Ni lini Serikali ya CCM itanunua laptop kwa kila mwanafunzi kuanzia shule za kata?

Hoja chini ya kiwango sana

Una akili ndogo mno hoja ukitoa unatakiwa kuangalia sector yote kwa ujumla ..

Shule za msingi kuna za Serikali na Private

Shule za private za msingi hawana laptop na huongoza mitihani kitaifa Hakuba mwanafunzi mwenye laptop na huwa hazitoi uji wala chakula sana sana utalipia usafiri tu sababu nyingi ni za day pili haziruhusu kabisa overtime kwa walimu wake Kuwa kila mwalimu ahakikishe mshahara analipwa afundishel vizuri ndani ya huo muda no overtime

Tatu hawatati watoto wanaosoma shule zao za private waende tuition yeyote mtaani wanajiamini kuwa wakuchofundisha ndani ya muda wa vipindi inatosha wasije kwenda tuition kuchanganywa bure

Ndio maana sio rahisi kukuta mtoto anasoma shule ya msingi ya private zilizo nyingi akienda tuition au akihitaji Mwakimu amfundishe muda wa ziada na hali shule na hana laptop lakini kitaifa anapata ufaulu mkubwa kitaifa wakati na yeye anasoma day kama yule wa serikalini

Hoja yako dhaifu mno
 
Maofisini tu hazipo ndio apewe kila mwanafunzi!!?? Nchi ya hovyo sana ..... Nchi Zima inatumia mifumo lakini ofinisini hakuna internet hakuna laptops Wala desktops ....ndio ziende Kwa wanafunzi....
Ni Kweli, nayoyaongea ni matazizo ya kimfumo,

Ili mwanafunzi apewe laptop lazima mwalimu awezeshwe kwanza, ofisi iwe na internate, solar na umeme uunganishwe, mwalimu awe trained,

Ndipo mwanafunzi apokee,

Pesa zipo nyingi serikalini, mipango yhabiti ndo hamna,

Na tunakosa vipaumbele, tunaacha vya msingi, tunaenda kununua magoli ya Simba na yanga Kwa 5ml ambayo imeweza kununua mahindi ya kunywesha uji shule moja Kwa mwezi mzima.
 


Shule za kata za mjini zina unafuu tofauti na shule zilizopo district /rural hizi zina pitia matatizo tofauti kidogo ukilinganisha na za mjini.. Walimu wanakosa motisha ya kwenda darasani miundo mbinu ni mibovu sana, umeme hakuna kuna sehemu bado kabisa huyu mwalimu anasaishaje kazi za wanafunzi wake, nyumba za walimu pia ni hakuna au zikiwepo ni zime ezekwa na nyasi, sasa alieishika hii sekta ya elimu kufanya vizuri au vibaya ni mwalimu sasa akiwezeshwa na mengine yanakua ni marahisi
 


Kuna wa form 6, na walio graduate chuo kikuu hawajui kuitumia, nchi kwisha hii.
 
Yote ni mema ,

Pia ni muhimu Serikali ikahakikisha Kila mtoto anapata hapo kikombe kimoja Cha uji Nchi nzima Kwa kuanzia Ili uwepo ushirikiano kati ya mwalimu na mwanafunzi.

Pia in the long-run ziwepo laptops mashuleni Kwa wanafunzi.

Nahisi hili linafanyika watoto wanapewa uji shuleni
 
Kuna wa form 6, na walio graduate chuo kikuu hawajui kuitumia, nchi kwisha hii.
Hata Mimi wakati naingia chuo kikuu, SIKUWAHI kumiliki laptop,Wala smartphone

Bt kuwa na maono mema ni jambo jema.
 
Soma HOJA ya mada hapo juu,

Inauliza " Ni Lini Serikali ya CCM itanunua laptop Kwa Kila mwanafunzi kuanzia shule za kata"

Yapo yanayotakiwa kuanza kutekelezwa Ili in the next 5-10 years tiweze kuwapa laptops wanafunzi saint kayumba!!
 
umeeleza vizuri sana,
nisingependa kueleza zaidi,
lakini ifahamike tu hisia na huruma mlizonazo wananchi wenzangu kwa walimu na hali za madarasa ya wanafunzi katika baadhi ya maeneo ni kweli hayaridhishi,
ni imani yangu serikali inaona na kuskia maoni yenu na inayachukua na kuyachakata na bila shaka itaboresha mazingira hayo kadiri ya upatikanaji wa fedha na elimu yetu itaimarika siku hadi siku...
 
Nahisi hili linafanyika watoto wanapewa uji shuleni
Wangekuwa wanapewa uji Nchi nzima shule za msingi,nisingeandika thread hii,

Baadhi ya shule, wilaya na mikoa kadhaa ndo wamefanikiwa.

Me nachoomba ni Serikali kuja na mfumo wa kufanikisha hili Nchi nzima.
 

Kwa serikali hii ni kupoteza muda kuisubiri ifanye maendeleo kwa nchi.
 

Wanao wanasoma shule gani ya kata hapa nchini?
 
Inapendeza sana mkuu hii inafariji kama kuna wawikilishi wa serikali mnajitolea kukusanya maoni, kujibu maoni, maswali na kufanyia kazi mapendekezo na kuyawekea dira katika nafasi zenu serikalini na kufikisha kwenye ngazi ya kitaifa... Mungu awawezeshe tu na kuwapa uvumilivu na jitihadi binafsi.. maendeleo ni mchakato na hayana chama,

Tukitumia hizi platform vizuri hakika zitaleta chachu, kuna nguvu sana kwenye sauti za wengi kwenye platform kama hizi na tutaweza kuboresha huduma nyingi sana za umma ikiwemo afya, elimu, uchukuzi, michezo, mawasiliano nk umuekua mfano kupokea vipande vya maoni na kuvikiunganisha na vitaleta tija
 
Wangekuwa wanapewa uji Nchi nzima shule za msingi,nisingeandika thread hii,

Baadhi ya shule, wilaya na mikoa kadhaa ndo wamefanikiwa.

Me nachoomba ni Serikali kuja na mfumo wa kufanikisha hili Nchi nzima.
Hivi si kuna wale ward education officers nahisi hilo ndiyo jukumu lao kuzungukia tarafa zao na kuchukua mapendekezo
 
Soma HOJA ya mada hapo juu,

Inauliza " Ni Lini Serikali ya CCM itanunua laptop Kwa Kila mwanafunzi kuanzia shule za kata"
Unaharibu ku force kwa nguvu hoja yako ikubalike badala ya kujenga hoja ya nguvu

Hoja yako imejaa Command utafikiri wewe ndie amiri jeshi mkuu wa Majeshi yote ya Tanzania mjingq wewe

Jenga hoja yenye nguvu wewe

Akili huna jifunze kujenga hoja

Kama upinzani una wajinga wasiojua kujenga hoja kama wewe CCM tutawala milele

Sijadiliani na mjinga kama wewe tena CCM tuna akili tunajielewa mtu akijenga hoja vizuri mbona tutamwelewa hivyo vi command vyako koko mpelekee hawala yako ohhh lini mpuuzi wewe
 
Huna HOJA, nenda kalale!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…