Ni halali Wazanzibari kufanya kazi za Watanganyika?

Ni halali Wazanzibari kufanya kazi za Watanganyika?

Hivi ni halali kwa Wazanzibari kuajiriwa Tanganyika kama waalimu bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi?

Ni halali Wazanzibari kuajiriwa kama watendaji wa mitaa na Kata?

Ni halali kwa Mzanzibari kuteuliwa kuwa Mkuu wa mkoa au wilaya huku Tanganyika?

Ni sawa kwa Mzanzibari kupewa Leseni ya biashara Tanganyika bila kwanza kupewa kibali cha kufanya kazi?

Mzanzibari anaweza kuteuliwa kusimamia wizara zisizo za Muungano?

Ni halali kwa Mzanzibari kugombea nafasi za kisiasa Tanganyika?

Kodi anayotozwa Mzanzibari inatakiwa iende nchini kwao Zanzibar ama itumike Tanganyika?
Mkuu, si halali kwa mujibu wa Wazanzibar lakini ni halali kwa mujibu wa katiba ya mpito ya 1964.
Katiba ya 1964 ilisema mambo yote ya Tanganyika yatakuwa ya muungano
Wazanzibar wanasema mambo ya muungano yalikuwa machache ingawa yameongezwa

Kwa mujibu wa Wazanzibar sehemu zote ulizotaja hapo si za muungano. Hoja yao ni kwamba kwa katiba ya mpito Tanganyika ilivaa koti la Muungano. Kitu cha kushangaza waliojificha ndani ya koti la Muungano ni Wazanzbar ambao hunufaika na mambo yale yale wanayolalamika yameongezwa kama ulivyoyataja

Kuteuliwa, hakuna sheria inayomkataza Mzanzibar asiteuliwe kwasababu nafasi 'X' husema kwa 'Mtanzania'
Hapa Wazanzibar wanavua Uzanzibar wao wanavaa Utanzania. Kwa miaka ya nyuma nafasi fulani za Tanganyika waliteuliwa katika spirit ya muungano lakini hawakupewa uongozi kamili

Kugombea: Again Wazanzibar wanapotaka kugombea wanavua Uzanzibar wao wanavaa Utanzania kwahiyo katiba inaruhusu wateuliwe. Ni kama ilivyo ardhi , elimu ya juu n.k. au usimamizi wa Taasisi za Tanganyika

Kodi: Yes,kuna kodi za muungano zinazopelekwa Zanzibar nje ya ile 4.5% ya pato la Tanganyika.
Tanganyika na Taasisi zake zinatoa ajira nyingi kuliko SMZ, hivyo kupunguza mzigo wa ajira Zanzibar.

Mfano, Zanzibar wanapewa 21% ya ajira za muungano wakiwa watu milioni 1.2 tu.
Ikiwa ajira za muungano ni 100,000 tunaongelea 21,000 mara mbili ya ajira za SMZ takribani 10,000.

Jambo la kushangaza kodi wanazolipa zinapelekwa Zanzibar! Yaani wanapewa ajira za bure za Watanganyika halafu SMZ wanalipwa kwa kupewa ajira hizo na kupunguziwa unemployment!

G55 wakati wa Mwinyi waliona upendeleo na matatizo makubwa. Yamerudi sasa hivi kila kitu Zanzibar hata majaji wa mahakama kuu wanateuliwa kutoka Zanzibar , mawaziri, viongozi wa Taasisi n.k.

Warioba kasema ni mambo 7 tu, mengine kila mtu aangalie utaratibu wake.

Watanganyika endeleeni kutoa hisani! kule Zanzibar Rais Mwinyi kasema ninyi ni sawa na wageni wengine
 
Upumbavu wa viongozi kuikumbatia zanzibar imesababisha maumivu Tanganyika.Tozo zinazobuniwa kila siku zinatokana na matumizi makubwa kama haya ya kuibeba Zanzibar.IPO siku haka kamuungano kakipuuzi tutakavunjilia mbali pale wazalendo tutakaposhika madaraka.Haiwezekani Zanzibar chao ni cha kwao lakini cha Tanganyika ni cha wote
 
Chao chao, chetu chao!

