Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Kuamini mafundi nikiambiwa cement imeisha napiga simu tu inapelekwa bila kufatilia. Kuna siku fundi anapiga simu kuwa wamesimama kazi kwa kuwa cement imeisha inabidi ipelekwe haraka.

Ikabidi niende mwenyewe kuangalia kazi imefikiaje hadi cement kuisha hivo, nilivyofika mafundi wakastuka sana maana hawakutarajia kuniona kwa wakati huo. Ikawa kila ninapoingia kukagua jamaa kama ananizuga ili niache nimsikilize yeye. Nikahisi kitu nikaongeza umakini kuangalia chumba hadi chumba.

Bwana weee! Si nikakuta kuna mifuko 9 ya cement haijatumika wameificha kwenye chumba chooni. Asee jamaa alibabaika sana akakosa la kusema.
Khaaa!! Mkuu ndio hukumtia hata kofi ???
 
hakuna mantiki ya kuweka wiring mbili zaidi ya kuongeza gharama

kinachofanyika ni kuweka 'change over switch' ya kubadili tanesco-solar mle kwenye DB (lile box lenye mifyuzi) na kama solar yako ni Inverterless, hapo utakua unabadili taa, unatoa za AC unaweka za DC ,

kama ni solar ya Inverter hapo hutabadili taa, zaidi fundi ataunga njia zinakazolishwa na solar mle mle kwenye DB kulingana na pendekezo la mteja pindi anapohamisha tanesco to solar

Asante kwa maelezo mazuri. Na solar yenye ukubwa gani naweza kufunga ili kutumia kwenye vifaa vya kawaida kama pasi, TV nk? Umesema hapo nikifunga invertor sina sababu ya kubadilisha taa, maana yake hata vifaa vingine naweza kutumia kwa hiyo solar?

Somo la solar haijanikaa vizuri.
 
Mnaejenga mijumba mikubwa mjitafakari mambo yamebadilika siku hizi hakuna kutembeleana ovyo wala kuishi kwa ndugu kama zamani na watoto wakikua wanakimbilia sehemu nyingine kutafuta maisha ,kwahiyo utabaki na jumba kubwa kama msikiti peke yako
Mi napenda mjumba mkubwa asee mambo ya kubanana hapana...acha hao watoto wasepe
 
Kuamini mafundi nikiambiwa cement imeisha napiga simu tu inapelekwa bila kufatilia. Kuna siku fundi anapiga simu kuwa wamesimama kazi kwa kuwa cement imeisha inabidi ipelekwe haraka.

Ikabidi niende mwenyewe kuangalia kazi imefikiaje hadi cement kuisha hivo, nilivyofika mafundi wakastuka sana maana hawakutarajia kuniona kwa wakati huo. Ikawa kila ninapoingia kukagua jamaa kama ananizuga ili niache nimsikilize yeye. Nikahisi kitu nikaongeza umakini kuangalia chumba hadi chumba.

Bwana weee! Si nikakuta kuna mifuko 9 ya cement haijatumika wameificha kwenye chumba chooni. Asee jamaa alibabaika sana akakosa la kusema.
Eeeheehe ukafanyaje sasa hapo?
 
Hili Jambo ni muhimu. Inabidi tuulize wataalam nisije kurudia kosa.
Kwa sasa,kulingana na mambo ya mgao wa umeme, kuwa na mfumo wa solar ni muhimu sana.
Mfumo wa solar utatumia hiyohiyo wiring kwa mtu mwenye uwezo kwa kuweka inverter na change over switch ili kubadili tanesco/solar, vyote hivyo vitahitaji distribution network mapema ikiwa ni sehemu ya battery,inverter na solar yenyewe.


Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Asante kwa maelezo mazuri. Na solar yenye ukubwa gani naweza kufunga ili kutumia kwenye vifaa vya kawaida kama pasi, TV nk? Umesema hapo nikifunga invertor sina sababu ya kubadilisha taa, maana yake hata vifaa vingine naweza kutumia kwa hiyo solar?

Somo la solar haijanikaa vizuri.
Mfumo wa solar ni pesa yako tu kila kitu unaweza unganisha,
Ila vitu vinavyotumia umeme mkubwa kama pasi,jiko huongeza gharama za solar upande wa battery, solar, inverter na charger controller,
Lakini kwa mfumo rahisi unaweka uthibiti wasitumie hivyo vitu pindi unapotumia solar

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom