othuman dan fodio
JF-Expert Member
- Jan 2, 2018
- 6,850
- 11,033
Usirudie tena huo ujinga wa kukatiza mbuga za wanyama zenye mbwa mwitu.....Kipindi Nikiwa na miaka 16, niliwahi kutiroka mateso ya mama mkubwa na kutembea kuanzia Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha Hadi Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, umbali wa kilometa zaidi ya 400 kwa muda wa siku 19 kukatisha kioande cha mbuga ya tarangire. Kulikuwa na wanyama wengi isipokuwa simba, tembo na chui. Nikikutana na kundi kubwa la mbwa mwitu lakini Kama siku yako haijafika, haijafika tu.
Whaat??? OoghMaisha ni safari ndefu sana nikikumbuka ya nyuma namwambia tu Mungu Asante umejua kunifurahisha[emoji120]nishawahi kuzimia na njaa mara mbili
Ukweli mtupu .Njaa haizoeleki kaka.
Umesema kweli ukikipata kula ila pia kila unapojaaliwa kumpa mwingine chakula basi fanya hivyo.
Unaweza dharau kipande cha muhogo lakini kikamaanisha karamu kwa mwingine.
Hata mimi naamini hivyo. Hii dunia haikuwa mahala pake.Huyu mwanao ndo maana mungu alimpenda zaidi, alikuwa na moyo wa pekee
Nikusahishe kidogo mkuu, ukipata nafasi ya kula na unaijua njaa, ukijaliwa kupata nafasi ya kuwasaidia wengine chakula usifikirie mara mbili.... njaa sio kabisa.Ukipata nafasi ya kula aisee kula, kuna watu hiki chakula wanakitafuta hawakipati.
Na Daima shida zinakujaga kwenye hali hii ya mke na mtoto mdogo. Ile kauli ya SINA HATA MIA ukisikia mtu anasema unaweza sema ana utani.Usiombe umasikini ukukute ukiwa na familia yaani una mke na watoto wadogo aisee utalia, bora nyie yanawakuta mkiwa bachelor
Kaka acha tu kufulia kusikie kwa jirani tu. Na nikifulia najikuta mikono inaishiwa nguvu kabisa na mwili unauma kama nimepigwa.Nimeandika, nikafuta, nimeandika tena nikafutaβ¦..aisee nikianza kueleza vile umasikini umenifanya server za JF zitajaa leo π , ila umasikini usikie kwa watu tu nyie ππ.
Cvez Jobless mwenzangu una lolote la kuchangia hapa? πππ
Acha tuendelee kula bata tu.
Najua Kile unasema. Life sucks aisehUnaweza ukadhani ni masihara ila hivi vitu vipo mkuu, kuna muda nilikuwa naona kabisa vidonda vya tumbo vinanyimelea, ile njaa ya kukosa kula siku nzima unaona kabisa tumbo linawaka moto kama limemwagiwa tindi kali.
Ukipata nafasi ya kula aisee kula, kuna watu hiki chakula wanakitafuta hawakipati.
Mke wangu kushindia mua tu tena akiwa mjamzito. Mungu atusaidie kwa kweli.
Muwa paipu au muwa gani?
Pumbavu wewe. Wewe unakula muwa gani?
Tulia mtani usiharibu mandhari π€£Heeee nyie mmetokea wapi mbona wanajf hatupo hivo
Muhimu sana kuwa na Duka unaloaminika. Yaani Unakuwa unafanya Madeni Recycling. Unalipa na kukopa hapo hapo.Nilipauka nkapauka kweli.
Kulikua na maduka 2 ambayo nilikua mteja pendwa (very important uwe na maduka ambayo wewe ni customer wa kila siku), sasa nkaanza kukopa bwana. Nmekopa nkakopa tena ikafika kipindi mangi akaniambia, mjuba, sasa hv unakopa mtajo, em nenda katafte kwanza uje upunguze madeni.
Nkakosa pa kwenda.
Sitasahau siku nmelala njaa. Imefika saa nane usingiz ukapaa na njaa takatifu, nkaenda bombani nkafungua maji nkanywa. Maji ya Dom yana chumvi wazee, ile chumvi ndo ikazidisha njaa kbsa.
Sikulala kabisa. Asubuh nmeamka hata nguvu ya kutembea sina.
Msela wangu mmoja sijui alijuaje, akanipigia sim akanipa hi af akanitumia li twente ndo nkasogeza maisha.
This life be humble aisee.
Hawa binadamu unaweza kuta waliumbwa kuwa Malaika wakajikuta wapo duniani aiseh.Hata mimi naamini hivyo. Hii dunia haikuwa mahala pake.
Yule jamaa alikuwa na roho ya kipekee. Hakusubiri kuombwa.
Hii story yangu ni cha mtoto, baada ya mauti yake waliibuka wengi mno. Kuna aliowapa hifadhi ya makazi, aliowapa mitaji na hata aliolipia ada za watoto wao.
Kuna binadamu Mungu aliwaumba waje kuwa mfano wa wema tu kwa binadamu halafu waondoke.
Hii comment yako imenikumbusha mbali sana.Na Daima shida zinakujaga kwenye hali hii ya mke na mtoto mdogo. Ile kauli ya SINA HATA MIA ukisikia mtu anasema unaweza sema ana utani.
Kufulia sio poa kabisaKufulia wanakuita kwa kimombo "Broke", kwa kinaijeria "sapaa", kusikiage tuuuu!
Nakumbuka wiki nzima niliwahi kuwa na bajeti ya 200 kwa siku naenda kula mhogo wa kuchemsha, nje ya hapo natembea kama saa zima sehemu flani ilikuwa na miti ya mapera na peaches.
Nilikuwa napenda sana mambo ya simu na niliweza kuwarekebishia watu wengi vitu vya kwenye simu ila mimi nilikuwa na kitochi kimechoka.
Nilianza kuhesabu majina kwa cm huku nikisema Nani anaweza kuniazma bila kuanza kunipa darasa la maisha ama kunitangaza
Sendo yangu ilikatika upande moja nikawa naipiga msumali ijishike, baada ya siku 3 inaachia napigilia tena, ilijaa matundu kibao
Nilikuwa natoa nguo zote kwenye tenga na kuanza kusachi moja moja kama ina hela naambulia patupu, kesho narudia nazikunguta kabisa lakini wapi
DuhIla Mungu si wa mmoja, hivi karibuni tu kulipitishwa mchango wa kifamilia, mzee kashikwa na tezi dume analia kama mtoto. Watoto wake hakuna hata mmoja mwenye muelekeo.
Aisee ni noma niliona kwa marehemu mzee wangu baada ya kupunguza kazini.Usiombe umasikini ukukute ukiwa na familia yaani una mke na watoto wadogo aisee utalia, bora nyie yanawakuta mkiwa bachelor
Sema umeshayapatia mwanangu π mi nakukumbusha tu namba yangu ni ile ile mkuu fanya hata ten mwanangu ππKaka acha tu kufulia kusikie kwa jirani tu. Na nikifulia najikuta mikono inaishiwa nguvu kabisa na mwili unauma kama nimepigwa.
Maisha yackuunga unga sio poa kabisa.