Ni kwanini mji wa Moshi hauna taa za barabarani za kuongoza Magari?

Ni kwanini mji wa Moshi hauna taa za barabarani za kuongoza Magari?

Kwa maoni yangu ukikuta Traffic Police yuko katika makutano ya barabara akiongoza magari kwa muda mrefu katika siku, basi ujue sehemu hiyo inahitaji mataa ili kuwa mbadala kwa kuwepo kwa Traffic. Lakini kama kuna eneo linahitajika mataa basi ni vizuri hiyo hoja ikapenyezwa kwa madiwani, nina imani mapato ya mji wa Moshi yanaweza kutenga sehemuya fedha na kununua hayo mataa kwa kushirikiana na TARURA. Arusha walianza kwa kupata ufadhili, hata Moshi inwezekana.
 
Anzeni kuomba kujengewa stend kwanza, inatia aibu
Stend mpya hiyo ujenzi unaendelea... Mkandarasi anadai malipo ya bilioni moja na ushee amalize kazi fasta....
IMG_20210216_233756.jpg
 
Tuombe wakati hela tunazo??

Bilioni 17 zipo tayari na mradi umeshaanza stendi inajengwa karibu na Kiborloni.

Hata hivyo, stendi iliyopo ni nzuri ila inahitaji kuhamishiwa pembeni ya Mji
Stend imeanza na gharama zake ni zaidi ya 21 bilioni mkuu....
IMG_20210216_233756.jpg
 
Michango imara sana.
 
"Ifahamike kuwa mpaka sasa Manispaa ya Moshi ndio manispaa inayoongoza kwa kuwa na mtandao mpana wa barabara ukiondoa majiji machache yalioyopo Tanzania, hii ni kwa mujibu wa TARURA. www.tarura.go.tz



Nini kinashindikana kuziweka hizi taa?"

Mtoa mada kutoa jibu na swali lake kwa wakati mmoja.

Moshi kuna mtandao mzuri sana wa barabara, na ninakubaliana na TARURA na mleta mada.

Mimi binafsi nikitokea, mfano, barabara ya International School nikipita Round about/keep left ya Mahakamani, wakati wa kutoka mjini sina haja tena ya kurudi na njia hiyo maana huko mbele kuna njia si chini ya nne za kutoka.

Hakuna sehemu yenye uhitaji wa mataa kwa mji wa Moshi. Roand about zipo kila Kona, na barabara zimejotosheleza.
Cc
instanbul Moshi ndio inaongoza Kitaifa kuwa na mtandao mpana wa barabara
 
Wakuu imebidi niuize ili nijue.

Ni kwanini mji wa Moshi ambao ndio makao makuu ya Mkoa wa Kilimanjaro hauna taa za kuongozea magari, ili hali miji midogo kama Singida, Shinyanga na Babati naona wameweka taa za kuongoza magari.

Ifahamike kuwa mpaka sasa Manispaa ya Moshi ndio manispaa inayoongoza kwa kuwa na mtandao mpana wa barabara ukiondoa majiji machache yalioyopo Tanzania, hii ni kwa mujibu wa TARURA. www.tarura.go.tz

Nini kinashindikana kuziweka hizi taa?
wanapenda mbege kuliko taa za barabarani
 
Moshi kuna round about kwenye makutano ya barabara kubwa, Hii ndio maana hamna mataa ya kuongozea magari. Round about ni mbadala wa trafic lights.
 
Moshi magari yanajaa kipindi cha Mwisho wa Mwaka Kama mwezi tu.
Kuweka taa barabarani kupoteza rasilimali uweka taa kwa ajiri ya mwezi 1 .
 
Wakuu imebidi niuize ili nijue.

Ni kwanini mji wa Moshi ambao ndio makao makuu ya Mkoa wa Kilimanjaro hauna taa za kuongozea magari, ili hali miji midogo kama Singida, Shinyanga na Babati naona wameweka taa za kuongoza magari.

Ifahamike kuwa mpaka sasa Manispaa ya Moshi ndio manispaa inayoongoza kwa kuwa na mtandao mpana wa barabara ukiondoa majiji machache yalioyopo Tanzania, hii ni kwa mujibu wa TARURA. www.tarura.go.tz

Nini kinashindikana kuziweka hizi taa?
Ni kweli mji wa Moshi hauna taa za barabarani licha ya kuwa mji muhimu unaoiunganisha kanda ya Kaskazini.
Mji huu hauna taa za barabarani kwa sababu zifuatazo:
1. Mpangilio mzuri wa mji. Wengi mtakubaliana na mimi kuwa Moshi ndio mji pekee uliopangiliwa vizuri zaidi..... Njia zote ndani ya mji zinaungana.
2. Mji wa Moshi una mizunguko kwenye maeneo muhimu ya makutano. Mzunguko wa mnara wa mwenge ukitokea au kwenda Arusha, mzunguko wa YMCA unaunganisha njia ya DSM, KCMC, Arusha na kuingia Moshi mjini. Mzunguko wa Clock tower, mzunguko wa Stand ya mboya, mzunguko wa police line.
3. Kuwepo kwa barabara ya njia nne (double roads) katikati ya mji. Magari yanapita mengi kwa wakati mmoja na pia ni rahisi kukatiza kwenye makutano.
4. Mtandao mpana wa barabara. Barabara za Moshi zote zina njia mbadala ikiwa moja itakuwa na foleni na zote zinawezesha kutoka au kuingia mjini.
5. Uelewa mkubwa wa matumizi ya barabara. Wakazi wengi wa Moshi wana uzoefu mkubwa wa kutumia barabara na ni nadra sana kuona "road rage" Moshi. Hata kipindi cha mwezi wa 12 wageni wanapokuwa wengi haijawahi kuwa changamoto.
6. Matumizi ya public transport. Wakazi wengi wa Moshi hutumia zaidi usafiri wa umma (vibasi) kuliko usafiri binafsi. Sio ajabu kukuta tajiri wa moshi akiwa kwenye bajaji akienda ofisini. Hii ni kwa sababu za kiuchumi zaidi 😂
7. Uwepo wa huduma muhimu nje ya mji. Mji wa Moshi sio kila huduma imerundikwa mjini. Huduma nyingi kama mahoteli, hospitali na masoko yako pembeni au nje ya mji.
 
Ni mji wa kishamba sana wakazi wake ni wezi sana
 
Back
Top Bottom