Nguvu ya Umma Senegal, funzo jingine kwetu

Nguvu ya Umma Senegal, funzo jingine kwetu

Duuh! Yawezekana mafunzo ya polisi na jeshi hapa Tanzania ni tofauti na nchi zingine. Hapa kwetu majeshi yetu yanaua raia ktk mikusanyiko kama hiyo. Mnakumbuka Arusha (Olasiti), Kinondoni na Iringa??
Wao hawachukui mateka(wafungwa) wao ni kujeruhi tu
 
Hii mambo ya kusubiri fulani alianzishe kwangu naona ni usanii tu, tunategana, kwasababu naamini kabisa, deep inside, hata wakina nyie mnaosubiri wengine waamke nanyi pia mnajua vizuri mnatakiwa kulianzisha, tatizo sijui mnachosubiri ni kitu gani...
Hili umeliona wapi katika niliyoandika hapo juu? Umejuaje kuwa ninasubiri..."
Ajabu chini unamzungumzia Sall unayedai ana malengo yake, sasa kama umeshajua hayo, palikuwa na haja ipi kuanza kwa kudai hujaelewa "maneno mengi" ya mleta mada?
Siwezi kuyaelewa hayo kutoka vyanzo vingine?

Nini kimekuleta wewe hapa kumjibia huyo ninayejibishana naye, ni mke wako?
 
Hii spirit ilikuwepo ndani ya chadema enzi zile Dr. Slaa ni katibu mkuu wa chama.

Nini sababu ya hii spirit kufa?
Sababu ni hizi hapa;-
1. Kubadili gia ya angani.
2. Hama hama ya makamanda ambao wamepiganiwa na wananchi kwa jasho na damu kurudi ccm.

Haya ndiyo yamesababisha watu kukata tamaa kukipambania chama maana wakaona kama wanasiasa wapo kwa ajili ya haja zao na siyo hoja zao.

Spirit hiyo iliyokuwapo enzi za Slaa haipo. Hilo ni jambo la kheri. Kujua mzizi wa fitna ulipo. Huo unaweza kuwa mwanzo wa kujinasua badala ya kukaa kuwalaumu wafuasi bila sababu za msingi.

Kutokea hapo tunayo nafasi ya kuzipanga safu zetu za uongozi kuwa kwenye utayari wa mapambano yenye mashiko.

Tupange safu zetu bila kuangaliana usoni:

Ieleweke kuwa viongozi wanaohitajika wanaonekana hivyo kwa matendo, maneno na hata kwa kuwaangalia usoni.

Ni muhimu ikafahamika wavumao baharini papa, lakini na wengine wapo. Kwa maana kamili ya kufahamu kuwa hayupo ambaye ni indispensable.
 
Hili umeliona wapi katika niliyoandika hapo juu? Umejuaje kuwa ninasubiri..."

Siwezi kuyaelewa hayo kutoka vyanzo vingine?

Nini kimekuleta wewe hapa kumjibia huyo ninayejibishana naye, ni mke wako?

Kwamba?

"Nini kimekuleta wewe hapa kumjibia huyo ninayejibishana naye, ni mke wako?"

Kulikoni kujidhalilisha hivyo ndugu?

Si makubaliano ni hoja kwa hoja? Povu lote hili kwamba ni mada tu hii?

Au kuna jingine ndugu?
 
Mimi naongoza waliolala,ipo siku watatoka usingizini na kuniuliza ila wewe mwenzang unaongoza maiti.

Maneno ya Jomo Kenyatta-akimwambia Nyerere.
Miaka ile tulimdharau sana Mzee Jomo lakini sasa anaonekana almost a genius kama alivyo P.W. Botha. Afrika tumetoka mbali kweli.
 
Hili umeliona wapi katika niliyoandika hapo juu? Umejuaje kuwa ninasubiri..."

Siwezi kuyaelewa hayo kutoka vyanzo vingine?

Nini kimekuleta wewe hapa kumjibia huyo ninayejibishana naye, ni mke wako?
Naona una quote kitu ambacho hata sijakuandikia wewe? hiyo paragraph ya kwanza nimemuandikia Uzima Tele acha kukurupuka, soma kuanzia mwanzo!.

Hiyo paragraph yako ya pili unaonesha umesha panic, bora nikuache tu, unaonekana mzee nikutunzie heshima tu!.
 
Kwamba?

"Nini kimekuleta wewe hapa kumjibia huyo ninayejibishana naye, ni mke wako?"

