Ngoma Inogile: Wapangaji sasa kulipa asilimia 10 ya kodi TRA

#TANZANIA:
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesisitiza wapangaji katika nyumba za kupanga kuwa wazalendo na kulipia asilimia 10 ya kodi wanazokuwa wakilipa kwa wenyenyumba ili kulipia kodi ya pango.

Source-MwanzoTv
 
Hahahahah hio TAX mi nikilala nazalisha nini hapo nyumbani? Nawasubiria kwa hamu na nimejiandaa kulala mahabusu safari hii!
Naomba kujua ile buku ya kila mwezi inayokatwa kupitia luku ni kodi ya nini?
 
Mwenye nyumba ndio alipe sio mpangaji! Hizo sheria kandamizi wanazojitungia tungia tu zitawafikisha mahali fulani maana hazitekelezeki
Basically analipa mwenye nyumba kwa mawazo ya Mwigulu na genge lake. TRA inawaomba wapangaji “wawe wazalendo” na waikate 10% juu kwa juu na kumpa mwenye nyumba 90% ya kodi ya pango ili hiyo 10% mpangaji asaidie kuipeleka TRA

Nani ana muda huo? Wenye nyumba hawatokubali na hakuna mpangaji mwenye moyo huo
 
#TANZANIA:
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesisitiza wapangaji katika nyumba za kupanga kuwa wazalendo na kulipia asilimia 10 ya kodi wanazokuwa wakilipa kwa wenyenyumba ili kulipia kodi ya pango.

Source-MwanzoTv
Kumekucha
 
Mwenye nyumba ndio mwenye jukumu la kulipa maana hapo kwenye kiasi cha Kodi unachomlipa mwenye nyumba inakatwa 10% na Kwa msingi huo lazima kuwe na makubaliano ya kwenye Mkataba wa upangishaji..
 
Do you copy, do you copy over.
255 men down men down over.
Roder that.
 
Hapo zitaanza habari za kutishiana matofali baina ya mpangaji na mwenye nyumba. Tunaoishi kwenye nyumba za urithi kazi ipo.
 
TRA imewashindwa wenye nyumba sasa inataka wapangaji wagombane na wenye nyumba. Kweli kwa maisha yetu ya kibongo umwachie mpangaji akate 10% si unataka umfakaranishe na mwenye nyumba na aishie kufukuzwa? Sijui tunaelekea wapi!
 
Waweke na tozo ya uhai kabisa na iwe ni 10,000 kila mtu aamkapo salama alipe ili akili ziwakae sawa
 
Eti mpangaji atoke nyumbani, alipie usafiri hadi TRA, aunge foleni kulipa withholding tax. Hizo gharama zake atalipwa na Nani,?!

Kama ni uzalendo na wao waache kutumia Ma-vieit mjini wapande Harrier!
Na huyo mpangaji akifanya hivyo and then akamletea mwenyenyumba kodi ambayo imepungua 10% atambiwa hi kodi yako ikiisha nataka chumba changu

Hata hao wenye Nyumba zenye fremu za biashara hi kodi hawalipi badala yake analipa mpangaji kwa kulazimishwa na TRA na mpangaji analipa hiyo 10% ya pango ili kukubali yaishe na sio kama TRA hawalijui hili wanajua vizuri sana kama hi kodi inalipwa na mpangaji na si Mwenye Nyumba



Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Waiweke tena kwenye LUKU ili kuepusha kukimbizana kimbizana barabarani
 
Nashauri hizi sheria zingeanza na elimu ya mlipa kodi kama ilivyo fanyiwa sensa ila viongozi wanakaa na kuamka tu kodi ya mpangaji si vizuri sana
 
Unakuta mpangaji kakaa na zuio miezi sita hajapeleka kisha mwezi wa saba anahama na kodi ya nyumba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…