Nguvu ya Umma Senegal, funzo jingine kwetu

Nguvu ya Umma Senegal, funzo jingine kwetu

Sijui tunahitaji mafunzo mangapi ya aina hii ili tuamke..

Inawezekana "tulishakufa" siku nyingi lakini sisi tunajiona bado tupo hai, kama tunashindwa kujifunza kwa majirani zetu hapo Kenya, hivi inawezekana kweli tukaenda kujifunza Senegal?

Naona hili letu ni taifa teule la wanakondoo.
Kenyatta ktk Ile miaka baada ya uhuru alimwambia Nyerere , Mimi Kenya naongoza wagonjwa mahtuti lkn wewe kule kwako Tz unaongoza Marehemu.
 
Ninachelea kumnyooshea kidole Maalim Seif kama navyochelea kuwanyooshea Malema au Raila katika walio hai. Kwa maana nyingine hao wamefanya mengi kuliko labda yote tutakayoweza kuyafanya sisi katika maisha yetu yote.

Kwangu miye kina Mandela, Tutu, Mtikila na kina Nyerere wanaangukia kwenye daraja hilo.

Nipende kumwalika mjumbe kutoka zenji bar kwa mwongozo wake kumhusu Maalim na wasifu wake. Mjumbe huyu labda walikuwa naye katika harakati zao za mapambano.

Zawadini ikikupendekeza tafadhali, kwa maana ya nini kuandikia mate?
Mkuu yale maandamano kwangu ni kigezo tosha cha mambo ya kufanya na kuyatarajia.
Kwanza: Yalifanyika baada ya lawama nyingi kwamba uongozi ulikuwa hautendi kulingana na matakwa ya umma.
Pili: Yalipofanyika matokeo yakaonekana kwamba katika mambo kama yale pande zote zinaathirika kwani askari na raia wote walionja joto ya jiwe ingawa raia waliumia zaidi; ila ndio mambo. Utarajie nini kwa raia asiye na silaha?
Tatu: yalipofanyika, nadhani umma ulielewa ni kwanini voingozi walikuwa wanasita kuwaambia waingie barabarani.
Nne: Baada ya hayo nadhani sasa kutakuwa na maandalizi ya kutosha ili umma ujitayarishe.

Z
 
Mkuu yale maandamano kwangu ni kigezo tosha cha mambo ya kufanya na kuyatarajia.
Kwanza: Yalifanyika baada ya lawama nyingi kwamba uongozi ulikuwa hautendi kulingana na matakwa ya umma.
Pili: Yalipofanyika matokeo yakaonekana kwamba katika mambo kama yale pande zote zinaathirika kwani askari na raia wote walionja joto ya jiwe ingawa raia waliumia zaidi; ila ndio mambo. Utarajie nini kwa raia asiye na silaha?
Tatu: yalipofanyika, nadhani umma ulielewa ni kwanini voingozi walikuwa wanasita kuwaambia waingie barabarani.
Nne: Baada ya hayo nadhani sasa kutakuwa na maandalizi ya kutosha ili umma ujitayarishe.

Z

Asante sana mkuu ninyi ni kama kisima chenye hazina msituchoke tunapotafuta nasaha kwenu. Mlikopita tutapita na tutafika.

Wanasema waungwana:

"samaki akikuambia kuna mnyama majini anaitwa mamba naye ana jicho moja inabidi ukubali kwani huko yeye anaishi naye."

Sisi nani kuyaona mapungufu ya Maalim Seif? Au sisi nani kusimama kuonyesha makosa pale na pale ilipaswa kuwa hivi?

Mwuungwana mwingine alisema dunia inahitaji matendo siyo maoni.

Cc: denooJ, Sexless, Erythrocyte, Proved, Kinyungu, joka kuu na wapambanaji wengine Kwa taarifa.

Ninajua ukakasi uliopo katika njia hii hata kwa wale wanaojinasibu kuwa wapambanaji kweli kweli wakiwamo vigogo.

Inafanana na yule kijana aliyemwuliza Yesu afanye nini kuurithi ufalme wa mbinguni. Kuuza vitu vyake vyote awape maskini .... ilimwondolea ujasiri wote aliokuwa akijinasibu kuwa nao. Kumbe alikuwa msaka fursa tu.

Ni heri kuwa na wachache waliodhamiria kuliko wengi mzigo.

Nyomi aliyo nayo Raila haina watu 1,000. Wanachama 8m + wasio na tija wa nini?
 
Nguvu ya umma Tanzania mnataka watu tutolewe viuno?
Naona Polisi wameapa kulinda na kukitetea chama cha mwenge...
 
Nguvu ya umma Tanzania mnataka watu tutolewe viuno?
Naona Polisi wameapa kulinda na kukitetea chama cha mwenge...

Anatolewa je mtu kiuno kwenye nyomi kama hilo au hili linalojua uwepo wa mola kama almighty?

 
Back
Top Bottom