Ndugu yangu na wengine sita wakamatwa usiku wa manane wakihisiwa kujifunza ugaidi na hatujui waliko hadi sasa

Ndugu yangu na wengine sita wakamatwa usiku wa manane wakihisiwa kujifunza ugaidi na hatujui waliko hadi sasa

Habari ndugu wana jf jamani hii nchi kamatakamata haijaisha...nina brother wangu ambae ni first born wetu aged 31 years amekamatwa yapata wiki mbili sasa usiku wa manane na watu tunaowahisi ni usalama wa taifa walienda wakavunja komeo la mlango wake wakaingia ndani walikuwa na bunduki wakamkamata pasi nakutoa maelezo maalum wakabeba na simu zake hatujuh aliko had leo hii mama yake mzazi analia kuchwa kutwa hajuh kam mwanae ni mzima ama amekufa kwa kwel hali ya usalama nchini si shwar na hatukuwah kumuona ama kumuhisi ana vitendo hivyo isipokuwa tu ni muislamu dhehebu la sunni na shughuli yake kuu tunaijua kwa hiyo ombi langu kwa mamlaka hatukatazi kuwakamata na kuwahoji ila ni vizuri mukawafahamisha ndugu wa karibu ili waelewe wapendwa wao wamepelekwa wap... pia ndugu wanajf naomb muendelee kupaza sauri kutokan na vitendo hivi vya usalam wa taifa
Hili tukio limetokea nchi gani? Kama ni Tanzania mkoa au mji gani?
 
Nakushauri iteni Ayo Tv tu huku upo nusu nusu sana Mkuu.

Ila huu utaratibu uliotumika umekaa kushoto sana.
 
Kama ni vyombo vya ndivyo vimemkamata na hahusiki na vitendo hivyo yupo mikono salama,hao Huwa na info za kutosha kabla ya kukamata mtu wiki mbili ni nyingi sana kwa asiyehusika au kuwa na shaka.
Moyo wa mtu msitu umjuavyo sivyo.
Muombee dua tu kama hausiki atarejea.
Daah its so sad ishu ikoje kile kipindi cha sakata la kibiti walikamatwa akiwepo na yeye ila wakarudishwa baada ya kuona hawakuw na hatia ila huyo imamu ambae alikuwa anawapa mawaidha yanayohusiana na jihadi nasikia aliuliwa huko huko na tangu kipindi hicho ratba yake masaa 24 tunaijua asubuh mpak saa 12 yupo kazin kwake alafu jion anarud nyumban analala na mkewe anathibitisha hajawahi kutoka usiku hata siku moja labda akahisi kuna shughuli nyingine anaifanya kwa siri
 
Habari ndugu wana JF,

Jamani hii nchi kamatakamata haijaisha. Nina kaka yangu ambae ni wakwanza kuzaliwa, miaka 31 amekamatwa usiku wa manane yapata wiki mbili sasa na watu tunaowahisi ni Usalama wa Taifa.

Walienda wakavunja komeo la mlango wake wakaingia ndani. Walikuwa na bunduki, wakamkamata pasi na kutoa maelezo maalum. Wakabeba na simu zake hatujui aliko had leo hii. Mama yake mzazi analia kuchwa kutwa hajui kama mwanae ni mzima ama amekufa.

Kwakweli hali ya usalama nchini si shwari, na hatukuwahi kumuona ama kumuhisi ana vitendo hivyo isipokuwa tu ni muislamu dhehebu la sunni na shughuli yake kuu tunaijua.

Kwahiyo ombi langu kwa mamlaka; hatukatazi kuwakamata na kuwahoji, ila ni vizuri mkawafahamisha ndugu wa karibu ili waelewe wapendwa wao wamepelekwa wap. Pia ndugu Wanajf naomba muendelee kupaza sauti kutokana na vitendo hivi vya usalam wa taifa.
Ungejitambulisha kwanza ili wajue wewe ni nani? Unaishi wapi? Hii itasaidia kukujua na kukuletea msaada.
 
Ukanda wa kusini bado si salama hasa maeneo ya mpaka na msumbiji kingine inawezekana yeye si gaidi ila marafiki zake au alikkuwa anafanya na biashara na wanaoshukiwa bila yeye kujua shughuli zao poleni
Okay.

V I jana wa akiiskam wasidanganyike kwa tamaa ya pesa.

Uislam haufundishi ugaidi.

Mkiona mtu hata msikitini anajidai kufanya urafiki abawarubuni kwa pesa mumtolee ripoti polisi haraka sana.
 
kama kachukuliwa na TISS basi kuna kitu nyuma yake. TISS hawawezi kukurupuka tu, labda kuwe na msukumo wa kisiasa.na kwa maelezo yako inaonyesha ndg yako hakuwahi kujihusisha na harakati za kisiasa.

chunguza vizuri mienendo yake, ukute anauhusiano na kile kikundi cha kigaidi kinacho terrorise eneo la cabo delgado, msumbiji.
 
Back
Top Bottom