Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

Hii inaweza kuwasaidia

Kwa hustler yeyote ukiingia kwenye mji au nchi yoyote ambao ww ni mgeni huna pa kufikia wala hujui utapata wapi kibarua, cha kufanya uliza mwenyeji yeyote akuelekeze mahali Soko kubwa la mji lilipo.

Amini nakwambia hutolala njaa pindi ukifika sokoni na hutakosa kazi ya kufanya hata kubeba mzigo utabeba na pesa utapata.

Why Sokoni na si mahala pengine? Sokoni ndio sehemu ambapo kuna mzunguko mkubwa wa pesa katika mji au kitongoji husika. Baada ya hapo sasa utaweza kuangalia ufanyaje ili utoke kimaisha.

Sehemu nyingine ambayo inaweza kukuokoa ni Migahawani au Hotelini. Hii sehemu inaweza kukuokoa usilale na njaa na pia unaweza kupata ujira mdogo. Ukifika maeneo hayo omba kazi ya kufanya usafi na hata kuosha vyombo. Hii itakusaidia sana kupata ujira mdogo na chakula pia.

Mwisho kabisa ni nyumba za ibada iwe msikitini au kanisani. Huku kunaweza kukupa fursa ya kukutana na watu wenye hofu na kumjua Mungu hivyo ni mara chache sana kwa wewe mgeni kukosa hifadhi au chakula, na ukiwa nao vizuri unaweza ukapatiwa connection ya kazi.

Kikubwa ukifika sehemu yoyote jiepushe sana kuomba Fedha bali omba kibarua /kazi ,hii itakuwezesha upate pesa ya kujikimu na vilevile kukuepusha dhidi ya fedheha na udhalili wa kuombaomba. Kumbuka mwanadamu hapendi kuombwa pesa.

Katika kutafuta pesa epuka kitu kinachoitwa kuona aibu, watu watakuchukuliaje nk. Mwanaume hachagui kazi as long as kazi hiyo ni ya halali na haimuondolei utu wake
 
Umasikini acheni nyie wazee unauma sana ,nikifikiria enzi nasoma form two mama kapanga chumba kimoja nakaka tumerudi likizo tunalala na mama yetu mzazi humohumo,nabibi humohumo namdogo wetu humohumo...achane nyie wazeee...vijana wakiume kulala chumba kimoja namzazi wakike kisa kukosa getho sio poa akili itakukaa sawa tu nalazima kama unajitambua ukakaze msuli ,nikupitia hali hyo iliyotufanya sote )mm nakaka kujituma kwakiwango cha rami hadi sasa tu namiliki nyumba ya vyumba kumi,nahata hatuishi hapo nyumbani tunajitegema kila mmoja.ufukara unakufnaya akili ikae sawa.
 
