Ni kheri ufiwe na mzazi kuliko kufiwa na mume/mke

Ni kheri ufiwe na mzazi kuliko kufiwa na mume/mke

Tatizo lako ni yale maagano ya kuungana na kuwa mwili mmoja, utabakije nusu mwili? Hivyo mme au mke ni muhimu zaidi.
 
Pole sana Mkuu, kama una nafasi ya kubadilisha mazingira fanya hivyo nyumba kodisha. Inaweza kukusaidia kuanza upya sasa hivi ni ngumu sababu nyumba ni ile ile, ndugu ni wale wale na wapo pale pale, marafiki ni wale wale. So kila utachofanya taswira ya mwenzio lazima ije, badili mazingira ukiweza!!

NB: Wanao ndiyo wanaona umuhimu wa mzazi ila wewe unaona umuhimu wa mke. Huoni umuhimu wa wazazi sababu ulishajitegemea
Kweli kabisaa ila ni depression anayopitia inamfanya aseme huo ujingaa ila mzazi anaumaa hata kama iwe unajitegemea kimaishaa.
 
Pole sana mkuu sio rahisi kukuelewa mimi nina ya tofauti nina umri wa 33 nimeshafiwa na watoto wawil;i asikuambie mtu hayo maumivu yake sio ya kuhadidhia, nlikuja gundua kumbe ndio maana mzee anafiwa na ,mwanae mwenye wajukuu bado analia uchungu hauelezeki. NB WAMEZALIWA WAKAISHI SIO MIMBA KUHARIBIKA mwenyenzi mungu alawalaze mahala pema peponi.
Pole sana mkuu...!
 
Maumivu ya kuondokewa na mzazi hayapimiki aisee, binafsi yananitafuna ndani kwa ndani, sijawahi kupata relief.
Mama yangu haipiti siku sijamuwazaaa..[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24] Hapana aiseee kifo kitu kibayaa sanaa
 
Mkuu mkuu usikufuru kama hauoni umuhimu wa mzazi potezea na sio kuanza kumuombea kifo kisa mtu uliyekutana nae ukubwani. Mzazi ana umuhimu wake na mke,mume ana umuhimu wake pia. Jambo usilolijua au kulifahamu asilimia kubwa ya wanawake wapo tayari kumpoteza Mume na sio mtoto au mzazi wazazi wake.

Pole kwa msiba
Umemaliza.
 
Haya ndo matatizo ya kuwa na mke mmoja, ungekuwa na mke wa pili au hata mchepuko huenda usingeathirika kwa kiwango kikubwa.

Wazungu wametuharibia sana na tamaduni zao za mke mmoja kuja kuzipandikiza kwetu kupitia dini na kupitia sheria za ndoa.

Wanaume wajue kwamba wao wanaathirika zaidi kumpoteza mwenza kuliko wanawake wanavyoathirika kumpoteza mme.

Kwa hiyo tamaduni zetu zilitoa mwanya wa mwanaume kujilinda na hali hiyo kwa kuwa na mke zaidi ya mmoja na hata itakapotokea mke ni mjamzito au ni mgonjwa bado mwanaume hawezi kuathirika kwani mke mwingine yupo.

Haya tuendelee kufuata mambo ya kizungu, imagine huyu mtu mwaka wa nne bado ameshindwa kukaa sawa.​
 
Vaa viatu vya watoto wako mkuu, waambie ni heri wao wamefiwa na mama yao kuliko wewe uliyefiwa na mke uone kama watakuelewa. Na kama huoni umuhimu wa wazazi basi maisha yako yalikuwa boarding school.

Pole sana mke anauma hasa ukiwaangalia watoto wanapomkosa mama yao. Ila jitahidi kuwa strong maisha yaendelee kwa faida ya watoto vinginevyo utawaacha kwenye ulimwengu wa peke yao.
Watoto wakikua wataelewa , halafu kwao ni rahisi sana ku move on,
Kuna baadhi yetu wanawake zetu ni mihimili flani ya mipango yetu , akiondoka unakuta hata baadhi ya mambo yanafeli.
Imagine mke anajua hadi biashara zako na wadeni wako na hadi mambo sensitive halafu aondoke ndo kinachompata mtoa mada , ni hali ngumu sana .
 
Shida si kukubali, inategemea bna personal attachment na huyo aliyeondoka., Mchango wake kwako watoto na kadhalika, kuna wenza uwepo wao nibzaidi ya nyota kwako, mnafanya mambo mengi ya maendeleo naye mnalala naye na pengine ni msiri wako wa ndani, huyu akiondoka duniani si rahisi kukubali .
Mzazi kama mzazi , ni rahisi sana ku move on maana kifo kinajulikana .mzazi hulali naye na wala hawezi kukufanyia ya mkeo .

Nb kama hamkufanya chochote cha maendeleo na mkeo , halafu akafariki , ni tofauti . Mtoa mada anaposema hata akiingia chumbani kuwa anasikia harufu ya mkewe maana yake kuwa walifanikiwa kujenga , angekuwa amepanga hilo lisingetokea , maana angehama tu nyumba.
Nikweli kabisa, mtu akishapata mwenza kaoa au kuolewa ule ukaribu wa ndugu au wazazi hupungua hata mawasiliano hupungua, mzazi utawaailiana naye mara 1 au 2 kwa siku lakini mpenzi hata mara mia na haukinai kabisa.

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Hata mi nimemuelewa sana na ni katika vitu vinasononesha sana .
Wazazi tunawapenda na kuwathamini, lakini for the sake of life huwa tunawaacha na kwenda kuanzisha maisha yetu mapya na wenza wetu , . Hiyo ni hatua ya kwanza ya kujiondoa kwao. , Ukiingia kwenye ndoa tayari kunakuwa na maamuzi ya kindoa na wazazi by default wanakuwa wako mbali na kinachoamuliwa au kufanyika kwenye ndoa.
Typical men huwa wanaondoka nyumbani kwa namna moja au nyingine wakiwa na miaka 13 hadi 18, na ndo muda mahusiano ya kindoa yanapoanza .
Hapa nimekuelewa

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
2019 nilifiwa na mke wangu hakika maumivu yake ni mazito, nyumba naiona chungu, ndani hakulaliki, naisikia harufu ya mke wangu mpaka sasa nikiingia ndani nasikia sauti yake.

Mke amefariki amekuachia watoto wadogo 3!

Kwa ambao hamjapitia hii changamoto ombeni sana Mungu awaepushe nayo.

Huu ni mwaka wa 4 lakini bado sijaweza kupata ahueni, nimeenda kwa psychologist lakini wapi.
Polee kwani bado hujapata mke? Si umeshaoa ww
 
Back
Top Bottom