Ngorongoro - Loliondo: Askari Polisi amekufa baada ya kupigwa Mshale mmoja tu, RC Mongella amlilia

Ngorongoro - Loliondo: Askari Polisi amekufa baada ya kupigwa Mshale mmoja tu, RC Mongella amlilia

Askari Polisi mmoja ameuawa kwa kupigwa mshale wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati wa zoezi la uwekaji mpaka katika eneo la pori tengefu kwenye Tarafa ya Loliondo.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella akisema kwamba kifo hicho kilitokea Juni 10 alasiri, na kusisitiza kwamba kama serikali wanatambua uzalendo wa askari huyo.

Ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi wa Tarafa ya Loliondo wilaya ya Ngorongoro kuwa watulivu na kusikiliza maelekezo ya serikali katika zoezi la uwekaji mipaka.

Wananchi wanatakiwa na Serikali kuhama katika eneo la Ngorongoro na kwenda kuishi Handeni, Tanga ambapo Serikali itawasaidia katika kuhama. Nia ikiwa ni kuhakikisha uhifadhi endelevu katika Hifadhi ya Ngorongoro.

Baadhi ya Wananchi wa Ngorongoro hawataki kuhama katika ardhi yao ya asili kwani Wanaishi hapo kisheria na Wanatambulika.
View attachment 2257198
Poa tu ajali kazini Ala wawache washkaji zetu
 
Aridhi yote Tanzania ni mali ya serikali inauwezo wa kuipangia matumizi yoyote kwa mda wowote, labda mbadili katiba iondowe hicho kipengere
Basi waende wakakaushe maji kwenye mito ili iendelee kubaki ardhi kama kawaida
 
Askari Polisi mmoja ameuawa kwa kupigwa mshale wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati wa zoezi la uwekaji mpaka katika eneo la pori tengefu kwenye Tarafa ya Loliondo.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella akisema kwamba kifo hicho kilitokea Juni 10 alasiri, na kusisitiza kwamba kama serikali wanatambua uzalendo wa askari huyo.

Ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi wa Tarafa ya Loliondo wilaya ya Ngorongoro kuwa watulivu na kusikiliza maelekezo ya serikali katika zoezi la uwekaji mipaka.

Wananchi wanatakiwa na Serikali kuhama katika eneo la Ngorongoro na kwenda kuishi Handeni, Tanga ambapo Serikali itawasaidia katika kuhama. Nia ikiwa ni kuhakikisha uhifadhi endelevu katika Hifadhi ya Ngorongoro.

Baadhi ya Wananchi wa Ngorongoro hawataki kuhama katika ardhi yao ya asili kwani Wanaishi hapo kisheria na Wanatambulika.
View attachment 2257198
Askari ameuawa halafu unasema hali ni shwari
 
Lakini wote na malikia hangaya nae aliongopa enzi zile
Samia alipoongopa kifo cha Magufuli akiwa Tanga hakuongea maneno ya shombo ya Majaliwa. Mnataka Rais aje mumuone Magomeni? Kamateni wanaosema Rais mgonjwa! Nyinyi ni maadui wa nchi.

Samia never said any of that diisparaging rubbish.

Majaliwa anongopa na kukazia kwa maneno ya shombo. Hajui cha kutamka kukiwa na crisis au watu wakiihoji serikali. He has no public relations savvy.
 
Aridhi yote Tanzania ni mali ya serikali inauwezo wa kuipangia matumizi yoyote kwa mda wowote, labda mbadili katiba iondowe hicho kipengere

Sio Mali ya serikali Bali inasimamiwa na serikali. Na serikali ikitaka kubadilika maamuzi lazima itoe sababu maalum kwa Nini?.
 
Wewe ndio upo nyuma yao. Kuhama kule ni hiari halafu mnatumia risasi kuhamisha watu. Huo sio uungwana.
Kaulize mgodi wa bulyanhulu watu walihamishwa vipi..pakiwa na maslahi ya nchi utahama tu,hao walihamishwa kistaarab tu,Sasa hv wanaleta ununda..utakutana na dola
 
kaphone si anatuaminisha ujinga kama alivotuambianMagufuli anatusalimia sana ?

acha wawanyooshe kima nyie
 
Ngorongoro na Loliondo!!!! mbona vinachanganya
Wananchi wapi wanatakiwa kwenda Handeni?
Ni wanachi wa tarafa ya Ngorongoro, Loliondo au wote?
Wilaya ya Ngorongoro ina tarafa 3 Loliondo,Ngorongoro na Sale tarafa ya Ngorongoro ndiko kunapatikana kreta ya Ngorongoro na pia ndiyo ilipo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro jina hili ndiyo jina la wilaya lakini makao makuu ya wilaya yapo Loliondo mbali sana kutoka Hifadhi ya Ngorongoro Wamasai wanaohamishwa ni wale wanaoishi kwenye eneo la Hifadhi ya Ngorongoro iliyopo tarafa ya Ngorongoro Taarifa ya askari kupigwa mshale kama ni kweli basi tukio hilo litakuwa limetendwa nje ya Tarafa ya Ngorongoro na zaidi ya hapo Wamasai hawatumii sana mishale kabila wanaotumia sana mishale tena kwa weredi mkubwa ni kabila la Wasonjo wanaoishi tarafa za Loliondo na Sale
 
Kwani kati ya Wamasai (wenyeji wa hilo eneo), wanyama na Waarab! Nani wenye haki ya kuishi hilo eneo?
kuwa mwenyeji haimaanishi ni kwako, ardhi yote ni mali ya serikali na inaweza kubadilishwa matumizi mda wwte, kuna watu wanawapa viburi wamasai halafu wao wako nyuma ya keyboard
 
kuwa mwenyeji haimaanishi ni kwako, ardhi yote ni mali ya serikali na inaweza kubadilishwa matumizi mda wwte, kuna watu wanawapa viburi wamasai halafu wao wako nyuma ya keyboard
Wapigania uhuru walikuwa wakipigania nini?
 
Jana spika WA Bunge kasema hivi ni vita vya uchumi yaani Tanzania itakuwa na laana tu
Tulia anajulia wapi vita vya kiuchumi? Yaani tumeshindwa kupromote utalii kwa vivutio lukuki, tatizo dogo tu la Ngorongoro tunaona tunahujumiwa au vita ya kiuchumi?
Hatuna tofauti na mtu anayeona amelogwa kila anapofeli katika mipango yake.
 
kuwa mwenyeji haimaanishi ni kwako, ardhi yote ni mali ya serikali na inaweza kubadilishwa matumizi mda wwte, kuna watu wanawapa viburi wamasai halafu wao wako nyuma ya keyboard
Serikali ni nani?!
 
Back
Top Bottom