Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Ndoto tunazoota na tafsiri zake

mwanzoni mwa wiki hii nilimuota mwanangu wa nguvu ambae amestangulia miaka minne iliyopita, ktk hiyo ndoto ilikuwa ni kama sherehe flani ambayo mimi nilialikwa tuu, nilipofika pale nilikuta watu wengi nisiowafahamu, ila nilimfahamu jamaa yangu ambae tayari ni marehemu, dah nilistuka, nikamwita kwa jina, jamaa akanipita kama hanifahamu, ila alienda pembeni hivi akaniita kwa ishara, nilipomfikia nikamuuliza G...ni wewe kweli? akanijibu yap ni mimi, jamaa alikuwa smart kavaa suti moja nyeusi iliyomkaa vyema..ikabidi nimuulize kaka we si umekufa? akanijibu mwanangu we acha tu, yah mimi nimekufa ila tuyaache hayo, vipi bi bimkubwa anaendeleaje? akimaanisha mama yangu, nikamwambia hajambo ila man kwanini upo hapa? akasema hapa waliopo karibia wote wameshakufa ila wapo watu watatu ambao mpo hai na hata hawa waliokufa si unawaona wapo hai? ilinibidi nikurupuke tuu, ndoto gani tena za namna hii? sasa kilichokuja nikumbusha hii ndoto ni hiyo siku iliyofuata ikaingia notification ya kuwatakia kheri za kuzaliwa bandugu kule facebook, jina la mwanangu ambaye ndio huyo Marehemu lilikuwa la kwanza....nilijisikia vibaya kwa kwali....siamini ktk ndoto ila...ndo hivyo
Kinachokufa ni mwili tuu ila roho zinaendelea kuishi katika hali nyingine, na hapo huyo mwanao alikuja kukusabahi tuu,, na ukitaka kujua ni hyo iilikuwa halisi ndoto hyo hukuisahau asbuhi na hutokuja kuisahau,, ila zile ndoto za kawaida km za kushiba alizosema mtoa mada huwa mara nyingi ukiamka unakuta umezisahau kwa 90%
 
Binadamu tumeumbwa kwa namna ya pekee sana,, ukizitafakari sana ndoto utagundua mengi sana kwenye ndoto ambapo huwa ni ulimwengu wa roho

Mfano ndani ya dk 5 unaweza kuota mambo ya kufanywa kwa mwezi mzima au mwaka mzima
 
Namba 3.Ndoto hizi ukiota lazima utaikumbuka yote na halafu unajiwa na hali ya kukufanya uitafakari au kuirudia kuikumbuka mara kwa mara,its vey interesting,kikubwa usiidharau aina hii ya ndoto maana huwa ni vitu halisi ninavyoweza kuja kukutokea..
 
sio kweli.
kwa mfano hiyo no. 2, mwanaume huwa anaota anafanya mapenzi na kujimwagia shahawa kutokana na kukaa muda mrefu bila kufanya mapenzi/kuzitoa hivyo inafikia kipindi zinatoka zenyewe.
umesoma kwa pupa.
hapo anaongelewa mawanamke mkuu.
kukutwa na mbegu za kiume wakati alilala peke yake.
hata kwenyw vyombo vya habari hizo habari hasa walimu vijijini hayo mambo hutangazwa.
au tuseme mwanaume ulale peke yako chumbani ukute mbegu za kiume kwenye makalio mkuu.
 
umesoma kwa pupa.
hapo anaongelewa mawanamke mkuu.
kukutwa na mbegu za kiume wakati alilala peke yake.
hata kwenyw vyombo vya habari hizo habari hasa walimu vijijini hayo mambo hutangazwa.
au tuseme mwanaume ulale peke yako chumbani ukute mbegu za kiume kwenye makalio mkuu.
wapi umeandika anazungumziwa mwanamke ?
 
umeacha moja ''hali ya kiroho pale ulipolala''
na hiyo aina ya kwanza nadhani ungesema kutokana na shughuli nyingi
 
nilitegemea kwa sababu ni jukwaa la kufikiri kidogo ungeelewa nilipoandika " Kuota unafanywa mapenzi" ''sio unafanya mapenzi".
asante kwa maoni lakin mkuu.
ubarikiwe.
duuu et unafanya na unafanywa hahahahh kwahy h ndo umeona style ya kujitetea eee
ubarikiwe pia.
 
Dah! Kuna mwaka nilikua na ukame balaha nikaota nimekutana mmojawapo kati ya wale wadada wanaounda kundi la Blue 3, basi si akaniachia number ya simu dah! Kuna mjinga si akaniamsha! Nikastuka nikiwa sijamaliziwa number moja ya mwisho aisee wacha nihangaike kubuni number ili niwasiliane na mtoto😀😀😀😀
 
Miye nikiota huwa nikiamka sikumbuki nilichoota usiku wa kuamkia leo! Je hilo nalo ni tatizo...
Ila nikinuiya kumwomba Allah anilinde usiku na anikumbushe ndoto nitakayoota huwa naikumbuka na nisipofanya hivyo sikumbuki.
Je hali hii inaashiria kitu gani?
 
