Ni kweli kuwa Shaka ni mpwa wa Rais Samia? Na kama ni kweli CCM mmebariki nepotism hii ndani ya chama?

Ni kweli kuwa Shaka ni mpwa wa Rais Samia? Na kama ni kweli CCM mmebariki nepotism hii ndani ya chama?

Ni mpwa au sio mpwa?
Watu wengine mnashangaza Sana mawazo yenu na namna mnavyofikiri, kwa hiyo akiwa mpwa wa Rais haruhusiwi kuwa kiongozi? Akiwa mpwa wa Rais anakuwa amekosa sifa za kuwa kiongozi? Akiwa mpwa wa Rais Hana haki ya kuteuliwa ? Kwa hiyo akili yako na mawazo yako maana yake mpaka leo George bush au Uhuru kenyata wasingefika walipo kiuongozi na kuwa Marais wa nchi zao kwa kuwa baba zao walikuwa Ni marais,. Hillary Clinton asingefika alipofika kiuongozi kwa kuwa mume wake alikuwa Rais. Acha mawazo mfu na ya kizamani, kinachoangaliwa ndani ya CCM Ni uwezo wa mtu kiuongozi katika kumudu mujukumu ya nafasi husika pamoja na sifa alizonazo kiuongozi kiujuzi kielimu kiuzoefu kitaaluma na mambo mengine Kama hayo. Ndani ya CCM haiangaliwi Dini ya mtu au kabila la mtu au ukoo wa mtu au fedha za mtu au sura ya mtu au ukanda wa mtu.Hakuna ubaguzi wa aina hiyo ndani ya CCM na ndio maana CCM inaendelea kuungwa mkono na mamillion ya watanzania na kuwa kimbilio la wanyonge,. Ndani ya CCM yeyote anaweza kuwa kiongozi ikiwa amekidhi sifa na vigezo vya nafasi anayoomba bila kujari Hali yake ya kiuchumi,hakuna ubaguzi ndani ya CCM ndio maana watu wanatimiza ndoto zao bila shida yoyote Ile Wala vizingiti vya kibaguzi Kama ilivyo katika vyama vingine.
 
Ridhiwani ni mtoto wa Kikwete rais mstaafu, Salma mama yake Riz1. Hussein ni mtoto wa mwinyi, Karume nao baba na mwana Marais. Sasa ajabu ya samia na Shaka iko wapi?
Daah! Utanifanya niikimbie nchi hii. CCM adui wa haki.
 
Tatizo lenu hamna akili ya kuelewa hoja ya mleta mada.

Mleta mada Sexless anazungumzia nepotism. Je, mnaelewa maana ya nepotism au mnakurupuka tu mifano yenu isiyokuwa na kichwa wala miguu.
Unatoa mfano wa George Bush Junior, Uhuru Kenyatta, Hussein Mwinyi nk. Je, George Bush Junior aliteuliwa na baba yake kugombea urais wa Marekani?
Je, Uhuru Kenyatta aliteuliwa na baba yake marehemu Jomo Kenyatta kugombea urais wa Kenya? Au Hussein Mwinyi aliteuliwa na baba yake Ali Hassan Mwinyi kugombea urais wa Zanzibar?

Jibu ni dogo na rahisi. Hapana. Sababu wakati wanagombea urais wazazi wao hawakuwepo madarakani.
Lakini, kwa issue ya Shaka ni tofauti. Samia yupo madarakani kama Rais na mwenyekiti wa chama halafu anamteua ndugu yake kushika wadhifa mkubwa ndani ya chama, hiyo ndiyo inaitwa "nepotism", kupeana nafasi za kazi au kupandishana vyeo au kuteuana kindugu. Hii ndiyo hoja ya mleta mada.

Sasa turudi kwenye hoja ya msingi, Je, Shaka, ni kweli ni mpwa wa rais Samia?

