Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

Nlienda bush kumsalimia mjomba angu alikua ni mkulima amevuna mahindi mengi ya njano lakini anko aliishi kivyake hakua na mke dah alipika ugali mkubwa wa njano nikajua anko ameandaa mboga akatenga ugali kwenye chungu atoa chupa inamafuta ya ng'ombe (samli) yameganda akaipisha juu ya jiko ikayeyuka akamimina kwenye bakuli akaweka chumvi ikawa ndio mboga unamega tonge unatoezea kwenye mafuta unameza ugali

Ugali na samli ni mtamu sana,yaani ukiniwekea pilau na ugali na samli nachagua ugali na samli ni chakula kizuri sana kwangu kuwahi kukijua
 
Yasikie tu! Usiombe yakukute!
img_1_1684594535034.jpg
 
Nimelala sana msikitini kwenye ile mikeka ya msikiti mpaka nikaota sugu kwenye mgongo na makalioni, enzi hizo nasoma chuo na sina hela ya kupanga chumba......ukiona mtu anamiliki vitu vya thamani izuie sana nafsi yako usimuonee husda au wivu.....kuna watu mafanikio waliyonayo ni haki yao wamepitia mengi magumu kufika hapo walipo
 
Ufukara si kitu chema kwa kweli, nakumbuka ilikuwa mwaka 2002 niliacha shule Mpwapwa Sekondari nikiwa naingia kidato Cha tatu kwa kukosa ada Elfu thelathini na Tano tu, familia yangu ilikuwa inapitia kipindi kigumu Sana kiuchumi baada ya redundunce ya mzee.
 
Mama yangu alikuwa mpika na muuza gongo kule Gongo la mboto mapolisi waliweka informer kila tukiwa tunaenda kupiga gongo wanakuja wanamkamata mama analia tukiwa mapolini kule kinyerezi(enzi hizo kinyerezi kulikuwa pori la kukamata hadi sungura na digi digi kabisa) sasa mama alikamatwa mfuluzo mbaya zaidi wakati mahita anatawazwa kuwa IGP si akapitisha opereshen maalum ambayo mama akabebwa na ma pipa na mtambo wa gongo mpaka kituoni akatuacha mimi na wadogo zangu watatu.Mimi niliachwa kwa sababu ni mdogo ikabidi mimi nikabidhiwe jezi na mchezo sijauelewa hivyo nikajikuta nina majukumu ya kulisha wadogo zangu na kumtafutia mama chakula ili ale kule lock up kwa sababu ndugu tulikuwa nao wachache pale Dar ambao kama vile walitutenga kwa sababu ya umasikini.Dingi ameshasepaga muda kakimbia familia sababu ni hiyo hiyo umasikini.
Ikanibidi niwe naenda matembezini na kiroba kwapani huko kutafuta mashamba ya watu mfano wa mashamba nilikuwa nayaonea ni ya miogo na viazi na minazi na mapera kule ulongoni enzi hizo hata TANESCO hawajaweka umeme hata nyumba moja.
Huwezi amini nilijua hadi kupandia minazi ili niibe madafu usiku anyway tu cut the story nilikuwa naondoka na kiroba kitupu nawaacha madogolas wamejikunyata nikirudi wanabidi wapokeee chochote ntachokuja nacho kwenye kiroba kuna siku nilikimbizwa na mwenye shamba ambae lilikuwa na miogo mitamu kumbe aliweka lindo baada ya kuona katikati ya shamba lake nimelaza mashina yote aisee.
KUMBE kitendo cha kuwa namletea miogo kila siku maza mapolisi wakawa wananichora na kunidiscuss siku moja nilikosa miogo nikapeleka madafu mawili mama aliachiwa tuongee nae nje ya kituo si akaanza kulia na kuniambukiza kilio na mimi kumbe ile ilikuwa pona yake si mkuu wa kituo akazipata zile habari maana kumbe watu wanapewa dhamana mimi sijui taratibu wakaniuliza eti kesho nije na mkubwa tumdhamini kwa vile ndugu walishatutenga ikabidi nikamchukue MAMA SALAWALA(sijui yupo wapi) ambae huwa tunamuuziaga gongo anaishi mzambarauni Gongo la mboto.
Mama akatoka mtaji ukawa umefilisiwa maana walibeba mtambo wa gongo na mapipa yote ikabidi mama awe raia mwema akaanza kuazima shamba tukawa tunalima huku tunashindia maembe
Anyway njaa ni noma inakosesha hadi ladha ya maisha
Sitaki kueleza mengi at the end nikafaulu mtaa mzima kwenda shule ya AZABOY nikaona shida zinazidi nyumbani hata nauli nikakosa ikabidi niende kujipendekeza kwa madogo wa dogo dogo center Mabibo karibia na shule ya loyola walipangishiwa nyumba na wadhamini wao wazungu.
Story ni ndefu ila acheni nijiite Billie humu JF kwa sababu hata mama yangu kwa sasa nimuanzishia biashara anaishi kwenye nyumba nzuri na kuna flame za kupangisha 8 na ana nyumba za wapangaji 5.
Upande wa mimi now nilivyo sitaki kusema ila nipo na familia ambayo watoto kula mpaka uwashikie fimbo au uwawekee katuni na almost kila kitu ndani hadi vyakula vinaharibika.SIJITAPI NAONGEA UKWELI TUPU NIMEJIFUNZA SHIDA NI ELIMU NZURI SANA KAMA UKIWEZA KUZITOROKA.
 
