Ni ipi siri ya Wachaga kuwa kabila lililoyaacha makabila mengine mbali mno kwenye mafanikio?

Ni ipi siri ya Wachaga kuwa kabila lililoyaacha makabila mengine mbali mno kwenye mafanikio?

1.Elimu: Hawa watu wamesoma sana na karibia kila sekta wapo na wanasaidiana sana.

2.Ushirikiano: Hapa siongei sana naamini hili ndilo kabila linaloongoza kwa kushirikiano, yaani wanaweza somesha mtoto wa ndugu yao asiye na uwezo na mwishowe wakamtafutia kazi nzuri au connection. Yaani mchaga akifanikiwa kwenye familia basi ujue ndugu zake wengi pia watafanikiwa tofauti mno na ndugu zetu wa Singida mtu anapata cheo badala awape ndugu zake connection au awapeleke shule anataka awe juu yeye tu na simu akipigiwa hapokei hii tabia ya ovyo sana na hata kwao wengi wao huwa hawajengi.

3.Mazingira: Kule kwao mazingira yanachangamoto fulani hivi, kumbuka sehemu kubwa ni mlima hivyo hata miundombinu sio mizuri sana hasa kipindi cha mvua na fursa ni chache, yaani ukiwa kule unaweza kuhisi uko porini lakini cha ajabu kuna mijengo ya hatari, sasa mvua ikinyesha unaweza kuwa na gari au pikipiki usione faida yake hivyo usafiri unabaki kuwa miguu tu na unaweza tembea umbali mrefu tu kufuata huduma au kufika nyumbani. Hii imechangia wengi kutafuta maisha sehemu zingine na huwa hawana utani wanapozikuta na hata wasipozikuta wanajitahidi kuzitengeneza.

4. Roho nzuri: Wachaga hasa wa Rombo hawa watu wana roho nzuri sana ni tofauti na makabila mengine yaani unakuta watu wana hasira hasira tu na roho mbaya.

5.Imani: Hawa jamaa wana imani sana, hapa sizungumzii kwenda ka isani au kwenda msikitini maana kama ni kwenda kanisani na kusali, Mbeya ndio vinara.

6. Wanaheshimu mila na desturi zao: kifupi wanajua wapi wametoka na wapi wanaenda. Hapa sitozungumza sana.
 
1.Elimu: Hawa watu wamesoma sana na karibia kila sekta wapo na wanasaidiana sana.

2.Ushirikiano: Hapa siongei sana naamini hili ndilo kabila linaloongoza kwa kushirikiano, yaani wanaweza somesha mtoto wa ndugu yao asiye na uwezo na mwishowe wakamtafutia kazi nzuri au connection. Yaani mchaga akifanikiwa kwenye familia basi ujue ndugu zake wengi pia watafanikiwa tofauti mno na ndugu zetu wa Singida mtu anapata cheo badala awape ndugu zake connection au awapeleke shule anataka awe juu yeye tu na simu akipigiwa hapokei hii tabia ya ovyo sana na hata kwao wengi wao huwa hawajengi.

3.Mazingira: Kule kwao mazingira yanachangamoto fulani hivi, kumbuka sehemu kubwa ni mlima hivyo hata miundombinu sio mizuri sana hasa kipindi cha mvua na fursa ni chache, yaani ukiwa kule unaweza kuhisi uko porini lakini cha ajabu kuna mijengo ya hatari, sasa mvua ikinyesha unaweza kuwa na gari au pikipiki usione faida yake hivyo usafiri unabaki kuwa miguu tu na unaweza tembea umbali mrefu tu kufuata huduma au kufika nyumbani. Hii imechangia wengi kutafuta maisha sehemu zingine na huwa hawana utani wanapozikuta na hata wasipozikuta wanajitahidi kuzitengeneza.

4. Roho nzuri: Wachaga hasa wa Rombo hawa watu wana roho nzuri sana ni tofauti na makabila mengine yaani unakuta watu wana hasira hasira tu na roho mbaya.

5.Imani: Hawa jamaa wana imani sana, hapa sizungumzii kwenda ka isani au kwenda msikitini maana kama ni kwenda kanisani na kusali, Mbeya ndio vinara.

6. Wanaheshimu mila na desturi zao: kifupi wanajua wapi wametoka na wapi wanaenda. Hapa sitozungumza sana.
Ongezea na kutoyapa kipaumbele mambo ya kichawi, kuna rafiki yangu wa Geita huko mpaka leo wazazi wake hawataki kabisa habari ya kujengewa nyumba ya kisasa wanaogopa watarogwa na majirani
 
Licha ya umasikini wetu wa taifa hapakosekani kundi la watu wenye nafuu, Tukigusia makabila yenye asili ya hapa kwetu, jamaa wapo mbali mno.

Kunaweza kuwa na makabila yanayowafatia ila ni gepu refu mno.

1.Elimu: Hawa watu wamesoma sana na shule zipo huko kwao tangu zamani sana, sehem zao kuna shule nyingi sana, hapa wenzao ni wahaya lakini tatizo wahaya wana shule chache sana huko kwao na sehemu waliyosifika ni kwenye elimu tu.

