Ndoa zimekuwaje? Kuna Video inatrend leo Mume akimkaba mkewe na kutaka kumuua live barabarani

Missed call 16 sikumaliziana charge tu na umeme huu wa mgao, haya ndio madhara ya kusomea primary vijijini unaamini adabu hufunzwa kwa kupiga, gari yenyewe ist namba c, unapiga demu kweli?
 
Huyo mbaba nae anatia aibu.. mnyanyasaji.. mp*mbavu, mke amuache libaki lenyewe.. akwende zake. *henzwi taipu.. kwani ndoa lazima.. aibu kwake sasa.. hata kazi afukuzwe mnyanyasaji wa wanawake.
Ndo missed calls 16?
 
Kupigana hadharani ni kosa la jinai, kupiga yaani shambulio la kudhuru mwili ni kosa la jinai, kwa ushahidi huu hivi tamwa tgnp uwt bawacha samia legal aid polisi dawati la jinsia wameshindwa kuchukua hatua kweli? Hibi hiki kipigo angekuwa polisi ndo anapigwa huyu mtu si angekuwa segerea tayari, au hadi mtu afe ndo tuone hiyo ni jinai?
 
Hao watu waliokuwa wanarekodi tu na kumbembeleza huyo mwanaume nao ni kama wapumbavu tu. Katika hali ya kawaida huyo mwanaume alipaswa kushambuliwa kwa fimbo na mawe, raia hawakupaswa kucheka na huyo mwanaume, ndoa sio kichaka cha kufichia ukatili.
We nae m*tak0 tu mjuba
Naona unaweka ushuzi tu hapa
 
Nguvu ya kisungura...🤣🤣🤣🤣
Jamaa anatamani amkague mke **** ...
Mamaee
 
Ndoa ni kama dini, watu wameaminishwa hakuna kutengana, hivyo wameuza nafsi zao huko....kufa kupona
Umeona eenhh??!!.Lkn ktk Imani kwa sisi Wakatoliki tunaamini ktk Msemo usemao "Philosophie anchillar Theologica",Kwamba Imani na akili husaidiana,kwa hiyo ktk Mazingira km hayo Kanisa laweza kuruhusu Mke na Mume watengane kwa muda ili kila mmoja kujitafakari na kisha kujirudi.Kuna kitu Kwenye Canon Law kinaitwa "Nullity of Marriage",huyo yamo Mambo 12 yanayoweza Kufanya ndoa isiwe halali,Mojawapo ni hali ya hatari kwa mmojawapo wa Wana ndoa.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Uko la ngapi mkuu? Yaani mtaani ukiona mke na mume wanadundana unaingilia ugomvi, huna shughuli za kukukeep busy?
 
Sahihi kabisa
 
Kwani wamelazimishwa kuendelea kuishi pamoja hao watu?

Mwanamke amepata sababu ya kupigwa nje

Mwanaume yupo hatarini kwa kesi ya mauaji kwa siku zijazo
 
Mimi ndio maana huwa namsisitizia mume wangu mara kwa mara "Mimi sio mali yako, ni mwenza wako" ili iendelee kuingia akilini. We are partners, lovers na hakuna anayemmiliki mwenzie wala baba au mama wa mwenzie. The options you have ukikosewa ni kusamehe au kuondoka na ni haki yako kufanya either of them!
 
Ha ha ha na mume wako huwa anajibu nini ukishamwambia hivyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…