Kulikoni kujidhalilisha hivyo ndugu?

Si makubaliano ni hoja kwa hoja? Povu lote hili kwamba ni mada tu hii?

Au kuna jingine ndugu?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] stress tu hizo.
 
Kwamba?

"Nini kimekuleta wewe hapa kumjibia huyo ninayejibishana naye, ni mke wako?"

Kulikoni kujidhalilisha hivyo ndugu?

Si makubaliano ni hoja kwa hoja? Povu lote hili kwamba ni mada tu hii?

Au kuna jingine ndugu?
Kuna ligi hapa!
 
Uzima Tele nimekupata na hoja yako inayonitaka nilianzishe peke yangu wengine mfuate..

Hivi, kwanini mnisubiri nilianzishe peke yangu ili nanyi mnifuate? kwamba ndio tuseme bado mmelala mnasubiri mpaka nitakapolianzisha ndipo nanyi mtaamka?

Hebu tutazame mifano iliyoletwa na mleta mada au mingine ambayo tumekuwa tukiishuhudia mara kwa mara maeneo tofauti; anzia na Kenya, nenda hapo Senegal, tusogee kule North kwenye ile Arab Spring ya wakati ule...
hivi huko kote ni nani aliyelianzisha akawapeleka watu barabarani kuwatoa vyumbani kwao?

Hii mambo ya kusubiri fulani alianzishe kwangu naona ni usanii tu, tunategana, kwasababu naamini kabisa, deep inside, hata wakina nyie mnaosubiri wengine waamke nanyi pia mnajua vizuri mnatakiwa kulianzisha, tatizo sijui mnachosubiri ni kitu gani...

Ndio maana kule juu nikasema hili ni taifa teule la wanakondoo, wasio na tofauti na marehemu..

Mkuu posts 61, 66 na 67 Zina share uzoefu kutoka Zanzibar ambako hii mambo ilishafanywa japo haikufika mwisho. Huu ni mfano wao mwingine:



Ya nini kuandikia mate? Tubadilishane uzoefu na wenzetu hawa.

Tatizo letu liko kwenye viongozi hapa ndipo kwa kuanzia.

Cc: Zawadini
 
Miaka ile tulimdharau sana Mzee Jomo lakini sasa anaonekana almost a genius kama alivyo P.W. Botha. Afrika tumetoka mbali kweli.
Kujua jinsi alivyokuwa 'genious", hakuna hata mmoja kati ya hao waliolala na sasa wapo macho; hakuna hata mmoja wao anayethubutu kuhoji ardhi aliyonyang'anya huyo jiniasi wao.
Huenda watakuwa bado wamelala!
 
Ungekuwa unajua vizuri historia ya siasa za Senegal ungelijua ya Kwamba Mark Sall aliyevurumishwa alikuwa ndiye Mpinzani Namba Moja Senegal (tuseme kama Mbowe na Chadema yake hapa Tanzania). Baada ya kuupata Urais kwa kumuondoa Abdoulaye Wade akanogewa na asali (Ahahahahaha, asali) hadi kutaka kuchonga mzinga!

Tafsiri ya Senegal ni Kwamba tusiwaamini wapinzani hata kidogo. Bora kubaki na CCM yetu na wapinzani kuambulia viti viwili vitatu vya ubunge na udiwani! Ahahahahaha!!!!
Elewa kuwa mfumo wa vyama vingi vya siasa (multiparty democratic system) maana yake ni kuwapa wananchi uhuru na nguvu ya kuchagua viongozi na vyama wanavyovyitaka.

Hata wakikosea basi waweze kufanya mabadiliko kupitia sanduku la kura au bunge. Sio mfumo wa kukipa chama au mwanasiasa yeyote ukiritmba wa uongozi. Hakuna mambo ya “kuamini” mtu au chama. Ni suala la wengi wape.

CCM inaweza kuondolewa na kurejeshwa madarakani kwa kura. Si huu ujinga wa kung’ang’ania uongozi kwa wizi wa uchaguzi kwa kutumia vyombo vya dola.
 
Nilianza na swali la kwamba nani ataanza kuhamasisha? Kule watu walihamasishwa kwanza kuamini uongozi/viongozi wao kwamba kinachodaiwa ni kwa maslahi yao.

Walipohamasika wakajengwa kujiamini na hivyo kuthubutu kuingia barabarani kuandamana; wakaingia.
Kuna umuhimu wa kujenga hamasa na kujiamini kabla ya kutenda.

