasa ongeza na tozo zingine ili tujenge nchi kwa haraka zaidi.

CCM nambali one.

E0NhMwdXIAAW0HL (1).jpeg
 
Back
Top Bottom