Na kama ni kweli, Je, uteuzi wake siyo nepotism??
Shaka yupo kwenye duru za CCM/ UVCCM kabla wewe hujaingia JF na kutengeneza account yako. Ni kwamba tu Mwendazake aliwavuruga mwaka 2016.
 
kinachoangaliwa ndani ya CCM Ni uwezo wa mtu kiuongozi katika kumudu mujukumu ya nafasi husika
Kwahiyo uwezo wa kiuongozi wa paymaster general (mpwa wa JPM) Dotto James ulifika mwisho mara tu Magufuli alipofariki?

Uwezo na umahiri wa kiuongozi wa mpwa wa Magufuli Herry James ulofika mwisho baada tu ya Magufuli kufariki?

Unapoleta kioja huku JF uwe umejipanga ndugu. Huku siyo Facebook.
 
Kwahiyo uwezo wa kiuongozi wa paymaster general (mpwa wa JPM) Dotto James ulifika mwisho mara tu Magufuli alipofariki?

Uwezo na umahiri wa kiuongozi wa mpwa wa Magufuli Herry James ulofika mwisho baada tu ya Magufuli kufariki?

Unapoleta kioja huku JF uwe umejipanga ndugu. Huku siyo Facebook.
Kwani hao wapo wapi kwa Sasa? Nafasi walizo nazo kwa Sasa hazitoshi kuwatumikia watanzania? Ulitaka wapewe nafasi zipi ili moyo wako uridhike?
 
Tatizo lenu hamna akili ya kuelewa hoja ya mleta mada.

Mleta mada Sexless anazungumzia nepotism. Je, mnaelewa maana ya nepotism au mnakurupuka tu mifano yenu isiyokuwa na kichwa wala miguu.
Unatoa mfano wa George Bush Junior, Uhuru Kenyatta, Hussein Mwinyi nk. Je, George Bush Junior aliteuliwa na baba yake kugombea urais wa Marekani?
Je, Uhuru Kenyatta aliteuliwa na baba yake marehemu Jomo Kenyatta kugombea urais wa Kenya? Au Hussein Mwinyi aliteuliwa na baba yake Ali Hassan Mwinyi kugombea urais wa Zanzibar?

Jibu ni dogo na rahisi. Hapana. Sababu wakati wanagombea urais wazazi wao hawakuwepo madarakani.
Lakini, kwa issue ya Shaka ni tofauti. Samia yupo madarakani kama Rais na mwenyekiti wa chama halafu anamteua ndugu yake kushika wadhifa mkubwa ndani ya chama, hiyo ndiyo inaitwa "nepotism", kupeana nafasi za kazi au kupandishana vyeo au kuteuana kindugu. Hii ndiyo hoja ya mleta mada.

Sasa turudi kwenye hoja ya msingi, Je, Shaka, ni kweli ni mpwa wa rais Samia?

Na kama ni kweli, Je, uteuzi wake siyo nepotism??
Wengi hawajui Kiingereza.

Shaka anaweza kuwa ndugu yake Samia, na Shaka akawa kiongozi ndani ya chama au Serikali, na ikawa haina tatizo. Lakini kama Shaka ni ndugu yake Rais Samia, halafu Samia akamteua Zhaka kumpa madaraka, hilo ni kosa kubwa kimaadili.

Watu kadhaa wamechangia mada bila hata ya kuelewa hoja. Eti wanafananisha Kikwete, Salma na Ridhiwan. Nadhani ni kwa sababu ya upeo na uelewa mdogo.

Kikwete hakumteua Ridhiwani wala Salma. Mwinyi hakumteua Hussein, wala marehemu mzee Jomo Kenyata hakumteua uhuru.
 
Kwani hao wapo wapi kwa Sasa? Nafasi walizo nazo kwa Sasa hazitoshi kuwatumikia watanzania? Ulitaka wapewe nafasi zipi ili moyo wako uridhike?
Kwann walitumhuliwa kule walikokuwa? Dotto James alikuwa ameatamia mihela ya nchi na Herry James alikuwa anakinyaga chama. Kwann waliondolewa mara baada ya mjomba wao kufariki???

Na hata shaka siku Samia akiondoa mguu ikulu atapeperushwa kama unyoya. Yangu macho. Acha kutetea ujinga.
 
