Nguvu ya Umma Senegal, funzo jingine kwetu

Nguvu ya Umma Senegal, funzo jingine kwetu

Alisema baba wa taifa, "binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja."

Kwa hakika Afrika ni moja na waafrika ni baba mmoja mama mmoja.

Haikuwa tofauti kwa kinara wa upinzani Senegal Ousumane Sonko hadi nguvu ya umma ilipoamua kutoa hukumu yake ya haki:

View attachment 2566852

Ousumane Sonko sasa yuko huru baada ya vishindo vya wakoma kuwafurusha washami.

Hii ni kama kwetu tu:

"Katiba mpya ipo kwa wakati tunaoutaka Sisi na kwa namna tunayoitaka. Hii ni hata kama tukiamua iwe hivyo sasa."

Bila ya hivyo ngonjera zitakuwapo nyingi, mara kuhusu pesa, wakati magoli tunanunua na tunawasaidia hadi ulaya kwa pesa zetu wenyewe.

Akiziita JPM -- "pesa zetu za ndani!"
Mkuu umenene; ila najiuliza hivi nani ataanza angalau kuhamasisha? Nashauri tufanye rejea ya maandamano ya Januari 27 kule ZANZIBAR. Mbinu gani ilitumika?
 
Ungekuwa unajua vizuri historia ya siasa za Senegal ungelijua ya Kwamba Mark Sall aliyevurumishwa alikuwa ndiye Mpinzani Namba Moja Senegal (tuseme kama Mbowe na Chadema yake hapa Tanzania). Baada ya kuupata Urais kwa kumuondoa Abdoulaye Wade akanogewa na asali (Ahahahahaha, asali) hadi kutaka kuchonga mzinga!

Tafsiri ya Senegal ni Kwamba tusiwaamini wapinzani hata kidogo. Bora kubaki na CCM yetu na wapinzani kuambulia viti viwili vitatu vya ubunge na udiwani! Ahahahahaha!!!!
Mawazo finyu hayo mbona Magufuri alileta udikteta wa wazi ambao waliomtangulia ndani ya CCM hawakuwahi kufanya?Kama yale matendo aliyoyafanya Magufuri wangeyafanya CHADEMA ungesema ndiyo sera za Chadema za kutojali shida za watu.Magufuri amekuwa Rais wa kwanza kufanya mambo ya kipuuzi na huku ccm wakiimba mapambio kwa vile tu falsafa yao ya ,'Zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa ccm 'zinafanya kazi hata kama taifa linaumia lakini kauli yao ya zidumu fikra sahihi kwa ccm ndiyo msingi wake.Huo ni upumbavu na ukosefu wa demokrasia ya kweli chama hicho .
Wakapanga njama za kumwongezea muda wa kutawala kumbe hawakujua kuwa Mungu wa mbinguni ana makusudi na Watanzania na siyo Magufuri.Endapo mtaendekeza huu ujinga na upumbavu Mungu ataendelea kuwaonyesha kuwa yeye ndiye mwenye mamlaka na taifa hili wala siyo mwenyekiti wa ccm.Vueni shuka jesi vaeni nguo nyeupe kwenye fikra zenu ili tuweze kusonga vizuri bila manung'uniko yoyote kwa Watanzania.
 
Mkuu umenene; ila najiuliza hivi nani ataanza angalau kuhamasisha? Nashauri tufanye rejea ya maandamano ya Januari 27 kule ZANZIBAR. Mbinu gani ilitumika?
Mkuu kwa sababu ya uzoefu tofauti ingependeza zaidi kupeana miongozo. Penye wengi hakuharibiki jambo.

Tusiokubaliana na hali iliyopo kukaa kimya au kushuritishwa kuridhia hakuwezi kuwa uchaguzi (option).

Kuna mahali tunakwama. Mawazo yangu ni kwenye uongozi, yaani organization.

Rejea nyuzi hizi:

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Magumu yetu Viongozi wa Upinzani mkwepe lawama vipi?

Itapendeza kusikia kutoka kwako mkuu.
 