Mama yangu alikuwa mpika na muuza gongo kule Gongo la mboto mapolisi waliweka informer kila tukiwa tunaenda kupiga gongo wanakuja wanamkamata mama analia tukiwa mapolini kule kinyerezi(enzi hizo kinyerezi kulikuwa pori la kukamata hadi sungura na digi digi kabisa) sasa mama alikamatwa mfuluzo mbaya zaidi wakati mahita anatawazwa kuwa IGP si akapitisha opereshen maalum ambayo mama akabebwa na ma pipa na mtambo wa gongo mpaka kituoni akatuacha mimi na wadogo zangu watatu.Mimi niliachwa kwa sababu ni mdogo ikabidi mimi nikabidhiwe jezi na mchezo sijauelewa hivyo nikajikuta nina majukumu ya kulisha wadogo zangu na kumtafutia mama chakula ili ale kule lock up kwa sababu ndugu tulikuwa nao wachache pale Dar ambao kama vile walitutenga kwa sababu ya umasikini.Dingi ameshasepaga muda kakimbia familia sababu ni hiyo hiyo umasikini.
Ikanibidi niwe naenda matembezini na kiroba kwapani huko kutafuta mashamba ya watu mfano wa mashamba nilikuwa nayaonea ni ya miogo na viazi na minazi na mapera kule ulongoni enzi hizo hata TANESCO hawajaweka umeme hata nyumba moja.
Huwezi amini nilijua hadi kupandia minazi ili niibe madafu usiku anyway tu cut the story nilikuwa naondoka na kiroba kitupu nawaacha madogolas wamejikunyata nikirudi wanabidi wapokeee chochote ntachokuja nacho kwenye kiroba kuna siku nilikimbizwa na mwenye shamba ambae lilikuwa na miogo mitamu kumbe aliweka lindo baada ya kuona katikati ya shamba lake nimelaza mashina yote aisee.
KUMBE kitendo cha kuwa namletea miogo kila siku maza mapolisi wakawa wananichora na kunidiscuss siku moja nilikosa miogo nikapeleka madafu mawili mama aliachiwa tuongee nae nje ya kituo si akaanza kulia na kuniambukiza kilio na mimi kumbe ile ilikuwa pona yake si mkuu wa kituo akazipata zile habari maana kumbe watu wanapewa dhamana mimi sijui taratibu wakaniuliza eti kesho nije na mkubwa tumdhamini kwa vile ndugu walishatutenga ikabidi nikamchukue MAMA SALAWALA(sijui yupo wapi) ambae huwa tunamuuziaga gongo anaishi mzambarauni Gongo la mboto.
Mama akatoka mtaji ukawa umefilisiwa maana walibeba mtambo wa gongo na mapipa yote ikabidi mama awe raia mwema akaanza kuazima shamba tukawa tunalima huku tunashindia maembe
Anyway njaa ni noma inakosesha hadi ladha ya maisha
Sitaki kueleza mengi at the end nikafaulu mtaa mzima kwenda shule ya AZABOY nikaona shida zinazidi nyumbani hata nauli nikakosa ikabidi niende kujipendekeza kwa madogo wa dogo dogo center Mabibo karibia na shule ya loyola walipangishiwa nyumba na wadhamini wao wazungu.
Story ni ndefu ila acheni nijiite Billie humu JF kwa sababu hata mama yangu kwa sasa nimuanzishia biashara anaishi kwenye nyumba nzuri na kuna flame za kupangisha 8 na ana nyumba za wapangaji 5.
Upande wa mimi now nilivyo sitaki kusema ila nipo na familia ambayo watoto kula mpaka uwashikie fimbo au uwawekee katuni na almost kila kitu ndani hadi vyakula vinaharibika.SIJITAPI NAONGEA UKWELI TUPU NIMEJIFUNZA SHIDA NI ELIMU NZURI SANA KAMA UKIWEZA KUZITOROKA.

[emoji22]

Apo kwenye gongo dah
 
Back
Top Bottom