Ni kweli watoto wa English Medium wana IQ kubwa kuliko wetu kayumba?
Kwenye lishe hapo napo Mungu tu huwa anatusaidia. Mtu anashindia viporo vya ugali alafu kwa kufosi anapata A kayumba, ukimpeleka kama MIT US huko unaweza kukuta ndio wakina Zuckerberg wakibongo, waliofungwa na mazingira
unakuta mtoto wa darasa la sita anaamka mwenyewe anajiandaa anaenda anaenda stendi anachukua usafiri mpaka shule, huyu atakama akipata 40 kwenye masomo ila kuna mambo anijifunza kama time management, kujitegemea ku survive kwenye dunia ngumu kuliko mtoto anae amshwa anakuta kila kitu tayari kaishandaliwa anapelekwa shuleni kwa gari
 
unakuta mtoto wa darasa la sita anaamka mwenyewe anajiandaa anaenda anaenda stendi anachukua usafiri mpaka shule, huyu atakama akipata 40 kwenye masomo ila kuna mambo anijifunza kama time management, kujitegemea ku survive kwenye dunia ngumu kuliko mtoto anae amshwa anakuta kila kitu tayari kaishandaliwa anapelekwa shuleni kwa gari
Ni kumuuza mtoto kuna umri wa kumuandaa kwa hayo ya changamoto

Mtoto mwenye kila kitu huwaza kusoma tu na ndio.maana private wanafaulu sana

Watoto huwawaza masomo tu si shida za daladala, na matusi ya makonda na kusukumwa asipande nk
 
Ndio maana ya kusomesha shule nzuri lishe inakuwa vizuri nk Zuckerberg na akina Billy Gates hawakusoma shule za kayumba

Ubahili kwenye kusomesha shule nzuri mbele kilio
Walisoma shule za maana ndio maana walogundua vipaji vyao mapema wakaacha shule kabisa na kurudi baada ya kuvitekeleza kwa jamii
Sio kayumba mtoto anakimbia Shule kwa sababu mwalimu wa hesabu anachapa sana hahahah. Tutapeleka kwa sababu ya umasikini, na sababu ya kutafuta pesa ihusishe kuwapa watoto mazingira rafiki kwa future yao
 
Ni kumuuza mtoto kuna umri wa kumuandaa kwa hayo ya changamoto

Mtoto mwenye kila kitu huwaza kusoma tu na ndio.maana private wanafaulu sana

Watoto huwawaza masomo tu si shida za daladala, na matusi ya makonda na kusukumwa asipande nk
Unakuta mtoto yuko la nne anamindeset ya baba mwenye wake wawili na watoto sita. Anawaza mambo yaliyo nje ya umri wake. Anaanza kuwanza mawazo ya kuleta chakula nyumbani wakati ni umri wa kuletewa.
 
Sio kweli isipokuwa English medium Wana exposure kubwa ya kufahamu mambo kuliko wa kayumba,kimsingi mtoto wa English medium hufundishwa mada hata wanazosoma kidato cha pili akiwa la kwanza,hakuna mizania iliyo sawa kwenye mfumo wetu wa elimu
 
Kazi ya elimu sio kumuingizia mtu vitu kichwani, kazi ya elimu ni kumsaidia mtoto kuugundua na kuufanyia kazi uwezo alionao.

Shule zetu za Kayumba hazimpi mtoto nafasi ya kuuonyesha na kuuvumbua uwezo alio nao bali mazingira yanamfanya awe mjinga zaidi hata kama anatapa A.

Mazingira ya Shule binafsi idadi chache ya wanafunzi, umakini wa walimu, ufatiliaji wa karibu na chakula bora (boarding) vinakuwa vichocheo vya mtoto kufunguka na kujitambua mapema. IQ yake inahamasishwa na sio kuhafifishwa.


Mimi si mtaalam wa elimu, ila nimesoma mahala hili wazo limenishangaza ila kama nimeelewa.

Nini maoni yako, kuna ukweli wowote
Siku hizi ukubwa wa akili hupimwa kwa kuangalia uwezo wa mtoto kuileta mboga nyumbani

Watoto wa boding na Hao wengine ndiyo wanao ongoza kwa udishi skuhizi
 
Kayumba na English Medium, huwa kipimo chake ni chuo kikuu... Unakuta wa kayumba anahitimu na GPA ya 4.5 na English Medium anahitimu na GPA ya 3.2
 
Mtoto anazaliwa kama computer isiyo na program yoyote! Then anaanza kuwa programmed na wazazi, ndugu na jamaa, then taasisi kama za dini nk, then shule za awali, kati na juu hatimaye chuo.

So formula ni ileile garbage in garbage out, ukimpeleka kayumba atafanana na kayumbaz wenzake, ukimpatia English medium school atapata kinachotolewa huko pia so shule haidetermine IQ au akili ya mtoto ila kila taasisi aliyopita na maarifa waliyompa! Kuna theory ya Nature vs nurture na Piaget tests zinaeleza vizuri sana hii saikolojia na zimefanyiwa utafiti, japo kuna outliers chache sana ambazo hazizidi 1% ya population


 
Kuna mwalimu ni ndugu yangu anafundisha shule ya vipaji (TABORA BOYS) huwa ananiambia kuwa huwa wana utaratibu wa kuwaadhibu wanafunzi waliofanya vibaya hususan wale wa advance,anakwambia kuwa wanafunzi kumi wa mwisho darasan wa HGL,PCM na PCB wengi kama sio wote ukiangalia historia yao wametoka shule private tena kubwa tu,walimu huwa wanajiuliza kwamba hawa wanafunzi wanaofanya vibaya ni kwamba wameshindwa kuendana na mazingira ya shule za umma au huko walikotoka walikuwa spoon feed yaani wanarahisishiwa kila kitu japo IQ zao ni ndogo!!!??? Anasema kuwa wanafunzi wanaochaguliwa shuleni kwao kutoka hizi st kayumba ni vipanga balaa na ndio wanaoshika nafasi za juu darasani,sema kwa upande mwingine hawa wa private anasema ni wazuri mno kwenye debate kutokana na kuwa na msingi waliojengewa kutoka hizo private schools
Hili linaukweli kabisaa!
 
Back
Top Bottom