Son of Gamba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2012
- 4,720
- 6,957
Asante mkuu.Wengi hawajui Kiingereza.
Shaka anaweza kuwa ndugu yake Samia, na Shaka akawa kiongozi ndani ya chama au Serikali, na ikawa haina tatizo. Lakini kama Shaka ni ndugu yake Rais Samia, halafu Samia akamteua Zhaka kumpa madaraka, hilo ni kosa kubwa kimaadili.
Watu kadhaa wamechangia mada bila hata ya kuelewa hoja. Eti wanafananisha Kikwete, Salma na Ridhiwan. Nadhani ni kwa sababu ya upeo na uelewa mdogo.
Kikwete hakumteua Ridhiwani wala Salma. Mwinyi hakumteua Hussein, wala marehemu mzee Jomo Kenyata hakumteua uhuru.
Hapana siyo mpwa wa RaisHujajibu swali la msingi, na swali ni hili:
Je, Shaka ni "mpwa" wa Rais Samia??
Tupe jibu hilo halafu tuanzie hapo mjadala wetu.
Jibu swali ni mpwa au si mpwa ,huko kote unazunguka ni ngonjera si ajabu mnafeli mitihani!Haijalishi kama ni mpwa au wana uhusiano gani, kinachoangaliwa ni weledi wa mtu aliyeshika nafasi husika.
Kama Shaka ana vigezo vya kushika nafasi yake na kachaguliwa kihalali hapo kuna shida gani?
Kama Samia ana sifa za kushika wadhifa alionao na kachaguliwa kihalali hilo nalo lina shida gani?
Ingekuwa mtu kapewa nafasi kwa kigezo cha undugu pekee ilhali hana sifa za kushika nafasi hiyo hilo lingeleta shida.
Mkuu, acha chuki ziso msingi.Jibu swali ni mpwa au si mpwa ,huko kote unazunguka ni ngonjera si ajabu mnafeli mitihani!
Swali la msingi ni kuwa Shaka ana sifa za kushika wadhifa alio nao au la?Tatizo lenu hamna akili ya kuelewa hoja ya mleta mada.
Mleta mada Sexless anazungumzia nepotism. Je, mnaelewa maana ya nepotism au mnakurupuka tu mifano yenu isiyokuwa na kichwa wala miguu.
Unatoa mfano wa George Bush Junior, Uhuru Kenyatta, Hussein Mwinyi nk. Je, George Bush Junior aliteuliwa na baba yake kugombea urais wa Marekani?
Je, Uhuru Kenyatta aliteuliwa na baba yake marehemu Jomo Kenyatta kugombea urais wa Kenya? Au Hussein Mwinyi aliteuliwa na baba yake Ali Hassan Mwinyi kugombea urais wa Zanzibar?
Jibu ni dogo na rahisi. Hapana. Sababu wakati wanagombea urais wazazi wao hawakuwepo madarakani.
Lakini, kwa issue ya Shaka ni tofauti. Samia yupo madarakani kama Rais na mwenyekiti wa chama halafu anamteua ndugu yake kushika wadhifa mkubwa ndani ya chama, hiyo ndiyo inaitwa "nepotism", kupeana nafasi za kazi au kupandishana vyeo au kuteuana kindugu. Hii ndiyo hoja ya mleta mada.
Sasa turudi kwenye hoja ya msingi, Je, Shaka, ni kweli ni mpwa wa rais Samia?
Na kama ni kweli, Je, uteuzi wake siyo nepotism??
Ndani ya CCM nzima ni Shaka peke yake ndiye mwenye sifa za kushika nafasi hiyo?Swali la msingi ni kuwa Shaka ana sifa za kushika wadhifa alio nao au la?
Kama hana hapo tunasema ni ‘Nepotism’ na tutaikemea vikali, ila kama anazo hilo lina shida gani Mtanzania mwenzangu.
Swali liwe Shaka anazo sifa za kuwa katibu mwenezi au hana?
Usifikie hitimisho kuwa ni nepotism ilhali hatujajua kama Ndugu Shaka Hamdu Shaka anazo sifa au la.
Mkuu ili twende sawa naomba unijibu.Ndani ya CCM nzima ni Shaka peke yake ndiye mwenye sifa za kushika nafasi hiyo?
Tena sifa hizo amezipata baada tu ya huyo "mpwa" wake kuwa Rais??
Sijawahi kumfanyia vetting wala kushuhudia akifanyiwa vetting hivyo siwezi kusema kama ana sifa au la.Mkuu ili twende sawa naomba unijibu.
