Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Ilibakia kidogo niingie huu msala. Fundi alinitamanisha Kwa kuwa tofali za msingi zillingia nyingi sana so Kwa ndani chooni kulikuwa na shimo kubwa
Self container ndani choo shimo bado ( mr ebo voice)
 
Sijui kwa nini hakuna mtu mwingine aliyewahi kukumbana na kadhia hii ambayo nusura inipe ugonjwa wa moyo!
 
Fundi wa kiswahil usipokuwepo wakat wa kaz.analipua.wachache sana wanafata vigezo.inabdi hata kama huna muda jenga kila unapopata kalikizo unakatumia effectively unakomaa site mwanzo mwisho.
 
Umetumia kanuni ipi ya hesabu iliyokupa jibu kwa hiyo nyumba ni sq 83 na kwa hivyo vipimo ulivyoambatanisha kwenye ramani yako
 
Hamna nyumba utajenga na tofali kiasi hichoo
 
Nimejenga uelekeo wa jua linapochomoza na jua linapozama yaani ilo joto lake full shangwe mchana hakukaliki jua linapiga sebuleni na chumbani kwangu usiku napo hakulaliki.mafundi vimeo sana wanashindwa hata kutoa ushauri
Hapo tatizo ni kiwanja kilivyo kaa au wewe mwenyewe.
 
Nimejenga uelekeo wa jua linapochomoza na jua linapozama yaani ilo joto lake full shangwe mchana hakukaliki jua linapiga sebuleni na chumbani kwangu usiku napo hakulaliki.mafundi vimeo sana wanashindwa hata kutoa ushauri
Nenda wanapouza maua nunua ile miti mikubwa kama vile royal palm, golden palm na ya aina hiyo, pande uelekeo wa kutokea na kuzama jua, itasaidia kuweka kivuli na kupunguza makali ya jua kwenye ukuta wako
 
Mchwa dawa yake ni kumuondoa malkia lakini hayo mambo ya madawa ni kudanganyana kuna watu wenye utaalam wa kuwaondosha mchwa.
Yule malkia sehemu anapoishi pamejengwa na kuimarishwa kiasi kwamba vitu kama moto au kemikali haviwezi kumdhuru. Na kama kwenye kichuguu hujamuondosha malkia basi hujafanya kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…