Nyerere huyo kwa ujuaji mwingi aliwauza Watanganyika kwa sababu ya personal ambitions za kutaka kutawala eneo kubwa, na kujionyesha kimataifa kuwa yeye ni "Uniter"

Unachukua 25% ya ajira unawapa watu wasiofika milioni mbili, halafu hata zile 75% zilizobaki bado wana haki ya kuziomba vilevile kwa hoja kuwa ni za watanzania wote bila kubagua mtu katoka wapi.

Haka ka muungano kanaifanya Tanganyika kuwa Kubwa Jinga na Zanzibar kuwa dogo Janja
 
Hivi ni halali kwa Wazanzibari kuajiriwa Tanganyika kama waalimu bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi?

Ni halali Wazanzibari kuajiriwa kama watendaji wa mitaa na Kata?

Ni halali kwa Mzanzibari kuteuliwa kuwa Mkuu wa mkoa au wilaya huku Tanganyika?

Ni sawa kwa Mzanzibari kupewa Leseni ya biashara Tanganyika bila kwanza kupewa kibali cha kufanya kazi?

Mzanzibari anaweza kuteuliwa kusimamia wizara zisizo za Muungano?

Ni halali kwa Mzanzibari kugombea nafasi za kisiasa Tanganyika?

Kodi anayotozwa Mzanzibari inatakiwa iende nchini kwao Zanzibar ama itumike Tanganyika?
Tatizo wapumbavu hawataki kuamini kuwa ccm ni mafii...tatizo la muungano linaanzia kwa nyerere kujidandanya kuwa muungano wa nchi na nchi ndiyo msingi wa waendeleo kwa bara la africa ,huo ulikuwa ujinga mkubwa sana ukweli kinacho sababisha maendeleo baina ya nchi na nchi ni ushirikiano mzuri na madhubuti ulio chini ya haki yote
 
Hivi ni halali kwa Wazanzibari kuajiriwa Tanganyika kama waalimu bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi?

Ni halali Wazanzibari kuajiriwa kama watendaji wa mitaa na Kata?

Ni halali kwa Mzanzibari kuteuliwa kuwa Mkuu wa mkoa au wilaya huku Tanganyika?

Ni sawa kwa Mzanzibari kupewa Leseni ya biashara Tanganyika bila kwanza kupewa kibali cha kufanya kazi?

Mzanzibari anaweza kuteuliwa kusimamia wizara zisizo za Muungano?

Ni halali kwa Mzanzibari kugombea nafasi za kisiasa Tanganyika?

Kodi anayotozwa Mzanzibari inatakiwa iende nchini kwao Zanzibar ama itumike Tanganyika?
Mkuu Allen Kilewella , kwanza kazi ni kazi, hakuna kazi ya mtu, hivyo hakuna kazi za Mtanzania wala kazi ya Mzamzobari, kazi ni ya wote. Pili hiki ulichokileta ni ubaguzi wa kutaka kuwabagua Wazanzibari!. Mwalimu Nyerere alisema hii ni dhambi!. Kiukweli somo la uraia linahitajika sana Tanzania kwa watu kama wewe!. Tanzania ni nchi moja, ya JMT, yenye uraia mmoja tuu wa Tanzania, kila Mtanzania ana haki sawa na haki zote za raia wa Tanzania.

Ndani ya uraia wa Tanzania kuna uraia mmoja tuu wa Mtanzania.

Kwa vile Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndani ya JMT kuna sehemu moja ya Zanzibar ina utawala wake wa ndani ambao Wazanzibari licha ya kwanza kuwa ni raia wa JMT wenye haki zote za uraia wa JMT, hawa wamepewa haki za ziada za ukaazi wa Zanzibar. Kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar sio kitambulisho cha uraia, hakuna uraia wa Zanzibar kuna uraia mmoja tuu wa JMT na ziada ya ukaazi wa Zanzibar.

Hivyo Wanzanzibari wana haki zote za uraia wa Tanzania na ziada ya haki za ikaazi wa Zanzibar.

Lile jambo langu likitimia, nafungua darasa la bure la Haki, kuwaelimisha Watanzania haki zao mbalimbali zikiwemo haki za uraia.
P
 
Hivi ni halali kwa Wazanzibari kuajiriwa Tanganyika kama waalimu bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi?

Ni halali Wazanzibari kuajiriwa kama watendaji wa mitaa na Kata?

Ni halali kwa Mzanzibari kuteuliwa kuwa Mkuu wa mkoa au wilaya huku Tanganyika?

Ni sawa kwa Mzanzibari kupewa Leseni ya biashara Tanganyika bila kwanza kupewa kibali cha kufanya kazi?

