Ndugu yangu alishinda betting milioni 7 na laki 4 mwezi wa kwanza, kwa sasa anatia huruma, hii michezo ina maendeleo kweli?

Kimburu wewe! Unakuja na I.D nyingine kujitetea
 
Wale wa Russia wa 1x bet ukiwala sana mikeka mitano mfululizo account inafungwa 😂😂

Ila kwakweli bado sijaona kampuni yenye market nzuri kama hao jamaa sema possibility ya utapeli ni kubwa
 
Issue nzima ni mentality mkuu pengine hakuwahi kushika kiasi icho. Kwa imani zangu m2 tu ina weza change life lako ukituliza ndonga ukafwata mikakati yako ulio jiwekea una wini
 
Kwani zile unazo pigwa mzee? mchezo ni pata potea ufanyie la maana ama ule bata wewe tu.
 
Huyo hata angeokota hiyo pesa still angeitumia vibaya. Self discpline ni tatizo. Na hili tatizo lipo hata kwa baadhi ya wachimbaji wa madini. Anateseka anapata mamilioni ndani ya miezi sita anarudi shimoni hana pesa.
 
Uwongo huu
Utalipwaje mirathi bila kua na account bank?
 
Watoto hawajui haya mambo.
Mchana Boda usiku mbeba mawe.
Wakati wewe unalala kuna wanaume na wanaweke usiku wanafanya kazi za hatari sana za kutumia akili pasipo kumwaga damu ya mtu.

Daima huwezi fanana na mtu aliyelala masaa mawili usiku akiwa anahangaika na mishe za akili.

Haya mambo yapo na tunaishi na hao watu..sisi tunahesabu siku..wao wanahesabu pesa.

Mfano mwaka huu wa Uchaguzi na Mwakani..kuna wana tayari wameshaansa vile vipeperushi vya vyama vyetu pendwa vya siasa na Mama Kizimkazi.

Mwanaume gani hajawahi fanya kazi ya risks na za office na bado unaibiwa.
Unaandika Projects au kutoa mawazo makubwa,watu wanapata hela za kufa mtu wewe unaambuliwa kupewa Mshahara wa 750,000 tena unakatwa na NSSF,PAYE..hizo ndizo kamari za maisha.
 
Hoja ya dhambi ya kamari ni dhaifu mno...halafu kuhusu pesa kwisha inatokana na akili za mtu
 
hakuna haramu wala halali katika utafutaji!
tofauti ni kwamba kuna uharamu uliokubalika na ambao haukukubalika.
Mwanza kuna jamaa aliuza bajaji yake mil 5. akawa anabeti stake ya mil 1 kila siku anapata laki 1.
miaka 5 hajapotezaga
 
Uwongo huu
Utalipwaje mirathi bila kua na account bank?
Uwe unasoma vitu kwa kuelewa.Kwa taarifa yako tu huwezi kunidanganya kitu chochote kinachohusiana na mirathi na sheria zake.Nakufafanulia sasa dogo alikuwa na account ila ATM hana .Unajua bank huwa zinafungwa sa ngapi?Ukiwa huna ATM wala sim banking hela utaitoaje?.
 
Kupata PESA inaweza kuwa kazi Sana Ila kuimiliki PESA ndo huwa inahitaji kuwa na open mind set kutokuwa na tamaa ya kutumia Sana plus mikakati.

Wengi hatuna huwezo wa kumiliki PESA that is way we live paycheck to paycheck life and hand to mouth life


Tatizo hapo sio hela ya kamali Ila hapo tatizo ni mind set ya MTU
 

Mtafute huyu mwamba ndio utajua inalipa au hailipi,SKOMOTA (Ngwana Sesi)...​

 
mtafute huyu mwamba Google ndio utajua inalipa au hailipi,Skomota(Ngwana Sesi)...
 
Pole kwake, na dogo2 vipi?
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Eventually the House Always Wins...; Odds Favor them
 
Na mimi nilitaka kusema hivo.
JF inaruhusu kutumia Kiingereza ila jamaa ana broken English mpaka msomaji unakasirika huyu mtu alikusudia kusema nini.
Mnamuonea tu,kwa wahaya Ni kawaida yao tu.Hakafu huyo ni chalii mdogo wa miaka 26 tu so bado ana theories nyingi kichwani,bado hajapajua field pakoje
 
Motivational speakers bana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…