Mama yangu alikuwa mpika na muuza gongo kule Gongo la mboto mapolisi waliweka informer kila tukiwa tunaenda kupiga gongo wanakuja wanamkamata mama analia tukiwa mapolini kule kinyerezi(enzi hizo kinyerezi kulikuwa pori la kukamata hadi sungura na digi digi kabisa) sasa mama alikamatwa mfuluzo mbaya zaidi wakati mahita anatawazwa kuwa IGP si akapitisha opereshen maalum ambayo mama akabebwa na ma pipa na mtambo wa gongo mpaka kituoni akatuacha mimi na wadogo zangu watatu.Mimi niliachwa kwa sababu ni mdogo ikabidi mimi nikabidhiwe jezi na mchezo sijauelewa hivyo nikajikuta nina majukumu ya kulisha wadogo zangu na kumtafutia mama chakula ili ale kule lock up kwa sababu ndugu tulikuwa nao wachache pale Dar ambao kama vile walitutenga kwa sababu ya umasikini.Dingi ameshasepaga muda kakimbia familia sababu ni hiyo hiyo umasikini.
Ikanibidi niwe naenda matembezini na kiroba kwapani huko kutafuta mashamba ya watu mfano wa mashamba nilikuwa nayaonea ni ya miogo na viazi na minazi na mapera kule ulongoni enzi hizo hata TANESCO hawajaweka umeme hata nyumba moja.
Huwezi amini nilijua hadi kupandia minazi ili niibe madafu usiku anyway tu cut the story nilikuwa naondoka na kiroba kitupu nawaacha madogolas wamejikunyata nikirudi wanabidi wapokeee chochote ntachokuja nacho kwenye kiroba kuna siku nilikimbizwa na mwenye shamba ambae lilikuwa na miogo mitamu kumbe aliweka lindo baada ya kuona katikati ya shamba lake nimelaza mashina yote aisee.
KUMBE kitendo cha kuwa namletea miogo kila siku maza mapolisi wakawa wananichora na kunidiscuss siku moja nilikosa miogo nikapeleka madafu mawili mama aliachiwa tuongee nae nje ya kituo si akaanza kulia na kuniambukiza kilio na mimi kumbe ile ilikuwa pona yake si mkuu wa kituo akazipata zile habari maana kumbe watu wanapewa dhamana mimi sijui taratibu wakaniuliza eti kesho nije na mkubwa tumdhamini kwa vile ndugu walishatutenga ikabidi nikamchukue MAMA SALAWALA(sijui yupo wapi) ambae huwa tunamuuziaga gongo anaishi mzambarauni Gongo la mboto.
Mama akatoka mtaji ukawa umefilisiwa maana walibeba mtambo wa gongo na mapipa yote ikabidi mama awe raia mwema akaanza kuazima shamba tukawa tunalima huku tunashindia maembe
Anyway njaa ni noma inakosesha hadi ladha ya maisha
Sitaki kueleza mengi at the end nikafaulu mtaa mzima kwenda shule ya AZABOY nikaona shida zinazidi nyumbani hata nauli nikakosa ikabidi niende kujipendekeza kwa madogo wa dogo dogo center Mabibo karibia na shule ya loyola walipangishiwa nyumba na wadhamini wao wazungu.
Story ni ndefu ila acheni nijiite Billie humu JF kwa sababu hata mama yangu kwa sasa nimuanzishia biashara anaishi kwenye nyumba nzuri na kuna flame za kupangisha 8 na ana nyumba za wapangaji 5.
Upande wa mimi now nilivyo sitaki kusema ila nipo na familia ambayo watoto kula mpaka uwashikie fimbo au uwawekee katuni na almost kila kitu ndani hadi vyakula vinaharibika.SIJITAPI NAONGEA UKWELI TUPU NIMEJIFUNZA SHIDA NI ELIMU NZURI SANA KAMA UKIWEZA KUZITOROKA.
Touching story,
MUNGU amekua mwema sana kwako stay blessed 🙏❤️
 
Hii inaweza kuwasaidia

Kwa hustler yeyote ukiingia kwenye mji au nchi yoyote ambao ww ni mgeni huna pa kufikia wala hujui utapata wapi kibarua, cha kufanya uliza mwenyeji yeyote akuelekeze mahali Soko kubwa la mji lilipo.

Amini nakwambia hutolala njaa pindi ukifika sokoni na hutakosa kazi ya kufanya hata kubeba mzigo utabeba na pesa utapata.

Why Sokoni na si mahala pengine? Sokoni ndio sehemu ambapo kuna mzunguko mkubwa wa pesa katika mji au kitongoji husika. Baada ya hapo sasa utaweza kuangalia ufanyaje ili utoke kimaisha.

Sehemu nyingine ambayo inaweza kukuokoa ni Migahawani au Hotelini. Hii sehemu inaweza kukuokoa usilale na njaa na pia unaweza kupata ujira mdogo. Ukifika maeneo hayo omba kazi ya kufanya usafi na hata kuosha vyombo. Hii itakusaidia sana kupata ujira mdogo na chakula pia.

Mwisho kabisa ni nyumba za ibada iwe msikitini au kanisani. Huku kunaweza kukupa fursa ya kukutana na watu wenye hofu na kumjua Mungu hivyo ni mara chache sana kwa wewe mgeni kukosa hifadhi au chakula, na ukiwa nao vizuri unaweza ukapatiwa connection ya kazi.

Kikubwa ukifika sehemu yoyote jiepushe sana kuomba Fedha bali omba kibarua /kazi ,hii itakuwezesha upate pesa ya kujikimu na vilevile kukuepusha dhidi ya fedheha na udhalili wa kuombaomba. Kumbuka mwanadamu hapendi kuombwa pesa.

Katika kutafuta pesa epuka kitu kinachoitwa kuona aibu, watu watakuchukuliaje nk. Mwanaume hachagui kazi as long as kazi hiyo ni ya halali na haimuondolei utu wake.
Nyumba za ibada unaweza ukafia humo labda msikitini ila hizi mbwa nyingine zimejiandaa kupokea tu wala sio kutoa
 
Daaaah acheni mikasa ni mingi lakn nakumbuka tu wakat nimeenda kuripoti chuo,,hela ya kuungaunga ile usajili ikakataa sikua hata mia,,,nilikaa siku mbili bila kula hadi vidonda vilitoka kooni aiseeee haya maisha. Lkn hali ile ilinitia uchungi nilijiapiza Mungu akiendelea kunijaalia uhai iwe mvua iwe jua kamwe wanangu wasije kupitia yale maisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna kipindi nilipitia SONONA kuu katika maisha YANGU........

