Ni kweli Mbowe kachoka, lakini Lissu sio mtu sahihi wa kumwachia chama

Lissu ana siasa za aina ya Hamas, Jamaa Islamiya/Muslim Brotherhood, au Hezbollah, hafai kuongoza chama cha kisiasa
 
Nikiri tu kuwa nilikuwa sijamjua vizuri hadi alipoanza kuwashambulia viongozi wenzake akiwepo boss wake nikajua hamna kitu hapo.
Bas hauko sawa kichwani, Mgombea unamjua ndani ya siku mbili?

Sisi Lissu tunamchagua kwa misimamo yake na mienendi yake tangu enzi za Jakaya Kikwete,

Wewe unamjua ndani ya siku mbili

Unatofaut gani na wale wanaohogwa chumvi ndani ya siku moja wakachagua mtu
 
Kwani uchaguzi wa nini sasa? Si Mbowe asogeze mbele aendelee kuwa mwenyekiti wa milele kama Rais wa China
 
Hata Samia mwanzo tulizani ni tofauti na mwendazake lkn alipoanza kutoa makucha tukajua rangi zake, same na Lissu kabla ya kugeuka tulidhani ni mtu sahihi.
Wewe mienendo ya Lissu umeijua ndani ya siku mbili sio?
 
Nikiri tu kuwa nilikuwa sijamjua vizuri hadi alipoanza kuwashambulia viongozi wenzake akiwepo boss wake nikajua hamna kitu hapo.
Mwanasiasa anayeogopa kushambuliwa hajakomaa

Kushambuliana ndio Siasa na hiyo ni sababu CCM ni Imara sana Kwa sababu hawaogopani 😂
 
Lissu mwenyewe mwanzo alikuwa agombee umakamu ndani ya wiki akasema atagombea uenyekiti.
 
Wajumbe wapo moyoni kwa lisu lakini machoni wapo kwa mbowe ili watafune pesa yake anayogawa sasa kupitia chawa wake akina Mdee, wenje Boniface na wenzao, Lisu atashinda kwa kura nyingi lakini watapora ushindi wake na kumpa mbowe ushindi haramu
 
Wewe mienendo ya Lissu umeijua ndani ya siku mbili sio?
Ni kama Lissu alivyobadili gia angani na kugombea uenyekiti. Mimi ni nani ning'ang'anie maiti nizikwe nayo.
 
Hata Samia mwanzo tulizani ni tofauti na mwendazake lkn alipoanza kutoa makucha tukajua rangi zake, same na Lissu kabla ya kugeuka tulidhani ni mtu sahihi.
Hebu toa sababu moja yakueleweka iliyokufanya uone Lissu hafai hizi siku mbili!?Sababu yenye kashiko.
 
Lissu mwenyewe mwanzo alikuwa agombee umakamu ndani ya wiki akasema atagombea uenyekiti.
Walikubaliana na mbowe kuwa kila mmoja agombee alipo sasa, lakini mbowe akaanza kumfanyia figisu figisu akamwekea wahuni wengi upande wa makamu mwenyekiti huku mtia nia ya Uenyekiti yaani heche akihujumiwa kama Zito, Kwa Hasira Lisu akaona Mbowe anawachezea anawafanya kuwa ni watoto wadogo ndipo kutangaza ghafra kuwa anagombea uenyekiti, alimshitukiza Mbowe, na endapo Mbowe asingefanya aliyofanya mda huu lisu angekuwa yupo kule kule kwa awali
 
Sifa ya sisi watanzania ni wanafiki usipate tabu ukiona mambo kama haya maana tunasoma upepo
Siku moja kwenye siasa ni sawa na mwaka mzima, kwa hiyo minyumbuliko inaruhusiwa kila dakika
 
Mrithi awe Abduli maana amekigharamia sana chama🐼
 
Wajumbe wapo moyoni kwa lisu lakini machoni wapo kwa mbowe ili watafune pesa yake anayogawa sasa kupitia chawa wake akina Mdee, wenje Boniface na wenzao, Lisu atashinda kwa kura nyingi lakini watapora ushindi wake na kumpa mbowe ushindi haramu
Hahaa Lissu atashinda lkn ataporwa ushindi umetumia utafiti upi au ule wa mitandaoni.
 
Kwanini kuwe na watu wawili tu waliochukua form? Wengine hawajiamini? Kama chama tu wanashindwa kichukua form hao watu wanafaa hata kuwa mawaziri kweli?
 
Mbowe hayupo tayari kumuachia mtu hicho chama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…