Ungekuwa unajua vizuri historia ya siasa za Senegal ungelijua ya Kwamba Mark Sall aliyevurumishwa alikuwa ndiye Mpinzani Namba Moja Senegal (tuseme kama Mbowe na Chadema yake hapa Tanzania). Baada ya kuupata Urais kwa kumuondoa Abdoulaye Wade akanogewa na asali (Ahahahahaha, asali) hadi kutaka kuchonga mzinga!

Tafsiri ya Senegal ni Kwamba tusiwaamini wapinzani hata kidogo. Bora kubaki na CCM yetu na wapinzani kuambulia viti viwili vitatu vya ubunge na udiwani! Ahahahahaha!!!!

Wapi napingana na wewe ndugu kiasi cha kupeana maangalizo ya kuzijua siasa za wapi?

"Ni hivi ndugu hapendwi mtu!"

Hakuna rafiki wala adui wa kudumu bali agenda.

Ndiyo maana uchawa ni upumbavu. Tunachopigania ni mwenye nchi kuwa mwananchi.

Ukilikoroga tunapita na wewe hata kama jina lako ni TAL kipenzi wengi leo.

Kuna tatizo gani hapo?
 
Mkuu kwa sababu ya uzoefu tofauti ingependeza zaidi kupeana miongozo. Penye wengi hakuharibiki jambo.

Tusiokubaliana na hali iliyopo kukaa kimya au kushuritishwa kuridhia hakuwezi kuwa uchaguzi (option).

Kuna mahali tunakwama. Mawazo yangu ni kwenye uongozi, yaani organization.

Rejea nyuzi hizi:

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Magumu yetu Viongozi wa Upinzani mkwepe lawama vipi?

Itapendeza kusikia kutoka kwako mkuu.
Nilianza na swali la kwamba nani ataanza kuhamasisha? Kule watu walihamasishwa kwanza kuamini uongozi/viongozi wao kwamba kinachodaiwa ni kwa maslahi yao.

Walipohamasika wakajengwa kujiamini na hivyo kuthubutu kuingia barabarani kuandamana; wakaingia.
Kuna umuhimu wa kujenga hamasa na kujiamini kabla ya kutenda.

Watu pia wahamasishwe kupokea matokeo ya matendo yao hayo, watapokuwa tayari. Nadhani una kumbukumbu japo kidogo ya matokeo yenyewe. Kwenye hili ukipata nafasi wasikilize wale wajumbe walioteuliwa, sijui niseme, kufuatilia au kutafuta ukweli wa mambo? Hao watu wapo bado.

Z
 
Nilianza na swali la kwamba nani ataanza kuhamasisha? Kule watu walihamasishwa kwanza kuamini uongozi/viongozi wao kwamba kinachodaiwa ni kwa maslahi yao.

Walipohamasika wakajengwa kujiamini na hivyo kuthubutu kuingia barabarani kuandamana; wakaingia.
Kuna umuhimu wa kujenga hamasa na kujiamini kabla ya kutenda.

Watu pia wahamasishwe kupokea matokeo ya matendo yao hayo, watapokuwa tayari. Nadhani una kumbukumbu japo kidogo ya matokeo yenyewe. Kwenye hili ukipata nafasi wasikilize wale wajumbe walioteuliwa, sijui niseme, kufuatilia au kutafuta ukweli wa mambo? Hao watu wapo bado.

Z

Ninakusoma vyema ndugu mjumbe. Yapo mengi ya kujifunza katika bandiko lako fupi. Itakuwa muhimu kwa wataka haki hapa nchini kulidadavua vyema.

denooJ, Sexless, Econometrician , Erythrocyte makaveli10 na wapambanaji wengine mahiri, pana wito wenu mahsusi huku, badala ya kusubiria dodo kwenye minazi.

Kwa hakika hili ndilo linalokosekana. Niungane nawe kwenye kuyaona hivi:

1. Ni lazima ifahamike kuwa nguvu ya Umma ndiyo njia pekee ya kuaminika ya kupata suluhu kamili.

2. Njia hii pamoja na kuwa ndiyo bora zaidi ina gharama zake ambazo ni lazima tuwe tayari kuzilipa. Hizo ni pamoja na kudhulumiwa, kukamatwa, kufungwa, kuteswa, kujeruhiwa na hata kufa.

