Ndo nimemaliza C-section ya 6, nimechoka akili na mwili. Halafu kuna Wanasiasa kwa mwezi wanakula 11 M na bado wanajiongezea mshahara 40%

Umeshasema nje,je hizo nchi zina uchumi sawa na wa kwetu?

Hivi unadhani huo mshahara ni masikhara,hata hiyo Kenya waliotuzidi uchumi hawawalipi MD wao huo mshahara
 
Umeshasema nje,je hizo nchi zina uchumi sawa na wa kwetu?

Hivi unadhani huo mshahara ni masikhara,hata hiyo Kenya waliotuzidi uchumi hawawalipi MD wao huo mshahara
Tanzania sisi ni nchi tajiri sana tena sana. Tuna rasilimali nyingi sana za kuweza kufanya hayo yote. Hakuna kinachoshindikana! Hakuna nchi iliyoendelea bila kuwekeza kwenye afya na elimu haipo kabisa!
 
Mkuu,

Ukiwa Rais nishtue nirudi nyumbani 🤣🤣🤣🤣.

Na uwe Rais hata kesho.
 
Pole sana mkuu, kati ya watu ninaowaheshim na kuwapenda ni madaktari, siku nikiwa rais nitaboresha maslahi yao kwanza. Japo sio wote aisee mm ni mhanga wa madaktari wazembe nimepoteza watoto 3 wa kufuatana sababu ya uzembe wa kipuuzi sana tena wote 2 hosipitali ya mkoa na wa3 clinick zote nimeenda pale hawakujua wakampa mama alu in 1st tresemester ikaharibu mtoto naambiwa kila kitu kipo sawa nlienda kujifungulia private kwa gajrama kubwa ile dr anaangalia picha nilotoka nayo gov hospital akasema mbina kichwa cha mtoto kina maji. Akaniita pembeni akaniambia jikaze mtoto hataishi na kweli nlikaa naye 4 days akafa.
Pole sana mkuu kwa kufanya kazi kwa bidii
 
Mkuu,

Mimi nikupe hongera pamoja na majukumu mazito. Ile feeling ya kumdeliver mtoto salama na kwa mafanikio, huwa inaleta amani na furaha sana moyoni.

Poleni sana. On call ya less than 9 USD ni kuchoshana. Ila kwa kuwa uliridhia mwenyewe, basi wajibika.
 
The hustle is real
 
Malipo ya wabunge ni rushwa iliyowekwa indirectly ili kuwalainisha wapitishe ajenda za watawala.
 
Daah andiko gumu hili, hongera na pole kaka.

Kama kawaida yako ukimakiza ukajipongeze na mrembo mkali hahaha mzee wa kitafuna
 
AMINA, Mwenyezi Mungu azidi kuwabariki na kuwapa maarifa zaidi ya kuendelea kufanya kazi yake iliyotukuka, Pia awape hitaji la mioyo yenu.
 
Pole sana mtumishi… wanakuja business owners na kaka yao Mpwanyungu kukwambia nenda kajiajiri…

Wanakuja ndugu zao viongozi wasio wahadilifu kukwambia ukipata upenyo hamisha mikasi na gloves nyumbani.

Mie jobless sina usemi zaidi ya pole.
Haya madongo sasa🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…