sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,264
- Thread starter
-
- #121
Mkuu, tunakisubiri kwa hamu unitagNitakuja na kisa changu namna nilijifanya mganga wa kienyeji ili nimpige dada mmoja wa kichaga 600,000 ili nipate kodi, kula na kadhalika.MUNGU ANISAMEHE SANA.
Komaa upate kikazi,afu usikae mjini kaa kijijiniTana mbaya zaidi iwe kwamba wewe baba yako kama alikuwepo hamkuwahi kulala njaa
unakuta wewe waweza jikaza ila wife na mtoto wenu kidume usoni ukiwacheki ni dhahiri kabisa njaa imewanyoosha si kidogo.
unamwaga machozi usiku kimyakimya ili kulinda brand, asubuhi unaamka 12 kamili kucheki vibarua vya kubeba zege (hapo una degree au diploma ya chuo). unazunguka weeee hadi saa sita ni bila bila! mwili unatetemeka balaaa,
wife ak=nanitumia sms kuwa kakopa chapati 6 kwenye mgahawa uende ule ushushie na maji usije nikazimia mbele za watu.
Mbona hata sisi walinzi tupo mkuu. Usichoke mkuu muombe Mungu huku ukizidi kupambana mambo yatakua sawa tu.Ila tatizo ni kwamba humu jamiiforums karibu kila mtu ana degree, niashara inayomlipa / kazi ya maana, nyumba na gari....
kweli, kijijin huwezi kulala njaaKomaa upate kikazi,afu usikae mjini kaa kijijini
Wanawake wengine wajanja, wakiona Maisha magumu, wanazoea nyumba zenye unafuu ukifika pale unasaidia kazikazi, wakipika chakula unakula na mtoto, kama kunachochote kitu unapewa unaondoka jioni, mi nimewakuta Sana home watu wa dizaini hii.Tana mbaya zaidi iwe kwamba wewe baba yako kama alikuwepo hamkuwahi kulala njaa
unakuta wewe waweza jikaza ila wife na mtoto wenu kidume usoni ukiwacheki ni dhahiri kabisa njaa imewanyoosha si kidogo.
unamwaga machozi usiku kimyakimya ili kulinda brand, asubuhi unaamka 12 kamili kucheki vibarua vya kubeba zege (hapo una degree au diploma ya chuo). unazunguka weeee hadi saa sita ni bila bila! mwili unatetemeka balaaa,
wife ak=nanitumia sms kuwa kakopa chapati 6 kwenye mgahawa uende ule ushushie na maji usije nikazimia mbele za watu.
>> source B]
Wife ana akili kuliko wewe.Tena mbaya zaidi iwe kwamba wewe baba yako kama alikuwepo hamkuwahi kulala njaa.
Unakuta wewe waweza jikaza ila wife na mtoto wenu kidume usoni ukiwacheki ni dhahiri kabisa njaa imewanyoosha si kidogo.
Unamwaga machozi usiku kimyakimya ili kulinda brand, asubuhi unaamka 12 kamili kucheki vibarua vya kubeba zege (hapo una degree au diploma ya chuo), unazunguka weeee hadi saa sita ni bila bila, mwili unatetemeka balaaa.
Wife akanitumia sms kuwa kakopa chapati 6 kwenye mgahawa uende ule ushushie na maji usije nikazimia mbele za watu.
Soma pia: Umaskini uusikie tu, Kipindi ukiwa ama kwa sasa ukiwa bado katika hali ya umasikini, ni changamoto zipi umepitia
Uko sahihi sana yani hata siwaelewagiIla tatizo ni kwamba humu jamiiforums karibu kila mtu ana degree, niashara inayomlipa / kazi ya maana, nyumba na gari....
Umeyaiga haya? Au ndio mwenye shida atajiju.Hata mimi naamini hivyo. Hii dunia haikuwa mahala pake.
Yule jamaa alikuwa na roho ya kipekee. Hakusubiri kuombwa.
Hii story yangu ni cha mtoto, baada ya mauti yake waliibuka wengi mno. Kuna aliowapa hifadhi ya makazi, aliowapa mitaji na hata aliolipia ada za watoto wao.
Kuna binadamu Mungu aliwaumba waje kuwa mfano wa wema tu kwa binadamu halafu waondoke.
Ulitakiwa umwambie kwanini bado upo duniani.Hii comment yako imenikumbusha mbali sana.
Kipindi cha mapito magumu nilikutana na ndugu kabisa wa mzee wangu. Nikamwambia hali halisi ya maisha.
Yule mzee alinijibu unakosaje hata mlo mmoja, huoni unajaza dunia tu si bora ungekufa na baba yako tu.
Hii kauli iliniliza kama mtoto mdogo.
Ila Mungu si wa mmoja, hivi karibuni tu kulipitishwa mchango wa kifamilia, mzee kashikwa na tezi dume analia kama mtoto. Watoto wake hakuna hata mmoja mwenye muelekeo.
Nilistopisha ule mchango na nikasimamia operation yake mpaka kutoka kwake hospitali.
Yule mzee anajifanya kasahau kila kitu ila najua nafsi yake inamsuta kila akiniona.