zwangandaba
JF-Expert Member
- Jan 31, 2023
- 747
- 1,404
Kumbe wanasheria kazi yao ni kutakatisha mali za wizi ekhMambo ya kununua kwa unaemwamini kwa kauli mali pekee haitoshi kwa ulomwengu wa sasa, kesho mwaweza kupishana kauli akakuchoma ama nae aliinunua ya wizi likakukuta wewe.
Kama ilivyo kwa gari, kwenye simu pia hakikisha hata ukinunua kwa rafiki yako kuwe na mkataba ulioandaliwa na attorneys waliojaa kama utitiri mjini, ni heri umpe attorney elf 50 kwajili ya mkataba kuliko kukamatwa na huna nyaraka yoyotr ya usbahidi.
Wewe unanunuaje simu mkononi pasipo na uthibitisho anayekuuzia ndiye mmiliki halali?
Simu yoyote iliyonunuliwa kihalali ina vithibitisho vikiwemo risiti halali na mkataba wa mauziano.
Kama hivyo hakuna basi endelea kununua simu kiholela ukisubiri somo la hekima.
Hiyo huwaga ni michozi ya polisi na hao matapeliPole sana kwake, nina rafiki alitoa hela nyingi kununua Samsung akashangaa baada ya miezi miwili anapigiwa simu na Askari wa Oysterbay kuwa simu ni ya wizi
Alichukulia masihara labda matapeli mpaka siku alivyoona kero ya kupigiwa imezidi na kuamua kwenda Polisi, akakuta kweli na simu kwa mujibu wao, ni ya mdogo wa kiongozi mkubwa sana nchini
Ilibidi aitoe bila masharti ya ziada maana walimtaiti kwa maelezo tu akaona hana pa kutokea na aliinunua kwa raia aliyeipost kwenye mtandao
Tuweni makini sana na simu hasa hizi Samsung either nunua dukani ama hakikisha anakupa risiti halali, vinginevyo nunua kwa unaemuamini