In that situation nilipoteza Kila kitu muhimu nilicho kipambania katika maisha yangu...............

Nili lose appetite kwenye Kila kitu kiasi Cha kukaa siku tatu bila kula chochote na huisi NJAA.............

Siku ya nne jion nikasema Nile japo kidogo maana nili Anza hisi NJAA nyumbani issues za misosi haikuwa shida....

Nikapakua sahani kubwa wali sato na mboga mboga na mchuzi wa kutosha lile tonge la kwanza lilitosha kunichana chana kama wembe kuanzia mdomoni, kwenye koo mpka kwenye utumbo......

Nilishindwa kukila kile chakula zaidi ya kukitazama na kutamani lakini nilikua nimechanika vibaya.....

Kwa muda wa siku tatu zingine nili ishi Kwa juice,uji na mtori tena ulipita Kwa maumivu mengi baada ya kipona madonda ya mdomoni kwenye koo mpka kwenye utumbo nikawa very strong linapo kuja swala la uvumilivu wa NJAA
 
Nilichojifunza ukiwa na hela njaa ikija inakupiga chabo inaamsha zake inaona kabisa jamaa hatishiki, yaan unaweza shinda siku nzima bila kula na njaa huhisi.

Kivumbi miaka hiyo unaamka hujui utakula nini, inafika jion unamtembelea msela geto angalau upige story uambulie nae haweki msosi mezani, unaamua kuangalia movie moaka unasinzia msela anaamka anakula akizan uko fofofo unajikaza ale amalize bila kuamka ili usimkate stimu, akimaliza kula unaamka unasepa, unafika geto unakunywa maji unalala, usingizi hauji. Panakucha unaamua ukapambane kitaa unaambulia patupu. Kila dili ikija inakurika aisee unaona hapa hapanifai.
Unajitafuta unajipata wale wale wanaanza kutangaza unaringa, unajivuna sana, jamani mbona wakati wa msoto hamkusema nateseka nasota sana.
Ni bora ninunue sigara japo sivuti nizituoe lakini kuna watu siwezi kuwasaidia hata wapigane na nyoka ntakaa upande wa nyoka.
 
Akikujibu niambie.

Huyo mke ninaye mpka leo.
I love her and she loves me.

Na sasa nimemfungulia shule ya wanafunzi wa awali ana wanafunzi zaidi ya 200 sasa. kila mwanafunzi analipa ada 480,000 kwa mwaka.
na mimi nina kazi nzuri tu Mgodini hapa Kahama

Uvumilivu wake ndo umeleta matunda mpka leo kwa kunitia nguvu na kujiona kuwa its possible

“As long as your breathing, Never give up”

Fight to the last drop of blood in your veins!!!!
 
Nilichojifunza ukiwa na hela njaa ikija inakupiga chabo inaamsha zake inaona kabisa jamaa hatishiki, yaan unaweza shinda siku nzima bila kula na njaa huhisi.

Kivumbi miaka hiyo unaamka hujui utakula nini, inafika jion unamtembelea msela geto angalau upige story uambulie nae haweki msosi mezani, unaamua kuangalia movie moaka unasinzia msela anaamka anakula akizan uko fofofo unajikaza ale amalize bila kuamka ili usimkate stimu, akimaliza kula unaamka unasepa, unafika geto unakunywa maji unalala, usingizi hauji. Panakucha unaamua ukapambane kitaa unaambulia patupu. Kila dili ikija inakurika aisee unaona hapa hapanifai.
Unajitafuta unajipata wale wale wanaanza kutangaza unaringa, unajivuna sana, jamani mbona wakati wa msoto hamkusema nateseka nasota sana.
Ni bora ninunue sigara japo sivuti nizituoe lakini kuna watu siwezi kuwasaidia hata wapigane na nyoka ntakaa upande wa nyoka.
Huu Uzi utachukua nyota 5 thanks mkuu Tupo hapa kujifunza......
 
Hata mimi naamini hivyo. Hii dunia haikuwa mahala pake.

Yule jamaa alikuwa na roho ya kipekee. Hakusubiri kuombwa.

Hii story yangu ni cha mtoto, baada ya mauti yake waliibuka wengi mno. Kuna aliowapa hifadhi ya makazi, aliowapa mitaji na hata aliolipia ada za watoto wao.

Kuna binadamu Mungu aliwaumba waje kuwa mfano wa wema tu kwa binadamu halafu waondoke.

Sure
 
Back
Top Bottom