Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Kumwamini fundi
na kumwachia pesa
na kujenga bila mimi kumsimamia au kuwepo

Ni kosa kubwa sana kwa mafundi hawa wa sasa hivi.
Materials nilikuwa nanunua mimi mwenyewe na uzuri nina idea za ufundi ilikuwa si rahisi kunidanganya

Wakati naanza ujenzi alikuta tayari nimeshanunua tofali, kokoto na mchanga. Cement na nondo nilikuwa nimeshazilipia tayari hardware ya jirani
 
Haya nyumba hii hapa 83 SQm ,ni matumizi mabaya sana ya akili na pesa kujenga nyumba ya vyumba 3 kwa SQM 150 ama 200 ni poor mind!,mwisho wa siku unatumia gharama kubwa pesa ambayo ilitakiwa uwekeze sehemu nyingine![emoji276],ni maaajabu sana tena sana kwa mtu mwenye kipato cha kati kujenga nyumba ya SQM 150 yenye vyumba 3,kuanzia SQM 150 kuendelea hiyo ni Guest house View attachment 2468926
Ramani za wenzetu mbele huko store kwao sio muhimu kama laundry room ona hapo chumba cha katikati ya jiko na public toilet ni laundry room, mbongo angefanya hiyo iwe ni store

Halafu jiko ni open kitchen saafi kabisa.

Ramani simple na imejitosheleza kwa wale wa kipato cha kawaida inawafaa
 
KOSA KUBWA AMBALO WAJENZI NA WAJENGEWA HUKIFANYA SIKU ZOTE;.
Ni kuharibu nyumba kuanzia kwenye msingi.
Nyumba sio chini ya 96% Tanzania, ujenzi wake umekosewa kuanzia msingi.

Msingi unatakiwa usiwe chini ya 60cm kutoka usawa wa Ardhi.
60cm ni sawa na laini 4 za tofali za nchi 6 au ngazi nne.

Kwani ni makosa kukosea msingi?
Unakosea msingi kwa mfano nyumba ikawa na laini 2 kutoka usawa wa ardhi;
1. Nyumba itapoteza uwiano kati ya msingi, boma na paa

2. Nyumba hukosa mvuto.
3. Mvua inaoonyesha matone yanayodondoka chini hurukia barazani au ukutani na kuharibu rangi.

4. Mara nyingi husababisha nyumba inakuwa fupi hivyo kuwa na joti kalu ndani.

...USHAURI;.Kabla hujaanza ujenzi pata ushauri wa kitalaam
Point muhimu
 
Pia mkumbuke kuzingatia uelekeo wa kuchomoza na kuzama kwa jua wa eneo husika sio kujenga tu kama ramani ilivyo.
Kuna block yangu ipo shambani hapo Mkuranga master bedroom ipo upande jua linapozama kwahiyo lile jua la jioni lote linatandika chumbani hivyo kama unataka kulala vizuri nasubiri hadi saa nne usiku ndio room inakua imepoa.
Panda mti
 
Wewe ndo mshamba kwa kuona uchaguzi wa wenzako wa kishamba wako ndo bora zaidi.

Wewe kama unapenda ndogo ni wewe. Waache wanaopenda kubwa wafanye wakipendacho.
Huyo jamaa anapenda nyumba ndogo kama kilinge
 
Mkuu Naomba ramani PM
Ukipata ni PM na mimi, ila sio kila ramani ipo poa. Kuna moja niliiona ya mkenya nikitukia namtafuta mtaalam atengeze structral drawing na badiliko modification kidogo kukidhi vionjo vyangu. Huwa narndelea kuangalia ipi bora zaidi, mpaka nikianza niwe nimapata hasa bora kuliko
 
kufanya wiring mbili ni nzuri zaidi, Bomba ni moja ila zinapitisha wires za Tanesco na hizo za Solar! Inapendeza zaidi
Yes. Mana kuweka inverter, kuzuia matumizi ya vitu kama pasi umeme ukikatika ni ngumu na italeta usumbufu
 
Kuna makosa kadhaa niliyafanya

1.Nilimuamini chalii mmoja kosa tu kasomea civil engeering nikq mtrust anichoree ramani kisha nikasafiri nje kidogo then nikawa tuma pesa ijengwe sikiwa na shaka coz aliye chora si ni engineer aisee niliporejea Bongo kuitazama lile boma yaan siku rizishwa nalo mosi vyuma vilikiwa vodogo, choo na bafu humo humo

Aisee sitokuja tena kumpa ndugu kazi ya ku deaign ramani au yoyote ile ya kuhusiana na ujenzi ata kama awe amesomea MIT, Oxford, ata Havard
Kosa ni lako, kabla ya kuanza ujenzi ilipaswa uangalie mrejesho wa ramani. Hii ni lazima, hata huyo uliemkabidhi ilipaswa akuhoji vitu flan ili ajue ukubwa wa chumba. Mfano chumba cha watoto unataka vikae vitanda vingapi vya ukubwa gani? Hivyo
 
Siriazi vyumba vitatu sqm 76!! Hapo sasa utakua umejenga nini!!,Hio nyumba itakua haina hewa kabisa na imebanana kila kona.standard vyumba vitatu ni sqm 150 ikiwa spacious inafika 200sqm,hii inaitwa medium size house.

Lakini kila mtu ana mapenzi yake ,kiukweli sipend nyumba yenye vyumba vidogo sana hii ni kutokana na nyumba niliyokulia kwa wazee,kipind hicho nipo form 6 naona kabisa chumba ni kidogo hakina hewa vitu vimebanana nikawa najisemea ikitokea nimefanikiwa kujenga yangu huko badae ntaongeza kidogo ukubwa.ila sio mita 5 hizo ni nyingi labda kwa masta.

Asikuambie mtu kuna raha ya kulala kwenye chumba kikubwa chenye hewa .
Hata hiyo ndogo inajengwa vizuri hewa unapata, unaeeka madilisha ya nguvu ukilala kama upo nje. Wewe unasemea nyumba enzi za wazee wetu vidiridha milango ilikuwa midogo. Hiyo nyumba ya 83 m3 ni kali ukiijulia wapi uiweke na vipi. Nikijenga hiyo hapo mbele naweza fanya midifikation kidogo ili mlango wa kuingilia usianzie dinning.
 
Back
Top Bottom