Ndege ya Precision yazimika injini ikiwa angani

Ndege ya Precision yazimika injini ikiwa angani

Mbona hiyo kawaida sana.
Miaka ya 90 ndege ya ATC , wakati huo Fokker Friendship ilizima engine tukitoka Kigoma kuja Tabora, pembeni alikaa mzee mmoja maarufu mwanasiasa, simtaji.Baadaye ilirekebishwa engine tukatoka Tabora kuja Dar.
Engine zote zikafanya kazi.
ENGINE ya Pili nayo ikazima, hapo ndo nikaona mlango wa kuondoka duniani.
Maana nikafikiri kama engine ile mbovu ya kwanza ikizima na hatuna parachute, dunia ndo kwaheri.
Lakini tulifika Dar bila matatizo.
Hizo ndege Fokker50 zilisimamishwa baadaye maana zilizeeka sana.
Fokker Wulf walitengeneza ndege za Luftwaffe, jeshi la anga la Nazi Germany. Ilikuwa kampuni kubwa ila ikapotea na sasa iko kwenye consortium ya Airbus
 
Nawaza huyp dogo amejuaje kama engine moja imezima? While haoni dashboard? Nitoeni ushamba hapo
 
View attachment 2306678
Abiria ndani ya ndege ya Kampuni ya Precision, jana waliingiwa na hofu ya usalama wao baada ya injini moja kuzima ikiwa angani.

Ndege hiyo yenye namba PW 467 ikitokea Kahama, ikielekea Dar es Salaam kupitia Mwanza, ilizima injini baada ya dakika 51 kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza.

Hofu ilianza kutokea baada ya abiria mmoja, kijana wa kizungu, kuanza kupiga kelele, akiwaeleza wenzake waliokuwa wameketi jirani, kwamba injini imezima.

Baadaye abiria wengine waliingiwa hofu, huku baadhi wakisali, wakilia na wengine kuonekana wamejiinamia, huku wamefunika nyuso zao.

Baada ya abiria kuonekana 'wakipaniki' ndipo rubani wa ndege hiyo alitangaza kuwepo kwa hitilafu hiyo huku akieleza kwamba hali siyo ya kutisha sana.

"Abiria wetu wapenzi, ndege yetu imepata tatizo la kiufundi, injini moja imezima, lakini hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kwani, tunapanga kutua katika kiwanja jirani na hapa tulipo," alisema rubani huyo.

Hata hivyo, tulizo la mwana anga huyo halikuleta afueni ya wasiwasi kwa abiria wengi, waliendelea na hofu yao, huku wengine waliokuwa hawajatambua kinachoendelea wakiungana na wengine kusononeka.

Rubani alirejea tena kwa tangazo; "Abiria wetu wapendwa, tunasikitika kwa kilichotokea, nawaomba kuwa watulivu wakati sasa tunajiandaa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Tutatua ndani ya dakika 20."

Baada ya muda huo, ndege hiyo ilitua salama katika uwanja huo na abiria walishangilia. Wengine walipiga kofi, wengine wakipiga kelele za shangwe na wengine wakimshukuru Mungu.

Mmoja wa abiria aliyekuwamo ndani ya ndege hiyo, Simon Mkina, aliandika katika ukurasa wake wa Twitter na taarifa hiyo kusambaa dunia nzima, huku akipongezwa kwa kutoa taarifa hiyo mapema.
Elimu tu mtu wangu, ndege nyingi tu kama sio zote zinatengenezwa na uwezo wa kukamilisha kazi hata ikibaki na injini moja tu.

Ningekuwa kwenye hiyo ndege abiria wenzangu wangeniona chizi kwa kutoonesha hata lepe la paniki, na kuwashangaa wanaopaniki hata baada ya rubani kutoa maelezo kamili kabisa!

Hint: sijawahi kupanda ndege🤣😂😂😂
 
yeah kwa sababu midege hii ina power backup nyingi. kama ni engine moja tu imekufa yeah anaweza kwenda kwa muda huo. haya yana migenerator ya kuzalisha umeme kusaida kuendesha ndege, lakini pia ya batteries kama generator pia zitazingua
 
View attachment 2306678
Abiria ndani ya ndege ya Kampuni ya Precision, jana waliingiwa na hofu ya usalama wao baada ya injini moja kuzima ikiwa angani.

Ndege hiyo yenye namba PW 467 ikitokea Kahama, ikielekea Dar es Salaam kupitia Mwanza, ilizima injini baada ya dakika 51 kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza.

Hofu ilianza kutokea baada ya abiria mmoja, kijana wa kizungu, kuanza kupiga kelele, akiwaeleza wenzake waliokuwa wameketi jirani, kwamba injini imezima.

Baadaye abiria wengine waliingiwa hofu, huku baadhi wakisali, wakilia na wengine kuonekana wamejiinamia, huku wamefunika nyuso zao.

Baada ya abiria kuonekana 'wakipaniki' ndipo rubani wa ndege hiyo alitangaza kuwepo kwa hitilafu hiyo huku akieleza kwamba hali siyo ya kutisha sana.

"Abiria wetu wapenzi, ndege yetu imepata tatizo la kiufundi, injini moja imezima, lakini hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kwani, tunapanga kutua katika kiwanja jirani na hapa tulipo," alisema rubani huyo.

Hata hivyo, tulizo la mwana anga huyo halikuleta afueni ya wasiwasi kwa abiria wengi, waliendelea na hofu yao, huku wengine waliokuwa hawajatambua kinachoendelea wakiungana na wengine kusononeka.

Rubani alirejea tena kwa tangazo; "Abiria wetu wapendwa, tunasikitika kwa kilichotokea, nawaomba kuwa watulivu wakati sasa tunajiandaa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Tutatua ndani ya dakika 20."

Baada ya muda huo, ndege hiyo ilitua salama katika uwanja huo na abiria walishangilia. Wengine walipiga kofi, wengine wakipiga kelele za shangwe na wengine wakimshukuru Mungu.

Mmoja wa abiria aliyekuwamo ndani ya ndege hiyo, Simon Mkina, aliandika katika ukurasa wake wa Twitter na taarifa hiyo kusambaa dunia nzima, huku akipongezwa kwa kutoa taarifa hiyo mapema.
Tungesema tuwahi Kuwakagua 'Kibaiolojia' hao Abiria Wote waliokuwa na Hofu kutokana na Hitilafu hiyo ni kwamba 99.9999% yao lazima tu walikuwa wameshajisaidia Small and Big Haja kwa pamoja.
 
Napata shida kuelewa juu ya kuzima kwa engine moja na ndege na kuendelea na safari. Ndege za Precision Air hazina engine tatu; zote zina engine mbili, kila bawa imefungwa engine moja. Kuruka na kupaa kwa ndege hizi za engine mbili, ni lazima engine zote mbili zifanye kazi. Ikitokea engine moja ikazima, ndege hiyo haiwezi kuendelea na mwendo katika uelekeo wake, kwani engine moja inayofanya kazi itavuta upande mmoja na kupoteza direction. Nadhani kulikuwa na hitilafu tu ya engine, lakini sio engine kuzima. Kama ingekuwa na engine tatu; engine hii ya tatu ambayo haitegemeani na nyingine (unpaired), hata ikizima, ndege inaweza kwenda in the same direction, labda speed ndio itapungua, kwakuwa the turning torque is balanced.
 
Back
Top Bottom