1: Ndoto Unazozipata kwa Sababu ya Kushiba, Maneno mengi uliyoongea au kumbukumbu ya mambo yaliyopita.
Ndoto hizi ni asili, Kila mwanadamu anaziota. Mtu akikwambia huwa haoti ujue ni Muongo.

Mwenye Hekima Suleiman Anaandika
" Kadiri mtu anavyohangaika zaidi, ndivyo atakavyoota ndoto;
sauti ya mpumbavu ni maneno mengi." Muhubiri 5:3
Hapa hakuna uhusiano na mapepo, majini wala mashetani.

2:Ndoto Zinazoletwa na Mashetani.
Hii inaushahidi wa kiuzoefu tu. Leo utakuwa umesikia mtu kalala, kaota anafanywa mapenzi na anapoamka asubuhi anakuta amemwagiwa hadi mbegu za kiume huku alikuwa peke yake kitandani.
Wapo wanaooteshwa na kuamka usiku kwenda kulima,kufanya kazi na wanaamka wamechoka, ikifika asubuhi anaweza kukumbuka kama alikuwa anaota anafanya kazi kumbe kazi ilikuwa halisi.

Wapo wanaoamshwa kichawi, wanafanyishwa matukio ya ajabu akiwa katika hali ya ndoto.
(Hapa wenye ukina zaid wanaweza kufafanua ila ni vitu halisi havihitaji kuamini Mungu/Shetani Yupo au hayupo)
cc Bilionea Asigwa Mshana Jr

Kwa watu wanaomuamini Yesu, Hutokaa ukutwe na mambo haya labda kama unaamini katika viwango vya unafiki au unachanganya dini na uchawi/ulozi.

3:Ndoto Zinazoletwa na Mungu.
Hizi Mungu mwenyewe anasema "Akiwepo nabii kati yenu, Nitasema naye kwa njia ya NDOTO" Hesabu 12:6
Lakini Sio tu nabii, hata watu wa kawaida, hata wasio watu wa Kitabu, hata viongozi.
Alisema kwa njia ya ndoto na Farao, Nebuchadneza, Yule mfungwa gerezani pamoja na Yesufu.

SIFA ZA NDOTO HIZI
1: Ziko wazi, hazina kona kona au kubahatishabahatisha.
2:Lazima zitimie.
3:Hazikutegemei wewe kuifanya itimiie.
4:Huwa haziji mara kwa mara.

MWIISHO
Nimeandika haya ili kusaidia watu ambao wanaota nndoto za kawaida tu, ambazo ukikaa mwenyewe ukafikiri kwa nini umeota hilo utagundua tukio lililopita au mazungumzo yaliyopita ndio chanzo cha ndoto lakini wameibuka watu ambao wao wanaamini kila ndoto ni matokeo ya majini. Kila ndoto lazima iwe na tafsiri, Kila ndoto ni ya Mungu au Ya shetani.

Wajuvi zaidi wa mambo haya wanaweza kuja kushuka nondo zaidi.
Asante sana kwa mwaliko nilikuwa offline ngoja nitulie nitarejea
 
Mm huwa sioti trust me huwa sioti
ukiona huoti ndoto yeyote ile basi punguza au acha kabisa kutumia pombe kali,bangi,au cocain utaona maajab. Kwa maana kila mwanadam anakawaida ya kuota ndoto kila siku ingawa kuna ndoto zingine huwa hatuzikumbuki kukicha.
 
Umofia kwenu wakuu,

Wapo watu ambao wanapenda kujua maana au tafsiri za ndoto kwa kuwa nyingi huwa zinakuja kwa mtindo wa mafumbo. Wapo wanaoamini kuwa ndoto zina taarifa zenye miongozo au kutoa tahadhari kwenye mwenendo wa maisha yao ya kila siku. Hivyo kuzielewa kuna maana kubwa sana kwao.

Nimeona ni jambo jema kukusanya mada ambazo zimeshawahi kujadiliwa kwa kina humu JF kuhusiana na Ndoto na Tafsiri zake, ili kuweka urahisi kwa wale ambao wanataka kujua tafsiri ya ndoto zao walizoota, pasi na kuwa na haja ya kuanzisha uzi mpya kuulizia kitu cha aina moja kila uchwao..

Zifuatazo ni mada zenye maswali na majibu kuhusu ndoto mbalimbali ambazo zimeshawahi kujadiliwa humu JF;

Hizi ni ndoto hatari sana maishani mwako..

Ndoto za kupaa na kuelea hewani zinaashiria nini?

Jinamizi ni nini? Kwanini hutokea wakati wa kulala tu?


Msaada: Nimeota nimeenda eneo nisilolijua na kukutana na vitisho


Ndoto za Mapenzi zinanitesa, nifanyeje?

Kuna mahusiano kati ya ndoto na maisha ya kawaida?

Naomba tafsiri ya hii ndoto: Nimeota nimekufa na kuwekwa ndani ya jeneza


Naomba mnitafsirie hii ndoto
========

NB
: Kama kuna uzi ambao ushawahi kujadiliwa kwa kina kuhusu ndoto na haupo kwenye hiyo orodha hapo juu, tafadhali tukumbushane ili niuongeze hapa.

Wasalaam..
Ukiota kaka yako anayembea na mwanamke wako ina maana gani
 
Back
Top Bottom