Ndugu yangu wa Kiume anaoga baada ya siku mbili, maji yapo ya kutosha. Hii ni kawaida?

Dah...kikawaida binadamu kamili haogi bila ya kuwa na sababu...hivyo hata wiki 2 mbona poa tu [emoji2960]
 
Kila mtu na lake wengine wanaitwa "maji kwake ni sumu, sabuni kwake ni bomu" kifupi "maji sumu sabuni bomu"
 
Kumbe humu wengi hamuogiiii?? Ajabu ya Mussa Kuoga Ni kila siku siyo Sheria but kiafya.Imagine unaenda chooni kila siku usipojikosha ka siku jua unatembea na vimelea vya kinyesi.
 
Alishawahi labda huko nyuma kukuambia kuwa angependa sana Ukubwani mwake aje kuwa Mganga wa Kienyeji wa Kutukuka?
 
Kwahiyo bro,Ndo umeamua kunianika humu 'jeifu'?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilisoma vibaya nikajua anaoga mara mbili kwa siku. Hahahhaa.

Man, mi nimekaa sana Iringa. hahhaha dah mtu wa Dar ukimuambia kwamba nilikua navusha week 2 anaweza asiamini.
 
Umeanza maneno maneno na ndugu yako, mwisho utafukuza kisa kuoga baada ya siku mbili.
 
Huyo ndugu yako sio ndimbo kweli??????
Maana hio tabia alikua nayo toka kygo boi kuoga mala mbili tu.Kwa term nzima
 
Wengine hata mwezi tunagonga sembuse huyo siku mbili maadam sijaaribu shughuli yoyote ya mtu nina amani kabisa.
 
Nyie ni wachagga?
 
Mangi kweli ngozi ya mwingine inakuwasha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…