Ni aibu kwa vyuo vikuu hapa nchini kushindwa kugundua chanjo ya Corona na sasa vinashindana kutoa tahadhari

Prof ni utafiti hawa wetu wametafit nini? Acha tupige nyungu
hawa wakwetu wako kwenye siasa. research hata za madawa hawafanyi.
sisi wataalam wetu wanasubiri mzungu atengeze dawa halafu waje waijadili. ndio wasomi wetu hao
 
 
Kama taifa tunashida kubwa zaidi yavkushindwa kwa vyuo vikuu kuwa na mchango unaoonekana kwa taifa,fikiria kama uwekezaji ungefanyika wa kiwango cha hivi karibuni katika taifa,kwenye kilimo,afya ikiwa ni pamoja na tafiti,na sayansi na tekinologia.Baada ya muda tungekuwa na jeuri ya Kumbeza beberu tunayejidai kumchukia ilhali tunamtegemea kiasi cha kumkabidhi hata uangalizi wa afya zetu.
 
Usikimbilie kulaumu tu sio kweli kwamba vyuo vimekaa kimya tu , Mfano hata sasa ukipita chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa wale ambao wako Dar kuna foleni kubwa pale wanauza dawa ambayo ni ya kujifukiza inataoa matokeo makubwa sana hasa kwa waleambao walikua na hali mbaya, tumesikia pia UDOM wamekuja na ya kwao, MUHAS kila siku Dr.Otieno anaelimisha juu ya tiba za asili na mimea kibongobongo hawajalala nakuhakikishia hata wewe mleta uzi katumie hayo matone ya UDSM hutojuta hata kama huna nyiumonia utakaa sawa , haya mambo yanaendana na funds na wakati mwingine political will, kwahiyo kuwatupia mawe wasomi kuwa hawako mstari wa mbele sio sawa kabisa , mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni
 
Lkn mkuu vyuo vikuu vipo miaka mingi sana kabla ya awamu hii
Katika Afrika maendeleo hakuna kwa sababu ya siasa za hovyo,badala ya siasakuwa
dira yakutuongoza imekuwa dira yakutupoteza.Tulipofika Afrika inahitaji ukombozi kwa mara nyinvine.
 
 
Unamaanisha hata kile chuo cha chama kivukoni nacho wameshindwa kugundua chanjo
 
Wanaotuangusha Ni Wasomi Wameshindwa Kufikiria Nje Ya Box!!
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Hiyo pesa ndogo sana kama pesa za sherehe ya uhuru inayofanyika siku moja zinapatikana leo hii hiyo pesa isipatikane?
 
Uko sahihi kabisaaaa!!!!!!

Vyuo vikuu vyetu vinatia sana aibu. Ma-Professor na Ma-Doctors wameacha kufanya tafiti mbalimbali na zenye tija kwa manufaa ya taifa wanakimbilia kwenye siasa wanakoishia kufanya kazi za ukarani tu.

Hawa ma-professor wetu wameendekeza njaa tu kwaajili ya matumbo yao na familia zao. Matokeo yao wameshindwa kufanya tafiti za kisayansi ili kupata chanjo na tiba ya; ukimwi, cancer, maralia, BP, Sukari, figo n.k.

Nakumbuka miaka ya nyuma Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere alianzisha taasisi iliyoitwa the village of science and technology lakini ma-professor akina Professor Shayo aliyekuwa wa chama cha Demokrasia Makini wakaki-dump wakaingia kwenye siasa.

Ninaomba wasomi wetu wabadilike. Angalia nchi za wenzetu huko Amerika na Europe ni vigumu kuwaona ma-professor na ma-doctors (PhD) wanaingia kwenye siasa wenzetu wanabaki kwenye vyuo na taasisi za utafiti ili wafanye kazi zinazoendana na taaluma zao.
 
Umeonea vyuo vyetu vikuu na vingine vingi vya hata mataifa makubwa. Kazi ya vyuo vikuu ni kuchochea fikirishi ya kitafiti. Vipo vyuo ambayo chokozo hizo zimetoa matokeo, lakini utafiti mkubwa unahitaji muda, na fedha nyingi sana!!!! Uwekezaji ndio tatizo la msingi na wanaoweza kufanya hivi ni wale wanaotarajia faida baada ya matokeo sahihi ya tafiti zao. Vyuo hivi havina pesa kiasi hicho!!!

Umeshajiuliza kwanini makapuni ya madawa ndio yanayofanya tafiti sio vyuo vikuu??? Utafiti sio jambo la lelemama. Hasira zako ziko misplaced!!
 
Lipo tatizo mahali zaidi ya kwa hao madoc na profs
 
Ni kweli vyuo vikuu vyetu vina mapungufu, lakini kuvilaumu kwamba vimeshindwa kufanya tafiti ambazo zingewezesha upatikanaji wa chanjo ya korona, ni kutojua usemalo.
1) Vyuo vikuu vikongwe ni mali ya serikali. Serikali ndio mwekezaji na ndiye anayeweka malengo ya nini kitokee au kizalishwe.
2) mpaka sasa kuna mengi sana yamegunduliwa au kutafitiwa na wasomi wetu, ambapo wengi wamefanya vizuri katika maabara kubwa za ulaya, au katika joint research, ni juu ya serikali kuamua ifanye nini na tafiti hizo.

3) Tafiti kama za chanjo ya korona kinahitaji maabara za kisasa, wataalamu waliobobea, wadau wenye utayari. Vyuo vikuu vyetu vinafanya kazi katika mazingira magumu sana. Hawa SUA wanahusika na utafiti wa panya mtegua mabomu aliyepata tuzo kubwa duniani. Ni SUA waliotoa mkakati wa KILIMO KWANZA, ambapo ile orijino ilichakachuliwa kikabaki kimkakati cha watu kupiga hela. SUA walilalamika sana kwa uchakachuaji huo. Huo ni mfano wa jinsi mmiliki wa chuo anavyokwamisha utendaji. Unaweza kuwa na wataalamu wazuri lakini unahitaji kuwa na programu nzuri ya utafiti, na iliyojengwa kwa muda mrefu. Pamoja na kwamba Marekani wanavyo vyote hivyo, ilihitajika fedha nyingi sana iwekezwe na serikali. Sisi serikalivipo tayari kuwekeza fedha inayohitajika?

Kama serikali ikiamua, inawezekana. Lakini waache tabia ya kuchomoa wasomi, badala ya kufundisha, kitafiti na kuzalisha, wanakuwa na kazi za ofisini na siasa
 
Umeandikaujinga mtupu hauko tofauti na ndugai
 
Mkuu hivi umesoma wewe au umesingiziwa kusoma?
Na sijui kama umesoma, ni mpaka level gani sijui!

Vyuo basically ni sehemu ambayo kweli kunatakiwa kuwepo research.
Lakini watu hawajui nyuma ya pazia kuwa hizo research LAZIMA ziwe funded na private/Public entities.

Researcher hawezi kurupuka na kufanya research bila kupata Sponsor au Funding Agent.
Makampuni makubwa sana kama Pfizer hiyo ndio biashara yao, wanakopa hadi benki au masoko ya hisa ili wafanye research ya dawa fulani na inakuwa patented ikiptikana.

Hivyo Chuo/Vyuo nchini Tanzania havina ubavu wowote kufanya research ya dawa yoyote kwa funding ya GOT tunayoifahamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…