DOKEZO Ni kweli Hospitali ya Taifa Muhimbili kulala kwa siku ni gharama zake ni tsh 50,000?

DOKEZO Ni kweli Hospitali ya Taifa Muhimbili kulala kwa siku ni gharama zake ni tsh 50,000?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kumbuka siyo kila kitu kina linganishwa. Yani Unalinganisha Texas Marekani na Tanzania? Dunia ya kwanza na Dunia ya 100 sijui?

Kipato chetu na chao havilingani, na hata standard za huduma wapatazo ni tofauti na tupatazo hapa kwetu. Na kama ilivyo kwa Tanzania hata marekani raia wengi hawana health insurance kwa sababu hawawezi kuzimudu. Wengi wenye Health Insurance huzipata kupitia kwa waajiri wao kama tu ilivyo hapa kwetu.

Gharama inatokana na package anayo weza kumudu, hata wao siyo suti kwamba one fit all. Ni wachache wanaweza kujinunulia Health Insurance huko Texas Marekani kama tu ilivyo hapa kwetu.

Kuhusu gharama, nadhani wao hupata value of their money, hapa kwetu hakuna kitu, kila kukicha NHIF wana hamisha magoli, utasikia utapata vipimo vya awali vya damu, vipimo zaidi utalipia, au utasikia huduma za tiba ya mionzi na uchunguzi wa mionzi utajilipia. Lakini utakuta wenzetu kule hizo huduma za uchunguzi wanapata zote kwenye basic package isipokuwa specialized procedures ndizo wanabidi wajipange.

Na hata hivyo wao sheria inawasaidi, mgonjwa hanyimwi huduma hata kam ahwezi kumudu, huduma atapata, deni litapelekwa kwa serikali.

Muhusika atakua na deni lakini halitomfanya ashindwe kuishi maisha yake, kwa maana nyingine siyo lazima alipe.

Hapa kwetu Insurance gharama iko juu sana ukilinganisha na vipato vya wananchi waliowengi. Sioni kama ni sawa kulinganisha gharama anazolipa mwananchi wa Texas marekani na hapa kwetu.
Hawa ndio Watanzania wasomi na wasafiri tunapata mawazo ya Kipato cha USA analinganisha na Tanzania aisee kama Nchi tuna safari ndefu sana.
 
Gharama kubwa halafu huduma mbovu.Halafu kunavichaa wanaendelea kumsifu huyo bibi Yao kuwa anaupiga mwingi.
 
Wakati huo huo Viongozi wa nchi wanatibiwa nje kwa gharama za mamilioni ya shilingi zinatokana na kodi za Watanzania maskini.
Ina maana tunakokwenda kila mtu ajijue!
 
1.Ndio ni elfu 50,000/=
2.ni kweli kama taifa hatupo salama Kwa mambo mengi si tu,gharama za hospitali-----bajeti ya ofisi ya mkuu wa wilaya ni mara 10 ya bajeti ya hospitali ya wilaya
3.Tanzania ni zaidi ya jehenamu
4.Ndio watanzania zaidi ya 90%ni masikini ila baa na makasino yanajaa,sigara zinanunuliwa,shisha zinavutwa,harusi zinachangiwa na hio hospitali ulioitaja huwa inajaaga hatakitanda hakuna
Umeandika ujinga mtupu #4. Hiyo ni kebehi kwa binadamu
 
Nope Tatizo watu hamtaki Kuambiwa Ukweli..
Hivi unajua Uendeshaji wa Hospitali Unachukua gharama Kiasi gani?
Unajua manunuzi ya Dawa yanachukua Gharama kiasi gani?
Malipo ya Vifaa tiba, Umeme, Maji na Bidhaa Vingine hospitali vinagharimu kiasi gani?

Tunapolalamika Tukumbuke Kuwa Hospitali Zinajiendesha Zenyewe na wala Hazina Ruzuku Kutoka Serikalini
Wizara ya AFya, bajeti yake huwa kuwa kuhusu nn na fedha hupelekwa wapii?
 