Sifa anazo au la?
Vizuri sana, basi tufuate ile kanuni “No research, no right to speak”Sijawahi kumfanyia vetting wala kushuhudia akifanyiwa vetting hivyo siwezi kusema kama ana sifa au la.
Samia ni jinsia ya KE anawezaje kuwa mpwa? au mimi ndo sijui kiswahiliNiko Zanzibar kutafuta namna ya kuufanya mkono uende kinywani. Katika stori mbili tatu mwenyeji wangu kagusia kuwa Shaka ni mpwa wa rais Samia.
Nimestushwa sana na hiyo kitu ambayo mwenyeji wangu ananiambia kuwa kwa hapa Zanzibar inajulikwna na kila mtu.
Hebu ndugu wadau nijuzeni. Habari hii nanyi mnayo? Mbona hamuisemi? Ina afya kwa chama na taifa? Kwann haikemewi ndani na nje ya chama? Kwann tunaruhusu nepotism hii?
Jiwe alimuweka mpwa wake kuwa paymaster general. Tukapiga kelele kwa pamoja japo hatukufanikiwa kuzibua masikio ya yule bwana. Sasa mbona huyu mama mwamnyamazia ?
NYONGEZA........,................
Nepotism ni mbaya, inaudhi wengi na inaminya haki na fursa za walio wengi. Alipofariki Rais Magufuli wapwa zake Hery James (alikuwa paymaster general) na Dotto James (alikuwa mwenyekiti UVCCM) walifukuzwa kwenye nyadhifa zao nyeti na kupewa vyeo vya kufutia machozi. Nikadhani wanaccm mmejifunza. Sasa mbona mnarudia makosa?
Elewa hivyo hivyoSamia ni jinsia ya KE anawezaje kuwa mpwa? au mimi ndo sijui kiswahili
Awe na vigezo au asiwe na vigezo bado swali la msingi linabakia pale pale.Vizuri sana, basi tufuate ile kanuni “No research, no right to speak”
Turejee kwenye makablasha tupate kumjua vizuri huyu bwana Shaka.
Kwa maandiko haya sina shaka kwamba ni aidha una chuki binafsi na CCM au na Samia au na Shaka au wote kwa pamoja.Awe na vigezo au asiwe na vigezo bado swali la msingi linabakia pale pale.
Je, vigezo vya Shaka vimeonekana baada ya mpwa wake kuwa Rais??
Lete majibu acha porojo. Tunajadili hoja ya "nepotism", mambo ya chuki binafsi hayo ni yako.Kwa maandiko haya sina shaka kwamba ni aidha una chuki binafsi na CCM au na Samia au na Shaka au wote kwa pamoja.
sijaelewa na siwezi kuelewa kama haujanielewesha.Elewa hivyo hivyo
Lipia basi mkuu. Elimu ni ghali.sijaelewa na siwezi kuelewa kama haujanielewesha.
Ni Kweli. Na baadae atakua mbarazaNiko Zanzibar kutafuta namna ya kuufanya mkono uende kinywani. Katika stori mbili tatu mwenyeji wangu kagusia kuwa Shaka ni mpwa wa rais Samia.
Nimestushwa sana na hiyo kitu ambayo mwenyeji wangu ananiambia kuwa kwa hapa Zanzibar inajulikwna na kila mtu.
Hebu ndugu wadau nijuzeni. Habari hii nanyi mnayo? Mbona hamuisemi? Ina afya kwa chama na taifa? Kwann haikemewi ndani na nje ya chama? Kwann tunaruhusu nepotism hii?
Jiwe alimuweka mpwa wake kuwa paymaster general. Tukapiga kelele kwa pamoja japo hatukufanikiwa kuzibua masikio ya yule bwana. Sasa mbona huyu mama mwamnyamazia ?
NYONGEZA........,................
Nepotism ni mbaya, inaudhi wengi na inaminya haki na fursa za walio wengi. Alipofariki Rais Magufuli wapwa zake Hery James (alikuwa paymaster general) na Dotto James (alikuwa mwenyekiti UVCCM) walifukuzwa kwenye nyadhifa zao nyeti na kupewa vyeo vya kufutia machozi. Nikadhani wanaccm mmejifunza. Sasa mbona mnarudia makosa?
Mkuu nimekuuliza unafahamu CV ya Ndugu Shaka?Lete majibu acha porojo. Tunajadili hoja ya "nepotism", mambo ya chuki binafsi hayo ni yako.