Mzanzibari anaweza kuteuliwa kusimamia wizara zisizo za Muungano?

Ni halali kwa Mzanzibari kugombea nafasi za kisiasa Tanganyika?

Kodi anayotozwa Mzanzibari inatakiwa iende nchini kwao Zanzibar ama itumike Tanganyika?
Suala la msingi hapa ni ,Jee ? Ni halali Tanganyika kulazimisha Muungano na Zanzibar?
 
Hivi ni halali kwa Wazanzibari kuajiriwa Tanganyika kama waalimu bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi?

Ni halali Wazanzibari kuajiriwa kama watendaji wa mitaa na Kata?

Ni halali kwa Mzanzibari kuteuliwa kuwa Mkuu wa mkoa au wilaya huku Tanganyika?

Ni sawa kwa Mzanzibari kupewa Leseni ya biashara Tanganyika bila kwanza kupewa kibali cha kufanya kazi?

Mzanzibari anaweza kuteuliwa kusimamia wizara zisizo za Muungano?

Ni halali kwa Mzanzibari kugombea nafasi za kisiasa Tanganyika?

Kodi anayotozwa Mzanzibari inatakiwa iende nchini kwao Zanzibar ama itumike Tanganyika?
Muundo wa muungano utazamwe upya ili kuondoa hii mikanganyiko iliyopo.
Kalamu Nguruvi3 zitto junior JokaKuu brazaj
 
2025 ni karibu sana kiuchaguzi ikiwa kutakuwa na mipango husika ya kuelekea huko, binafsi nakataa kata kata kuongozwa na mzanzibar ikiwa chama chochote cha siasa kitamteua kugombea, nitaunga upande mwingine. Narudia kwa mara nyingine, Raisi aliyepo ametokana na katiba ya nchi na watanzania temeheshimu hilo,tusubili 2025 kuona nini kitatokea.
 
Mkuu Allen Kilewella , kwanza hiki ulichokileta ni ubaguzi wa kutaka kuwabagua Wazanzibari!. Mwalimu Nyerere alisema hii ni dhambi!. Kiukweli somo la uraia linahitajika sana Tanzania kwa watu kama wewe!. Tanzania ni nchi moja, ya JMT, yenye uraia mmoja tuu wa Tanzania, kila Mtanzania ana haki sawa na haki zote za raia wa Tanzania.

Ndani ya uraia wa Tanzania kuna uraia mmoja tuu wa Mtanzania.

Kwa vile Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndani ya JMT kuna sehemu moja ya Zanzibar ina utawala wake wa ndani ambao Wazanzibari licha ya kwanza kuwa ni raia wa JMT wenye haki zote za uraia wa JMT, hawa wamepewa haki za ziada za ukaazi wa Zanzibar. Kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar sio kitambulisho cha uraia, hakuna uraia wa Zanzibar kuna uraia mmoja tuu wa JMT na ziada ya ukaazi wa Zanzibar.

Hivyo Wanzanzibari wana haki zote za uraia wa Tanzania na ziada ya haki za ikaazi wa Zanzibar.

Lile jambo langu likitimia, nafungua darasa la bure la Haki, kuwaelimisha Watanzania haki zao mbalimbali zikiwemo haki za uraia.
P
Hawa watu wanavitambulisho vya uzanzibar na hata kwenye mambo mengine vinatumika kuwabagua wabara, kingine Hawa watu wanaminywa vichwa kuleta utofauti Kati ya watu wa visiwani na watu wa bara. Ukienda tu na chogo wanajua huyu mtanganyika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ndio hoja ya msingi ya serikali tatu, rais wa muungano na wa Zanzibar wote ni wazanzibari, nani anatetea maslahi ya Bara ndani ya Muungano? Bara inaporwa tu hakuna wa kuitetea, waliopigania Uhuru wa Tanganyika wanadhihakiwa mno
Yaani hao top ni matatizo tupu.

Rais wa JMT ni Mzanzibar.

Makamu kwakweli hana influence yeyote ya kisiasa.

PM naye haeleweki.

Tanganyika imebakia Yatima inapigwa front and behind , right ,left and center hakuna wa kuitetea.

Ndio maana kila kitu ni ghali na hakuna anayejali.

Maisha mtaani ni magumu mara dufu. Hao ambao wana jiweza hawawakumbuki kabisa wasiojiweza.
 
Back
Top Bottom