Neno "DEAR" linatumika vibaya au ni Ushamba wangu

Neno "DEAR" linatumika vibaya au ni Ushamba wangu

Kwa nilichokiona processor yako iko slow sana
 
Nani alikudanganya dear ni kati wapenzi tu? Ushamba mwengine! Barua zangu zote nilipofika form two na kutaka kuwaonyesha ndugu zangu kuwa nimeanza kujua kiingereza nilikuwa naanza na ''Dear sister, Dear Father, Dear Brother.....
Kwenye upande wa barua ipo hivyo. Formal letter lazima ianze na dear.
Ila kibongobongo kwenye maongezi ya kawaida inaleta ukakasi.

Kwahiyo wewe mshkaji wako wa kiume akikuita dear utaona sawa? Kama ni sawa tufunge huu uzi kabisa
 
Kweli hii lugha ilikuja na Meli
Sa hapo mbona hakuna tatizo kabisa
 
Dear Ina maanisha mpendwa...

Mpendwa mteja hauna Salio la kutosha kukamilisha muamala huu

Dear customer you don't have enough balance to complete this transaction...


Cc: Mahondaw
 
Wewe ndiyo una tatizo.
Umezeeka kama mimi na English yetu ya shule za Nyerere.
Nadhani darling, My love na honey zina maana tofauti na dear ingawa dear inawahusu wote hao wengine.
 
Dear friend, dear father, dear mother, dear brothers and sisters, dear colleagues, ...
 
Kwa miaka ya hivi karibuni matumizi ya neno dear yameongezeka sana, zamani ukimuita mtu dear maana yake kuna mapenzi kati yenu
Siku hizi dear linatumika kwa mtu yoyote yule hasa sisi wadada tunaitana sana hivyo.
Cha kushangaza sasa...Unaweza ukawa unawasiliana na mtu/mdada ambae hamfahamiani hata sura, inaweza ikawa kibiashara au kwa sababu nyingine, anakwambia okay dear, yaani dear dear za kutosha. Hili huwa linanishangaza yaani iweje huyu mtu hanijui kuniita dear amewaza nini. Sipendi hii tabia.

Sasa leo mimi nimefiwa na mjomba wangu jamani kwanza nipeni pole maana nina majonzi ya kutosha. Huyu mjomba tumeishi nae kipindi nipo mdogo, so ni mjomba wangu wa karibu sana. Rambi rambi napokea.

Nikapost whatsapp status rest in peace my uncle..kuna dogo mmoja ambaye ni fundi seremala huwa namtumia kunitengenezea baadhi ya kazi zangu akarespond ile status akasema "pole dear". Nimejibu asante lakini nimejiuliza sana huyu dogo vipi kuniita dear wakati hatuna hata mazoea nae zaidi ya kazi mara moja moja kuniita mimi dear. Sijapenda naona kama ni ukosefu wa adabu.

Je nyie wenzangu neno dear mnalitumia kwa watu aina gani? Mimi nalitumia kwa mpenzi na kwa mashosti zangu wa karibu kabisa.
Yani mimi mtu nisiyempenda akiniita hivo nachukia sana
 
Back
Top Bottom