Kwann walitumhuliwa kule walikokuwa? Dotto James alikuwa ameatamia mihela ya nchi na Herry James alikuwa anakinyaga chama. Kwann waliondolewa mara baada ya mjomba wao kufariki???

Na hata shaka siku Samia akiondoa mguu ikulu atapeperushwa kama unyoya. Yangu macho. Acha kutetea ujinga.
Acha ramli na ndoto
 
Niko Zanzibar kutafuta namna ya kuufanya mkono uende kinywani. Katika stori mbili tatu mwenyeji wangu kagusia kuwa Shaka ni mpwa wa rais Samia.

Nimestushwa sana na hiyo kitu ambayo mwenyeji wangu ananiambia kuwa kwa hapa Zanzibar inajulikwna na kila mtu.

Hebu ndugu wadau nijuzeni. Habari hii nanyi mnayo? Mbona hamuisemi? Ina afya kwa chama na taifa? Kwann haikemewi ndani na nje ya chama? Kwann tunaruhusu nepotism hii?

Jiwe alimuweka mpwa wake kuwa paymaster general. Tukapiga kelele kwa pamoja japo hatukufanikiwa kuzibua masikio ya yule bwana. Sasa mbona huyu mama mwamnyamazia ?

NYONGEZA........,................
Nepotism ni mbaya, inaudhi wengi na inaminya haki na fursa za walio wengi. Alipofariki Rais Magufuli wapwa zake Hery James (alikuwa paymaster general) na Dotto James (alikuwa mwenyekiti UVCCM) walifukuzwa kwenye nyadhifa zao nyeti na kupewa vyeo vya kufutia machozi. Nikadhani wanaccm mmejifunza. Sasa mbona mnarudia makosa?
Kwa wazanzibar kuwa ndg inawezekana. Maana wazenji waliosomasoma karibu wote ni ndugu.

Sioni kama kuna tatizo katika hilo ili mradi tu awe sifa stahiki. Mbaya ni kuteua wasio na sifa kwa kigezi cha undugu au kujuana!
 
Sifa hizo zimeonekana baada ya Samia kuingia ikulu?
Mkuu sijasema kwamba ana sifa. Nimesema ilimradi awe na sifa stahiki.
Sasa kama anazo au hana, waliomteua ndio wanajua.
Na kama hata aliyemteua naye hana sifa, basi hapo ni ngoma droo!

Muhimu ni kutengeneza njia ili watoto, wapwa, wajukuu nk, na wao wasijekulalamika kama mtoa hoja. Nepotism haiwezi kuisha
 
Shaka ndiyo nani wengine huku vijijini nishida kupata taarifa zote za mjini[emoji29]
 
Niko Zanzibar kutafuta namna ya kuufanya mkono uende kinywani. Katika stori mbili tatu mwenyeji wangu kagusia kuwa Shaka ni mpwa wa rais Samia.

Nimestushwa sana na hiyo kitu ambayo mwenyeji wangu ananiambia kuwa kwa hapa Zanzibar inajulikwna na kila mtu.

Hebu ndugu wadau nijuzeni. Habari hii nanyi mnayo? Mbona hamuisemi? Ina afya kwa chama na taifa? Kwann haikemewi ndani na nje ya chama? Kwann tunaruhusu nepotism hii?

Jiwe alimuweka mpwa wake kuwa paymaster general. Tukapiga kelele kwa pamoja japo hatukufanikiwa kuzibua masikio ya yule bwana. Sasa mbona huyu mama mwamnyamazia ?

NYONGEZA........,................
Nepotism ni mbaya, inaudhi wengi na inaminya haki na fursa za walio wengi. Alipofariki Rais Magufuli wapwa zake Hery James (alikuwa paymaster general) na Dotto James (alikuwa mwenyekiti UVCCM) walifukuzwa kwenye nyadhifa zao nyeti na kupewa vyeo vya kufutia machozi. Nikadhani wanaccm mmejifunza. Sasa mbona mnarudia makosa?
Mbona wamejazana kifamilia huko.
 
Back
Top Bottom