3. Kuwahamasisha watu ili kuwajengea kujiamini kwa ajili ya utekelezaji na ujasiri wa kuyakubali matokeo yoyote yatakayotokea, kunataka viongozi mahiri kweli kweli. Bila shaka wa aina ya kina Nyerere, Maalim Seif, Mandela, Malema, Tutu, Odinga, Sonko na wa namna hiyo.

4. Viongozi wetu ni muhimu wajkajihoji wenyewe kwa kuanzia, kuona kama kwenye kigezo #3 wanatosha.

Ieleweke kuwa viongozi wanaohitajika wanaonekana hivyo kwa matendo, maneno na hata kwa kuwaangalia usoni.

5. Badala ya kukaa kuwalaumu wananchi kuwa hawachukui hatua, tuwe tayari kupanga safu zetu za uongozi pasi na kuangaliana usoni.

Ni muhimu ikafahamika wavumao baharini papa, lakini na wengine wapo. Kwa maana kamili ya kufahamu kuwa hayupo ambaye ni indispensable.

Pamoja na kukushukuru niweke wazi kuwa nyuzi mbili hizi kutokea katika mchango wako naziona kuwa zingali zinaishi:

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Magumu yetu Viongozi wa Upinzani mkwepe lawama vipi?

Mdogo mdogo, tunasonga. Mdogo mdogo tutafika.

Cc: joka kuu, Yoda, Mag3, Proved
 
Mimi nina wasiwasi sana ule Mwenge wanakimbiza nchi nzima.Ule ndiyo utakuwa uchawi wa kutupumbaza.Haiwezekani watu wazima wanatumia mabilioni ya pesa kukimbiza moto nchi nzima.
Ule mwenge unatamkiwa maneno kadhaa kadhaa ya ajabu!
Nahisi ni ulozi unaoingia Moja kwa Moja kwenye vichwa vya raia
 
Wapi napingana na wewe ndugu kiasi cha kupeana maangalizo ya kuzijua siasa za wapi?

"Ni hivi ndugu hapendwi mtu!"

Hakuna rafiki wala adui wa kudumu bali agenda.

Ndiyo maana uchawa ni upumbavu. Tunachopigania ni mwenye nchi kuwa mwananchi.

Ukilikoroga tunapita na wewe hata kama jina lako ni TAL kipenzi wengi leo.

Kuna tatizo gani hapo?
Nimekuelewa Mkuu.
 
..Maalim Seif alikuwa na nguvu na ushawishi mkubwa lakini alikuwa anafeli na kupata kigugumizi dakika za mwisho za kuchukua ushindi wake.
 
..Maalim Seif alikuwa na nguvu na ushawishi mkubwa lakini alikuwa anafeli na kupata kigugumizi dakika za mwisho za kuchukua ushindi wake.
Nje ya uwanja tunaweza kuwa wazuri sana kwenye kuona makosa. Kwamba pale yule angefanya au asingefanya vile.

Ngoma Huwa iko field ambako issue inakuwa si uchambuzi tena bali kuwajibika kwa vitendo.

Maalim Seif alikuwa gari kubwa kwenye mambano yake. Akiipigania Zanzibar huru ambapo alichelea tu, kuiona Zanzibar ikiteketea kwa moto.

CC: Zawadini
 
Nje ya uwanja tunaweza kuwa wazuri sana kwenye kuona makosa. Kwamba pale yule angefanya au asingefanya vile.

Ngoma Huwa iko field ambako issue inakuwa si uchambuzi tena bali kuwajibika kwa vitendo.

Maalim Seif alikuwa gari kubwa kwenye mambano yake. Akiipigania Zanzibar huru ambapo alichelea tu, kuiona Zanzibar ikiteketea moto.

CC: Zawadini

..kwangu mimi Maalim Seif anabeba lawama za kushindwa kuwaongoza wananchi kutetea ushindi walioupata.