Biashara - Ni kama kipaji chao cha asili hata kwa ambao wameishia darasa la 7 wapo wanaofanya makubwa, ukija kwa wasomi nako wamejaa wamefungua makampuni, najua kuna wanaofatia wapo wakinga, waha, wasukuma, n.k ila wameachwa mbali sana.

siasa - ukiachana na ccm hawa ndio waasisi wakubwa wa vyama vingi maarufu vya upinzani kuanzia tlp, nccr, chadema, vyote vina asili ya wachaga,

kuendeleza na kujenga kwao hawana mpinzani, nimeona makabila mengine wengine wanajaribu jaribu wanajenga nyumba za kisasa huko vijijini kwao ila unakuta kijiji kizima nyumba hizo zinahesabika,

Kwenye system na political positions hawajajaa sana
ila kila ofisi wamejaa, mashirika ya uma na kimataifa wapo.

Ni nadra sana kusikia mambo ya uchawi uchagani kwamba flani kamtupia jini jirani kisa mtoto wake kapata kazi, kurogana kisa ndugu kapiga hatua, n.k. uchawi ni adui mkubwa sana wa maendeleo na kwa kiasi kikubwa wamejitahidi kuukwepa, just imagine nina rafiki yangu wa huko Geita alitaka kuwajengea wazazi nyumba ya kisasa, watakataa kabisa kwasababu eti majirani wataona wivu wanaogopa kurogwa.

Wanaheshimu mila na desturi zao: kifupi wanajua wapi wametoka na wapi wanaenda, wachaga ikifika december kuna mtu asiejua balaa lao ? huwa ni kama waisrael wa sehem mbali mbali wanarudi kwao, hii pia inafanyika na kabila lililofanikiwa zaidi Nigeria waigbo hurudi kwao kila mwisho wa mwaka.
..........................

Kwa wengi unaweza kukuta kwenye elimu wapo ila kwengine zero

wengine unaweza kuta wanajitahidi biashara ila huko kwao hakutamaniki na elim bado sana

n.k.
Haya mawasilisho yako ni kwa mujibu wa tafiti gani na iliyofanyika mwaka gani?
 
Ongezea na kutoyapa kipaumbele mambo ya kichawi, kuna rafiki yangu wa Geita huko mpaka leo wazazi wake hawataki kabisa habari ya kujengewa nyumba ya kisasa wanaogopa watarogwa na majirani
Geita ya wapi hiyo unaizungumzia? Nyimba nzuri kila kona kwenye vijiji vya Geita huwa huzioni? Mnapenda sifa za kijinga sana!
 
ENEO PEKEE WALILOSHINDWA KUFANIKIWA, NI KWENYE NDOA.

NDOA ZAO HAZIDUMU KABISAA.

MAENEO MENGINE WAKO VIZURI
Ukiitafuta sn hela mapenzi ni gharama na yanaharibu ubongo bila mafanikio chanya. ..km unaelewa what I mean. ..hivyo iliuwekeze nakuchanganua mbinu za kupata hela mapenzi weka pembeni. ..u gonna win
 
Wachaga acheni kujipigia promo. Wazanaki tupo juu zaidi yenu.
Wazanaki wapo juu, nafasi yenu bado ipo katika historia ya nchi hii, Nyerere aliweka taifa mbele na sio watu wake, hata watoto wake hakuwapa upendeleo

wazanaki wengi wana hali za kawaida tu na hapa ndipo tunaamini Nyerere hakuwa na upendeleo.
 
Imeandikwa: “ laana isiyo na sababu haimpati mtu “
62a01ce5cef754dd1dd774814e2209d7.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lengo langu nipate mke anaeweza kupambana na maisha ili tufike mbali zaidi sasa sijui wapi wako hao wanawake ukiondoa wachaga
WAKATI WEWE UNAWAZA MTU WA KUSAIDIANA NAYE MAISHA.
MWENZIO ANAWAZA KIPATO CHAKE NI CHAKE YEYE, YEYE TU.

MALEZI NA MAKUZI YAO YAWE WAANDA KUWA WANAUME WA KIKE.
HAO HAWANA HAIBA ZA KIKE, HUWEZI KUTA WANAONGEA KWA UPOLE, UNYENYEKEVU, UTII, KUJISHUSHA.
ZAIDI NI WATU WA MASHINDANO, KUPENDA KUTAWALA (HASA KAMA MUME SIO WA KABILA YAO), KIBURI, JEURI, DHARAU, UBABE UBABE.
 
Wachaga wako kama wahindi, wanaharibu watoto wao, utakuta mmoja dishi limeyumba huwezi kumjua kirahisi...

Huyo ndio anawapa utajiri...

Kingine ni watu wa kafara za damu za wanyama kwa wafu/mizimu...
Wewe una uelewa mdogo sana juu ya hili kabila. Pia yawezekana umejazwa propaganda na chuki dhidi ya hili kabila. Ungekuwa na mtoto binti ningeanza kumtafuta akuletee mjukuu wa kichaga ili akusaidie kupunguza chuki zako kwa wachaga.
 
Back
Top Bottom