Bueno
JF-Expert Member
- Sep 9, 2022
- 4,114
- 6,449
Wazee wameshika Bango wanawaambia Vijana wawe wabunifu halafu wao wapo tu huko wanaenda kushindwa negotiation za ajabu ajabu wamekomaa Vijana wawe wabunifu wasisubiri ajira za Serikali Ajira Portal PSRS Utumishi bali Vijana wajiajiri wakati huo Wazee wanatembelea LC 300 zilizotokana na Pesa za hao hao VijanaKatika moja ya comment zilizowahi kunishtua ni hii ya jobu aliyoitoa akiwa spika.
Alidai kwamba wenzetu baadhi ya mataifa linapohusika suala la mikataba, hawana masihara hata kidogo huchukua vijana smart class A wenye uwezo mkubwa wa kusoma kuelewa na kufikiri kwa upana juu ya mikataba tunayoingia kama taifa ni kwa namna gani itanufaisha umma. Akasema kwetu Tanzania hali ni tofauti kabisa kwani sisi huwatumia maprof wetu.
Ni kweli wana elimu nzuri lakini wamechoka kiakili kwa namna ambayo ni rahisi sana kutuingiza chaka. Alisema hii mikataba inaandikwa kijanja sana na ni mabook makubwa makubwa hiyo yanahitaji akili fresh ili kuyasoma kuyaelewa na kufanya maamuzi sahihi.
Mada ya mikataba ya nchi ni nzito sana haikupaswa kabisa kufanyika kizembe.