..Ccm wako madarakani Znz kwasababu viongozi wao hawaogopi kutetea na kulinda wizi wa kura. Wanaiba kura, wanalinda, na kuchukua ushindi.
 
Mimi nina wasiwasi sana ule Mwenge wanakimbiza nchi nzima.Ule ndiyo utakuwa uchawi wa kutupumbaza.Haiwezekani watu wazima wanatumia mabilioni ya pesa kukimbiza moto nchi nzima.
eti unapeleka ujumbe ma tv na ma redio yote na magazeti yanafanya nini hadi watu wafukuze mwenge kupata ujumbe mfano "ukimwi"
 
Sijui tunahitaji mafunzo mangapi ya aina hii ili tuamke..

Inawezekana "tulishakufa" siku nyingi lakini sisi tunajiona bado tupo hai, kama tunashindwa kujifunza kwa majirani zetu hapo Kenya, hivi inawezekana kweli tukaenda kujifunza Senegal?

Naona hili letu ni taifa teule la wanakondoo.
Upo sahihi kabisa mkuu
 
3. Kuwahamasisha watu ili kuwajengea kujiamini kwa ajili ya utekelezaji na ujasiri wa kuyakubali matokeo yoyote yatakayotokea, kunataka viongozi mahiri kweli kweli. Bila shaka wa aina ya kina Nyerere, Maalim Seif, Mandela, Malema, Tutu, Odinga, Sonko na wa namna hiyo.
Hii spirit ilikuwepo ndani ya chadema enzi zile Dr. Slaa ni katibu mkuu wa chama.

Nini sababu ya hii spirit kufa?
Sababu ni hizi hapa;-
1. Kubadili gia ya angani.
2. Hama hama ya makamanda ambao wamepiganiwa na wananchi kwa jasho na damu kurudi ccm.

Haya ndiyo yamesababisha watu kukata tamaa kukipambania chama maana wakaona kama wanasiasa wapo kwa ajili ya haja zao na siyo hoja zao.
 
Watanzania wanayo imani kubwa Sana na serikali ya CCM katika kuwaongoza na kuwatumikia,wanaelewa na kutambua dhamira njema iliyo nayo serikali ya CCM katika kuwahudumia,ndio sababu ya Kuendelea kuwa watulivu n wenye Imani kubwa kwa serikali ya ccm maana wanatambua usikivu wa serikali yao pamoja na uzalendo wa viongozi wao wa ccm
nani anafaidi zaidi, mtoa sadaka au mpokeaji? watu wamechagua kuhubiri ili kupokea na si kutoa. nani aliyeko mbele kwa ajili ya kutoa huko ccm?
mchunga ng'ombe huwaongoza ili wale kwa faida yake. tusiwe kama ng'ombe, faida kwa mfugaji.
 
..kwangu mimi Maalim Seif anabeba lawama za kushindwa kuwaongoza wananchi kutetea ushindi walioupata.

..Ccm wako madarakani Znz kwasababu viongozi wao hawaogopi kutetea na kulinda wizi wa kura. Wanaiba kura, wanalinda, na kuchukua ushindi.

Ninachelea kumnyooshea kidole Maalim Seif kama navyochelea kuwanyooshea Malema au Raila katika walio hai. Kwa maana nyingine hao wamefanya mengi kuliko labda yote tutakayoweza kuyafanya sisi katika maisha yetu yote.

Kwangu miye kina Mandela, Tutu, Mtikila na kina Nyerere wanaangukia kwenye daraja hilo.

Nipende kumwalika mjumbe kutoka zenji bar kwa mwongozo wake kumhusu Maalim na wasifu wake. Mjumbe huyu labda walikuwa naye katika harakati zao za mapambano.

Zawadini ikikupendekeza tafadhali, kwa maana ya nini kuandikia mate?
 
Excessive use of a pronoun "I". Egocentrism is a curable disease. Please consider to seek for medical advice.
Can't say much about this, in substance or proper use of language.
 
Back
Top Bottom