Watu pia wahamasishwe kupokea matokeo ya matendo yao hayo, watapokuwa tayari. Nadhani una kumbukumbu japo kidogo ya matokeo yenyewe. Kwenye hili ukipata nafasi wasikilize wale wajumbe walioteuliwa, sijui niseme, kufuatilia au kutafuta ukweli wa mambo? Hao watu wapo bado.

Z
Hili la kuhamasishwa kwanza nimelielewa, kwamba kabla ya kufikiria watu kwenda barabarani, kwanza nguvu kubwa iwekwe kwenye uhamasishaji ili kuwaandaa watu kuwa tayari kupigania haki zao.

Hili likifanikiwa ndio litatuondolea huu ukondoo tulionao hivi sasa, kwasababu huu ukondoo wetu hauwezi kuondoshwa na yanayotokea kwa majirani zetu, mpaka kwanza tumwagiwe maji baridi [hamasa] yakutuamsha.
 
Mwanzo umeandika ukidai hujui hiyo nyomi ina malengo yapi, hivyo unadai unamuona mleta mada ana maneno mengi yasiyoeleweka...

Ajabu chini unamzungumzia Sall unayedai ana malengo yake, sasa kama umeshajua hayo, palikuwa na haja ipi kuanza kwa kudai hujaelewa "maneno mengi" ya mleta mada?

Kama kweli ulikuwa hujaelewa, ungetakiwa umuache akufafanulie kwanza ndipo uanze kujadili, lakini kujadili kwa kirefu kitu ambacho unadai hukukielewa mwanzo naona hilo ni tatizo lako na sio vinginevyo..

Mkuu, JF kama kokoro ina wajumbe wa kila aina. Wengine inashangaza wanataka au hawataki nini.

Uzuri ni kuwa hao ni wachache wasiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili.
 
Kujua jinsi alivyokuwa 'genious", hakuna hata mmoja kati ya hao waliolala na sasa wapo macho; hakuna hata mmoja wao anayethubutu kuhoji ardhi aliyonyang'anya huyo jiniasi wao.
Huenda watakuwa bado wamelala!
Hilo sio suala langu hapa. Kinachonihuzunisha sana ni jinsi watu hao waovu walivyoweza kuona mapema sana kasoro za msingi (basic flaws) na unafiki ndani ya viongozi wetu waheshimiwa sana na ndani ya jamii zetu za Kiafrika. Tena mwanzoni kabisa baada ya uhuru.

Si uongo kwamba Nyerere, pamoja na dhamira yake njema sana kwa taifa, alitengeneza mfumo wa kidikteta unaolelewa na kulindwa sana na CCM hata kwa gharama ya damu ya wananchi. Ili tu asikosolewe wala kuwa na mshindani.

Aidha, karibia Afrika nzima walioongoza kupigania uhuru ndio pia walioasisi mifumo ya ukandamizaji, ufisadi na hujuma dhidi ya wananchi na chumi za nchi zao.
 
Hilo sio suala langu hapa. Kinachonihuzunisha sana ni jinsi watu hao waovu walivyoweza kuona mapema sana kasoro za msingi (basic flaws) na unafiki ndani ya viongozi wetu waheshimiwa sana na ndani ya jamii zetu za Kiafrika. Tena mwanzoni kabisa baada ya uhuru.

Si uongo kwamba Nyerere, pamoja na dhamira yake njema sana kwa taifa, alitengeneza mfumo wa kidikteta unaolelewa na kulindwa sana na CCM hata kwa gharama ya damu ya wananchi. Ili tu asikosolewe wala kuwa na mshindani.

Aidha, karibia Afrika nzima walioongoza kupigania uhuru ndio pia walioasisi mifumo ya ukandamizaji, ufisadi na hujuma dhidi ya wananchi na chumi za nchi zao.
Mkuu 'Drifter', kumhesabu Jomo kati ya viongozi "walioweza kuona kasoro..." za aina yoyote katika uongozi wa nchi yoyote siyo kweli hata kidogo.

Kulalamikia hali hii ya sasa inayoendeshwa na CCM, kuwa ni kwa sababu iliasisiwa na Mwalimu Nyerere baada ya miaka yote hii, pia siyo sahihi.

Inaweza kuwa sawa kumlaumu George Washington leo hii kwa hali aliyoiacha Marekani enzi za utumwa alipokuwa kiongozi wa nchi hiyo?
 
Back
Top Bottom