Ni kweli kuwa Shaka ni mpwa wa Rais Samia? Na kama ni kweli CCM mmebariki nepotism hii ndani ya chama?

Asante mkuu.
 
Jibu swali ni mpwa au si mpwa ,huko kote unazunguka ni ngonjera si ajabu mnafeli mitihani!
 
Jibu swali ni mpwa au si mpwa ,huko kote unazunguka ni ngonjera si ajabu mnafeli mitihani!
Mkuu, acha chuki ziso msingi.

Swali msingi ni kuwa aidha Shaka kapewa nafasi ile kwa weledi, Ujuzi, Uzalendo na uzoefu wake au kapewa tu ati kisa ni mpwa Rais?

Kama kapewa kwakuwa na sifa basi swali la pili halina msingi wowote.

Tusichokitaka ni mtu kupewa nafasi ya kuongoza ilhali hana sifa na ati kisa tu ana undugu na kiongozi fulani.
 
Swali la msingi ni kuwa Shaka ana sifa za kushika wadhifa alio nao au la?

Kama hana hapo tunasema ni ‘Nepotism’ na tutaikemea vikali, ila kama anazo hilo lina shida gani Mtanzania mwenzangu.

Swali liwe Shaka anazo sifa za kuwa katibu mwenezi au hana?

Usifikie hitimisho kuwa ni nepotism ilhali hatujajua kama Ndugu Shaka Hamdu Shaka anazo sifa au la.
 
Ndani ya CCM nzima ni Shaka peke yake ndiye mwenye sifa za kushika nafasi hiyo?
Tena sifa hizo amezipata baada tu ya huyo "mpwa" wake kuwa Rais??
 
Ndani ya CCM nzima ni Shaka peke yake ndiye mwenye sifa za kushika nafasi hiyo?
Tena sifa hizo amezipata baada tu ya huyo "mpwa" wake kuwa Rais??
Mkuu ili twende sawa naomba unijibu.

Sifa anazo au la?
 
Sijawahi kumfanyia vetting wala kushuhudia akifanyiwa vetting hivyo siwezi kusema kama ana sifa au la.
Vizuri sana, basi tufuate ile kanuni “No research, no right to speak”

Turejee kwenye makablasha tupate kumjua vizuri huyu bwana Shaka.
 
Samia ni jinsia ya KE anawezaje kuwa mpwa? au mimi ndo sijui kiswahili
 
KATIKA KOSA KUBWA LILILO FANYWA NA CHAMA CHANGU CHA CCM, NI KIMPA UENEZI HUYU SHAKA! ile nafasi haimtoshi kabsaaa, tumekabidhi leaner kuindesha ndege ya masafa marefu!! pale inatakiwa tumuweke kijana mwenye uwezo wa kupambana na wapinzani!!
 
Vizuri sana, basi tufuate ile kanuni “No research, no right to speak”

Turejee kwenye makablasha tupate kumjua vizuri huyu bwana Shaka.
Awe na vigezo au asiwe na vigezo bado swali la msingi linabakia pale pale.
Je, vigezo vya Shaka vimeonekana baada ya mpwa wake kuwa Rais??
 
Awe na vigezo au asiwe na vigezo bado swali la msingi linabakia pale pale.
Je, vigezo vya Shaka vimeonekana baada ya mpwa wake kuwa Rais??
Kwa maandiko haya sina shaka kwamba ni aidha una chuki binafsi na CCM au na Samia au na Shaka au wote kwa pamoja.
 
Kwa maandiko haya sina shaka kwamba ni aidha una chuki binafsi na CCM au na Samia au na Shaka au wote kwa pamoja.
Lete majibu acha porojo. Tunajadili hoja ya "nepotism", mambo ya chuki binafsi hayo ni yako.
 
Ni Kweli. Na baadae atakua mbaraza
 
Lete majibu acha porojo. Tunajadili hoja ya "nepotism", mambo ya chuki binafsi hayo ni yako.
Mkuu nimekuuliza unafahamu CV ya Ndugu Shaka?
Ukajibu hufahamu

Sasa kama hujui mtu anazo sifa au la unaanzaje kujadili ‘Nepotism’ mkuu?

Huoni kuwa unafanya udanganyifu wa fikra tunduizi (Fallacies in Logic)?

1. Umefanya ‘Hasty Generalization’ - Huna taarifa za kutosha kuhusu Bwana Shaka ila umehitimisha kuwa kapendelewa ati kisa ana undugu na Rais.

2. Umefanya ‘Post hoc ergo propter hoc’ - Umehisi kuwa ati kwakuwa Samia ni Rais basi ndiyo maana Shaka kawa Katibu Muenezi.

Ndiyo maana nikasema hebu turudi kupitia makablasha yetu tutafute taarifa zaidi za Bwana Shaka tuone kama anazo sifa au kapendelewa.

Pia ikifaa turejee mchakato wa upatikanaji wake je Kanuni za Chama zilivunjwa ilimradi “Mpwa wa Rais” apite au la.

Kabla ya hapo sioni kama tupo kwenye nafasi ya kulisema zaidi, vinginevyo iwe kishabiki tu Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…