Ndugai: Toka Magufuli aage Dunia, umuhimu wa Dodoma unafifishwa kwa makusudi kabisa

Ndugai: Toka Magufuli aage Dunia, umuhimu wa Dodoma unafifishwa kwa makusudi kabisa

"....wakati fulani Dodoma ilikuwa mchaka mchaka wa hakika kuelekea kuwa Mji mkuu wa Serikali ki vitendo na hata ulipokuwa unawaangalia Viongozi wakuu wa Serikali ulikuwa unaona nyuso za haja za kulimaliza hilo mapema kabisa."

"...sasa hivi kila warsha na kongamano ni Dar!"

"...hii siyo sawasawa kabisa Dodoma ni Mji na makao makuu ya Nchi ki sheria na hata hao wanaofanya kampeni za kufifisha safari hiyo wanapoteza muda wao bure tu."

"...ndugu zangu wapende ama wasipende Dodoma ni lazima wataishi kwa sababu Bunge lilishatunga sheria na kamwe haiwezi kubadirika."

Amesema Ndugai.

Baada ya kumdhihaki marehemuna kugundua baadae .....
 
Eti "sheria ya Dom mji mkuu kamwe haiwezi kubadilika", hii ni kweli ndugu zangu ?
Hatumii akili,ikiwa iliwezekana kubadili sheria za vyama na katiba kuhusu sifa na vigezo vya mtu kuwa mbunge.
Akazane kama alivyoahidi kuwalinda kwa nguvu zote wanawake.Mbona sasa anamsema kwa kumzunguka.Tuendako tuwe na Spika nje ya wabunge.
 
Hata kusini ilififishwa na Magu akaelekea kanda ya ziwa na Ndugai alikaa kimyaaaaa.Amuache mama yetu afanye kazi.
 
Kwa akili za Ndugai,warsha na seminar na makongamano yakifanyika yote Dom ndio inakuwa Mji mkuu?

Una akili kweli wewe Ndugai? Kwamba kwenye miji yote mikuu Duniani ila warsha na makongamano yanafanyika kwenye capital cities?
Yafanyike pia huko Katavi , kwa nini Dar tu? Huko kwingine sio Tanzania kwani?
 
"...ndugu zangu wapende ama wasipende Dodoma ni lazima wataishi kwa sababu Bunge lilishatunga sheria na kamwe haiwezi kubadirika."
Huyu mzee; ati sheria ya Bunge haiwezi kufutwa ama kubadilishwa ?
 
Sheria kitu gani bwana! Dodoma ni Kijiji hapafai na hapana hadhi ya kuwa jiji.


Loo! Salale! Kama supika (siyo spika) analalamikia serikali huyo machinga asemeje?
Issue kuwa Jiji au kuwa makao makuu?
 
Kwani Chifu Hangaya mwenyewe anasemaje?
 
Simuongelei prof mkuu! Huu mkataba magu aliuusoma kidogo mashariti yake na nafikiri ukitafuta iyo clip ipo mkuu kwa uchache ule unatosha kuuwona huu mradi miyeyusho
Yule jamaa alikua fix sana, tumia clip hiyo Kisha tafuta clip ya marehemu Kinjeketile akiwa hospital jamaa alivyo mnukuu uwongo mtupu wakati tulimsikia. Eti Ccm ni chama changu. Sasa ndiyo uje umuamini ktk mkataba aliousoma yeye.
 
"....wakati fulani Dodoma ilikuwa mchaka mchaka wa hakika kuelekea kuwa Mji mkuu wa Serikali ki vitendo na hata ulipokuwa unawaangalia Viongozi wakuu wa Serikali ulikuwa unaona nyuso za haja za kulimaliza hilo mapema kabisa."

"...sasa hivi kila warsha na kongamano ni Dar!"

"...hii siyo sawasawa kabisa Dodoma ni Mji na makao makuu ya Nchi ki sheria na hata hao wanaofanya kampeni za kufifisha safari hiyo wanapoteza muda wao bure tu."

"...ndugu zangu wapende ama wasipende Dodoma ni lazima wataishi kwa sababu Bunge lilishatunga sheria na kamwe haiwezi kubadirika."

Amesema Ndugai.
Aache upuuzi na akae kimya kabisa.. Kuna gharama kubwa isiyo na sababu kwa kwenda kufanyia kila kitu Dodoma.. Hiyo pesa anayeukia ni mwananchi wa kawaida
 
Ila ukweli nchi tayari imewekeza fedha nyingi kwa huu mradi wa kuhamia Dodoma. Kama wafanyakazi wa serikali tayari wanaishi na kufanya kazi huko, kwa nini zoezi liendelee kusuasua!? Kama hili suala limepoteza maana itamkwe wazi wazi kuliko huu ujinga unaoendelea.
 
Ndugai mwisho wa kukalia hicho kiti ni 2025 kwahiyo anza kupasha
 
Ndugai yuko sawa kabisa yaani hawa watu wanaturudisha nyuma kuliko toka!
Hata kama yuko sawa si waambizane kwenye vikao vyao vya chama na serikali?!
Kuwalalamikia wananchi haisaidii cho chote..!
 
Back
Top Bottom