Mama yangu alikuwa mpika na muuza gongo kule Gongo la mboto mapolisi waliweka informer kila tukiwa tunaenda kupiga gongo wanakuja wanamkamata mama analia tukiwa mapolini kule kinyerezi(enzi hizo kinyerezi kulikuwa pori la kukamata hadi sungura na digi digi kabisa) sasa mama alikamatwa mfuluzo mbaya zaidi wakati mahita anatawazwa kuwa IGP si akapitisha opereshen maalum ambayo mama akabebwa na ma pipa na mtambo wa gongo mpaka kituoni akatuacha mimi na wadogo zangu watatu.Mimi niliachwa kwa sababu ni mdogo ikabidi mimi nikabidhiwe jezi na mchezo sijauelewa hivyo nikajikuta nina majukumu ya kulisha wadogo zangu na kumtafutia mama chakula ili ale kule lock up kwa sababu ndugu tulikuwa nao wachache pale Dar ambao kama vile walitutenga kwa sababu ya umasikini.Dingi ameshasepaga muda kakimbia familia sababu ni hiyo hiyo umasikini.
Ikanibidi niwe naenda matembezini na kiroba kwapani huko kutafuta mashamba ya watu mfano wa mashamba nilikuwa nayaonea ni ya miogo na viazi na minazi na mapera kule ulongoni enzi hizo hata TANESCO hawajaweka umeme hata nyumba moja.
Huwezi amini nilijua hadi kupandia minazi ili niibe madafu usiku anyway tu cut the story nilikuwa naondoka na kiroba kitupu nawaacha madogolas wamejikunyata nikirudi wanabidi wapokeee chochote ntachokuja nacho kwenye kiroba kuna siku nilikimbizwa na mwenye shamba ambae lilikuwa na miogo mitamu kumbe aliweka lindo baada ya kuona katikati ya shamba lake nimelaza mashina yote aisee.
KUMBE kitendo cha kuwa namletea miogo kila siku maza mapolisi wakawa wananichora na kunidiscuss siku moja nilikosa miogo nikapeleka madafu mawili mama aliachiwa tuongee nae nje ya kituo si akaanza kulia na kuniambukiza kilio na mimi kumbe ile ilikuwa pona yake si mkuu wa kituo akazipata zile habari maana kumbe watu wanapewa dhamana mimi sijui taratibu wakaniuliza eti kesho nije na mkubwa tumdhamini kwa vile ndugu walishatutenga ikabidi nikamchukue MAMA SALAWALA(sijui yupo wapi) ambae huwa tunamuuziaga gongo anaishi mzambarauni Gongo la mboto.
Mama akatoka mtaji ukawa umefilisiwa maana walibeba mtambo wa gongo na mapipa yote ikabidi mama awe raia mwema akaanza kuazima shamba tukawa tunalima huku tunashindia maembe
Anyway njaa ni noma inakosesha hadi ladha ya maisha
Sitaki kueleza mengi at the end nikafaulu mtaa mzima kwenda shule ya AZABOY nikaona shida zinazidi nyumbani hata nauli nikakosa ikabidi niende kujipendekeza kwa madogo wa dogo dogo center Mabibo karibia na shule ya loyola walipangishiwa nyumba na wadhamini wao wazungu.
Story ni ndefu ila acheni nijiite Billie humu JF kwa sababu hata mama yangu kwa sasa nimuanzishia biashara anaishi kwenye nyumba nzuri na kuna flame za kupangisha 8 na ana nyumba za wapangaji 5.
Upande wa mimi now nilivyo sitaki kusema ila nipo na familia ambayo watoto kula mpaka uwashikie fimbo au uwawekee katuni na almost kila kitu ndani hadi vyakula vinaharibika.SIJITAPI NAONGEA UKWELI TUPU NIMEJIFUNZA SHIDA NI ELIMU NZURI SANA KAMA UKIWEZA KUZITOROKA.