Ni kwanini licha ya kuwa na Watanzania zaidi ya million 60 bado sura za viongozi wa upinzani ni zilezile?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Hili swali huwa najiuliza sana pasi na kupata majibu. Niwaombe wanabodi kwa utulivu kabisa mnisaidie kujua nini kiini cha hali hii!

Ni takrinani kwenye majimbo mengi yaliyowahi kuongozwa na wapinzani, ni walewale walioongoza huko nyuma wana nafasi kubwa sana ya kugombea tena hizo nafasi na pengine hata kushinda.

Mf. Msigwa , Sugu , Lema , Mbowe , Kiwanga , Wenje , Zito ,Bwege , Mnyika , nk hapo nimeacha tu wale wadada waliojichanganya ambao hawatabiriki Kwa sasa ingawa nao bado wangekuwa hawajajivuruga walikuwa na nafasi kubwa sana za kushinda kwenye majimbo yao.

Hali Iko hivyo pia Kwa baadhi ya vyama juu ya wagombea urais unakuta mgombea ni huyohuyo mihula yote.

Sababu yaweza kuwa nini hasa?
Je
Vyama havina mkakati wa kuibua viongozi wapya?

Je ni Kwa sababu ya ubora wahao viongozi Kwa maana ya kwamba ni bora hawana mbadala?

Je ni Kwa sababu ya kukandamizwa wanaoibukia?

Je ni Kwa sababu ya uwekezaji wao mkubwa ndani ya vyama Kwa hiyo wako hapo kulipwa fadhila?

Au ni jambo la kawaida tu hamna shida.
 
Kabla hujajibiwa na wewe jibu swali.
Kwanini viongozi wa serikali ngazi za juu kama Mawaziri ni walewale?
Teu ,tengua, teua tena watu walewale wakati Watanzania tupo milioni 61.
Tangu awamu ya Kikwete, Magufuli na Samia Mawaziri ni walewale .
 
Hivi unadhani ku train au scouting ya top level ya uongozi wa chama kikubwa kama CHADEMA kinachoogopwa na utawala au chama tawala ni kazi ndogo?.

Huoni mwanzoni au hapo kati walijichanganya wakabeba hadi mapandikizi wa mfumo na chama upande wa pili, wakaishia taarifa zao kuvujishwa au viongozi hao walioingia kimakosa wakawa chanzo chokochoko za migogoro ya ndani ya chama!.

Hata hivo ni pongeze uongozi wa jua CHADEMA kwa kazi nzuri na ngumu ya kukijenga chama pamoja na mazingira magumu wanayoyapitia, ila wakumbuke kuwa giza nene linapotanda wajue kupambazuka kumekaribia!.
 
Hao akina Makamba, Nyerere, Mwinyi, Kikwete, Lowasa, Kawawa, Sokoine na wengine wengi ambao ni warithi wa mababu na mababa zao ndani ya CCM ina maana watanzania tuko watu 30 tu? Pambana na utawala wa kisultani ndani ya CCM ili nchi iendelee, mtoto wa nyoka ni nyoka.
 

Hujiulizi inakuwaje bado chama ni kile kile muda, na wakati kinakaa madarakani kwa shuruti?
 
Angalau huko tunaona watoto wao lkn huku ni walewale
 
Halafu jiulize umetawaliwa na chama kile kile for thanks 60yrs!na royal families zile zile!
Hapana mkuu maana tumeshuhudia Marais na mawaziri wakuu hata makamu wa rais wakitokea pande tofauti tofauti za nchi yetu
 
Kwani kina Wasira, Kinana, Kikwete, Mwinyi etc wamekuwa na sura mpya!
 

Umesahau kujiuliza kwa nini chama tawala ni kile kile. Kwani wamefanya, wanafanya au watafanya kipi kwa nani lini na wapi?
 
Umesahau kujiuliza kwa nini chama tawala ni kile kile. Kwani wamefanya, wanafanya au watafanya kipi kwa nani lini na wapi?
Kwa nini mnakimbizia hoja kwenye chama tawala mi nauliza chanzo mkijibu chanzo inawezekana ni hichohicho na majibu sahihi yakajibu kote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…