Ndoa yangu inakwenda kuvunjika naombeni ushauri nifanyeje?

Ndoa yangu inakwenda kuvunjika naombeni ushauri nifanyeje?

Mamlaka ni mtonyo, hivi unaweza kukoroma na huna hata buku mfukoni[emoji1787]???
Huwezi mkuu. Nimemshangaa mno huyo mama. Imagine Putin na mamlaka yake au hayati theodore roosevelt wa Marekani, au Jiwe au JK then awe lofa kweli? Muambie aiweke statement yake vizuri tuielewe. Kajikoroga sana
 
Kwahiyo hoja hapo ni kunyimwa unyumba ndio unataka kumuacha?? Jipe muda jaribu kufikiri mazuri anayokufanyia mbali na hilo baya, zimwi likujualo halikuli ukaisha, miaka 10 kuishi na mwanamke Si mchezo
 
Mna matatizo nyie
Kuamua kuwa na watoto wawili ni matatizo???Hapana hata kwetu tupo wawili na mm ndiyo mkubwa nina miaka 29 anayenifuata anamiaka 20 je baba na mama yangu walikuwa na matatizo???
 
Kuamua kuwa na watoto wawili ni matatizo???Hapana hata kwetu tupo wawili na mm ndiyo mkubwa nina miaka 29 anayenifuata anamiaka 20 je baba na mama yangu walikuwa na matatizo???
Mna matatizo na mtakufa muishe bila kumbukumbu
 
Mna matatizo na mtakufa muishe bila kumbukumbu
Mawazo finyu kufa kupo baba yangu kwao yupo pekee na ana miaka 62 kama sijasahau kwaiyo ww unazaa kijiji kwasababu ya kumbukumbu????
 
Nimeishi na mwanamke miaka 10 tuna mtoto mmoja wakike yupo darsa la 5. Mimi ni fundi ujenzi nafanya kazi za mashirika kama NSSF, ALUMINIUM EMIRRAT naza mitaani ndogo ndogo.

Familia naihudumia kwa kila kitu na mke anafanya kazi siku nikikwama akitoa hata buku yake ni ugomvi. Sasa naona mwezi huu ndiyo mambo yamekuwa kuwa mambo baada ya project nyingi kusimama kwa hiyo kipato changu kimeshuka japo najitahidi kuhudumia familia kwa vyovyote.

Sasa imefika hatua hata unyumba nanyimwa inaniuma kila nikitaka kumwacha nikimwangalia mwanangu machozi yanatoka tu.

Vipi kuhusu kumchukua mwanangu ana miaka 10 wa kike je nikienda kisheria naweza kabidhiwa mwanangu?

MSAADA WA KIMAWAZO WANAJAMII.
Afadhali hata wewe unaomba na kunyimwa, mwenzio hawezi kuomba wala hawezi kuhudumia mke kachoka kumpikia eti nampikia anakula lakini hakuna kitu kesi iko baraza, pole sana.
 
Sasa imefika hatua hata unyumba nanyimwa inaniuma kila nikitaka kumwacha nikimwangalia mwanangu machozi yanatoka tu.
I can feel your pain, tafadhali kaeni chini muongee. Na mwenyezi Mungu awatangulie. Usikubali Hilo kosa la kuvunja ndoa, baadhi ya wanawake ni viumbe wa ajabu sana
 
Mpaka anakunyima unyumba maana yake kuna mwingine anampa unyumba. Amua kusuka au kunyoa
 
Akirudi mke ana mimba ya bahasha mwengine
Hata akikaa hapo 24/7 kama alioa mtu wa watu atagongewa sana tu na atalea mbegu za wengine mpaka ashangae .
Bora ajipe likizo kidogo atarudi na maamuzi sahihi
 
Kwa kamasi hizi zinazokutoka una kipi sasa cha kuvutia mwanamke na wewe hebu usinichekeshe, wanawake huwa hatuhangaiki na mwanaume anaelizwa na mwanamke maana tunajua ni boya flani hivi, fatilia utagundua wanawake tunamkimbilia sana mwanaume anaeliza wanawake sio anaelilia wanawake km wewe
prostitute 😡
 
Nakushauri ukipata nafasi pitia zile clips za 'divorce court' kwenye youtube, ni za Judge Lynn Toler.

Judge huyu ana ushauri mzuri sana kwa wanaotaka kuoana, walio kwenye ndoa na wanaotaka kuachana.
 
Back
Top Bottom