Huu uzi naundika mahususi kwa kwasababu ya mdau mmoja ambaye anatupigia sana makelele hapa jukwaani kuhusiana na mwanamke bikira,kwa mtazamo wake anaona mwanamke bikira ndio sababu ya utengamano wa ndoa kitu ambacho si kweli kwa asilimia mia moja
Kwanza ieleweke sio kwamba hatupendi wanawake wajitunze mpaka siku ya ndoa laa! Tunapenda sana na kila mzazi angependa mabinti zake waolewe katika hali hiyo na hii inawezekana kama jamii ikiweka sana mkazo katika elimu ya dini na mila na desturi zikilindwa.
Mfano Lesotho sasa hivi kila mwaka wanafanya sherehe za kuwatunuku vyeti mabinti ambao wako bikira ambao wametimiza miaka 25,wanapimwa na kupewa vyeti rasmi,kwahiyo kumbe haya yakifanywa katika jamii inawezekana kabisa
Sasa tuje upande wa pili wa shilingi,kuoa mwanamke bikra hakukupi asilimia mia moja kwamba huyo mwenza wako atakuwa mwaminifu kwa asilimia mia,na hii ni kutokana na mfumo wa maisha ambao tunao sasa,hii sayansi na tekinolojia imekuja na faida na hasara zake
Vishawishi ni vingi mno huko mitandaoni,mambo ya chumbani sasa hivi yapo mitandaoni kwahiyo watu hupenda kujaribu mambo mapya,kwahiyo hata huyo bikira wako nae hajapona juu ya hili,maana naye anashawishiwa kula muogo wa shamba moja kila siku huchoki ebu jaribu bwana muhogo wa jang'ombe,je hapo hajaliwa?
Huko nyuma sio kwamba mababu zetu pamoja na kuoa mabikira sio kwamba hawaja chapiwa laa! Ila hakukuwa na nyenzo za kuchunguzana na kukamatana haraka kwakuwa mpaka umjue mgoni wako basi ufanye kazi kweli
Istoshe wazee wetu walijua haya mambo yapo lkn walijitahidi kadri ya uwezo wao kuepusha ndoa kuvunjika,wazee wakirudi nyumbani kutoka safari,basi hawaendi makwao moja kwa moja ila watatuma mtoto wa jirani apeleke koti nyumbani ikiwa na ishara kwamba amerudi,hivyo kama hapo kwake kuna sintofaahamu yoyote basi asiikute,naam ndio maana waliishi kwa amani na starehe
Sisi karne hii hizi simu ndio mvunjaji wa kwanza wa ndoa zetu,siku hizi tunafumaniana kupitia meseji,halafu cha ajabu eti meseji ndio inavunja ndoa,hivi tupo serious kweli? Yaan umetumia gharama kubwa kuoa,kumchagua mchumba,kumhudumia halafu siku moja tu inaingia meseji halafu ndoa inakuwa hakuna tena,ni aibu kubwa
Hivi kama tukiacha kuchunguzana katika simu unafikiri ndoa hazitadumu? Kwa maono yangu kuna sababu nyingi sana za watu kuchepuka,ukosefu wa mapenzi,kutopeana mda kumfanya mwenzio kuwa mpweke na hakuna kitu kibaya kama kuwa mpweke katika ndoa,kutokuwepo kwa maelewano na ugomvi kila mara,kutopeana haki ya tendo la ndoa na mambo kadha wa kadha
Kwahiyo tusijidanganye kuchepuka kutakuwepo tu iwe umeoa bikra au sio bikra,na bikra mzuri ni yule ambaye amejitunza mpaka ndoa,kama ulimtoa bikra kabla ya ndoa wala usijisifu kwakuwa sio mcha mungu,ni mcha mungu pekee ndio ana nafasi kubwa ya kutochepuka kwakuwa ana hofu ya Mungu,lakini bikra yake sio dhamana ya uaminifu wake,ingawa kidogo ana uhafadhali
Ukitaka kudumu katika ndoa mheshimiane yaani msitengenezeane mazingira ya kuwa na mashaka,muaminiane hiyo ndio silaha kubwa sana,mkiaminiana hata kuwekeana soft ware za kuchunguzana hamtafanya,ila mkitaka kuachana fasta endekezini kupekuana simu zenu na kuwekeana hizo soft ware zenu nipo pale nawazoom mtaendelea kulialia mpaka kiama
Ni hayo tu!