Wizara ya AFya, bajeti yake huwa kuwa kuhusu nn na fedha hupelekwa wapii?
Hilo ni swala gumu kulijibu maana ili nilijibu lazma niwe mwanasiasa huwa mnaambiwa kila Siku msome bajeti mjue wanaweka Nini na Zinahusika na nini
 
Hapo achana na safari zake za kusafiri na kijiji cha watu nje ya nchi ambazo ni bilions of money hutumika,serikali kutumia tsh bilion 500 kwa mwaka kununua magari ya mafisadi wanajiita viongozi.

Halafu ujakaa sawa unasikia mtu mishipa ya shingo inamtoka kwenye usimba na Yanga.

Tena bila kusahau wao viongozi(kwangu mimi ni matapeli na wahuni) wakiumwa hukimbilia kutibiwa nje ya nchi kwa kodi zetu.Magufuli simkubali ila chuma kilifia mzena nchini TZ akiwa rais wa nchi.

Ikiwa huduma bora za afya ni jukumu la serikali yoyote duniani kwa wananchi wake tena iwe bure au kwa gharama ndogo sana lakini Tanzania serikali inakwepa wajibu wake,Bado unajiuliza kuna jehanamu au unakubaliana na mimi jehanamu ni Tanzania.

Nachelea kusema hii nchi tuliwakabidhi madaraka hakuna mwenye uchungu nayo wote ni wabinafsi hakuna cha TISS wala cha mahakama.

Uzi tayari.
 
Hapo achana na safari zake za kusafiri na kijiji cha watu nje ya nchi ambazo ni bilions of money hutumika,serikali kutumia tsh bilion 500 kwa mwaka kununua magari ya mafisadi wanajiita viongozi.

Halafu ujakaa sawa unasikia mtu mishipa ya shingo inamtoka kwenye usimba na Yanga.

Bado unajiuliza kuna jehanamu au unakubaliana na mimi jehanamu ni Tanzania.

Uzi tayari.
"Any government is an organ of exploitation by nature."
Mikhail Bukanin
 
Hapo achana na safari zake za kusafiri na kijiji cha watu nje ya nchi,serikali kutumia bilion 500 kwa mwaka kununua magari ya mafisadi wanajiita viongozi.

Halafu ujakaa sawa unasikia mtu mishipa ya shingo inamtoka kwenye usimba na Yanga.

Bado unajiuliza kuna jehanamu au unakubaliana na mimi jehanamu ni Tanzania.

Uzi tayari.
Watakuambia serikali sikivu ya dr wao haijafanya watu waugue,na kwamba suala la kuugulia hospitali ama nyumbani ni suala la mtu binafsi.
 
Huduma bora za afya ni wajibu na jukumu la serikali lakini Tanzania wanalikwepa hili jukumu
Kimsingi ni kweli haliwahusu kwa sababu hata wao wenyewe wakiugua hata homa ya mafua au kipandauso huwa wanaenda kutibiwa nje ya nchi kwenye nchi zilizoendelea za Ulaya, Marekani au India. Sasa kwa nini unataka watoe huduma bora za afya hapa Tanzania wakati wao wenyewe hawatibiwi kwenye hizi hospitali za hapa nchini?
 
Kimsingi ni kweli haliwahusu kwa sababu hata wao wenyewe wakiugua hata homa ya mafua au kipandauso huwa wanaenda kutibiwa nje ya nchi kwenye nchi zilizoendelea za Ulaya, Marekani au India. Sasa kwa nini unataka watoe huduma bora za afya hapa Tanzania wakati wao wenyewe hawatibiwi kwenye hizi hospitali za hapa nchini?
Tatizo sio kutibiwa nje hilo kwangu halina shida tatizo wanatibiwa kwa kodi,fedha na mali umma.
 
Tatizo sio kutibiwa nje hilo kwangu halina shida tatizo wanatibiwa kwa kodi,fedha na mali umma.
Umma wenyewe umezubaa, Sasa kwa nini Wajanja wasitumie hiyo nafasi katika kujinufaisha? Siku zote wajinga ndio waliwao! Whether we like it or not, but it is a bitter truth!
 
Back
Top Bottom